Sakata la Wachimba Visima KM Mkumbo bado hajaeleweka kabisa!

Akilinjema

JF-Expert Member
Aug 9, 2016
11,433
11,747
Amani ya Mwenyezi Mungu aliyeumba Wanadamu wote iwe juu ya kila asomae na kuchangia Mada hii!
Kufuatia sakata la Wachimba visima kutakiwa wajisalimishe na kwenda kulipia tozo husika hali ambayo imeleta taharuki kubwa miongoni mwa jamii kiasi cha Watu kueleza kwa vipi Serikali yenye jukumu la msingi kushindwa kuwapatia huduma muhimu sana ya maji ambayo ndiyo uhai wa mwanadamu Kwa zaidi ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanganyika badala Yake inataka kuwasakama wananchi ambao baada ya kupata shida Kwa miaka mingi ya Kukosa Maji hali iliyopelekea kujiongeza Kwa kuchimba visima vya Maji Kwa matumizi mbalimbali ikiwemo ya majumbani au viwandani n.k?
Taharuki hiyo imepelekea KM Mkumbo kuelezea yafuatayo ;
1. Wenye visima vyenye urefu usiozidi mita 15 hawahusika na malipo
2. Wenye visima visivyozidi urefu mita 15 na visivyokuwa na miundombinu yoyote Kama vile kufungwa pump hawata husika na malipo pia
3; wenye visima vyenye kuzidi zaidi ya mita 15 na walifunga pump hao Ndiyo walosemekana kutakiwa kulipa !

Hoja binafsi :
Kwa kuwa kiwango cha meza ya Maji (water table ) hutofautiana kati ya maeneo flani na mengine je kigezo cha kina cha urefu wa kisima chaweza kuwa na mashiko?
Mwingine akichimba mita 15 hatapata hata tone la Maji hadi achimbe mita 100 ndo atapata Maji Walau kidogo na Kwa urefu huo swala la kufunga pump huwa haliepukiki je alipishwe sababu ya kuishi maeneo ambayo water table iko Chini zaidi ukilinganisha na maeneo mengine?

Ushauri ;
1. Mtu aliyechimba kisima chake Kwa matumizi ya nyumbani/familia alilipishwe kabisa maana Mtu huyu Maji ya Dawasco yangekuwa yapo kwake asingechimba kisima kabisa!
2. Mwenye kisima ambacho hutumika Kwa matumizi ya viwanda/biashara hawa nao wasilipishwe maana wanalipa kodi ya mapato na bila Maji wataweza kufunga kiwanda au biashara husika!

Wanaopaswa kufikiriwa kulipa:
1. Wale walichimba visima exclusively kwaajili ya kuuza Maji Kibiashara na mauzo yao yawe yanazidi shilingi milioni 4 Kwa mwaka hao Walau wanaweza kuchangia kiasi kidogo!

Karibu Kwa majadiliano na michango yenye Tija kwa maendeleo ya Taifa letu!

Alamsiki!
 
Hata mimi swala la visima ni kama bomu akilini mwangu. Hasa kwa wananchi wa vijijini wenye hali ngumu na duni. Hivi ni lazima kweli ?!
 
Ila si wanadai kuanzia futi sita kwenda chini kila kilichopo ni mali ya serikali?

Labda wanatumia logic hiyo.
 
hili la kutaka tozo za visima vya maji ni unyonyaji mkubwa, wanataka waTZ wafe!!!?

maji yao hayana uhakika....mtu unaImprovise ili uSurvive napo wanataka tena kukubana,

hii ni sawa na baba mzazi anakunyima nauli ya bus kwenda shule, unaomba lift unapata...anajua, anakuja anakwambia umpe ela (nauli) uliyoSave baada ya kupanda lift.

pathetic
 
Amani ya Mwenyezi Mungu aliyeumba Wanadamu wote iwe juu ya kila asomae na kuchangia Mada hii!
Kufuatia sakata la Wachimba visima kutakiwa wajisalimishe na kwenda kulipia tozo husika hali ambayo imeleta taharuki kubwa miongoni mwa jamii kiasi cha Watu kueleza kwa vipi Serikali yenye jukumu la msingi kushindwa kuwapatia huduma muhimu sana ya maji ambayo ndiyo uhai wa mwanadamu Kwa zaidi ya miaka 55 ya Uhuru wa Tanganyika badala Yake inataka kuwasakama wananchi ambao baada ya kupata shida Kwa miaka mingi ya Kukosa Maji hali iliyopelekea kujiongeza Kwa kuchimba visima vya Maji Kwa matumizi mbalimbali ikiwemo ya majumbani au viwandani n.k?
Taharuki hiyo imepelekea KM Mkumbo kuelezea yafuatayo ;
1. Wenye visima vyenye urefu usiozidi mita 15 hawahusika na malipo
2. Wenye visima visivyozidi urefu mita 15 na visivyokuwa na miundombinu yoyote Kama vile kufungwa pump hawata husika na malipo pia
3; wenye visima vyenye kuzidi zaidi ya mita 15 na walifunga pump hao Ndiyo walosemekana kutakiwa kulipa !

Hoja binafsi :
Kwa kuwa kiwango cha meza ya Maji (water table ) hutofautiana kati ya maeneo flani na mengine je kigezo cha kina cha urefu wa kisima chaweza kuwa na mashiko?
Mwingine akichimba mita 15 hatapata hata tone la Maji hadi achimbe mita 100 ndo atapata Maji Walau kidogo na Kwa urefu huo swala la kufunga pump huwa haliepukiki je alipishwe sababu ya kuishi maeneo ambayo water table iko Chini zaidi ukilinganisha na maeneo mengine?

Ushauri ;
1. Mtu aliyechimba kisima chake Kwa matumizi ya nyumbani/familia alilipishwe kabisa maana Mtu huyu Maji ya Dawasco yangekuwa yapo kwake asingechimba kisima kabisa!
2. Mwenye kisima ambacho hutumika Kwa matumizi ya viwanda/biashara hawa nao wasilipishwe maana wanalipa kodi ya mapato na bila Maji wataweza kufunga kiwanda au biashara husika!

Wanaopaswa kufikiriwa kulipa:
1. Wale walichimba visima exclusively kwaajili ya kuuza Maji Kibiashara na mauzo yao yawe yanazidi shilingi milioni 4 Kwa mwaka hao Walau wanaweza kuchangia kiasi kidogo!

Karibu Kwa majadiliano na michango yenye Tija kwa maendeleo ya Taifa letu!

Alamsiki!
Ushauri mzuri
 
Yeye kasema tuishi kama mashetani sasa kuna shetani anaoga?

Hahaha huu ni mpango wao wa kutaka pafyumu ya Chibu iuzike. Hii ni kwakua tukikosa maji itabidi tujipulizie pafyum angalau harufu ya ubeberu ikate.

Nipo kwenye mood nzuri sana sasa hivi. Usinichukulie serious
 
Ila si wanadai kuanzia futi sita kwenda chini kila kilichopo ni mali ya serikali?

Labda wanatumia logic hiyo.
no way, wameona watakosa hela za bill ya maji yao yasiyo na uhakika,
kama wangesambaza maji ktk kila nyumba na yakawa na uhakika kuna mtu angehangaika na kuchimba kisima!!

kuchimba kisima napo ni kama mchezo wa pata potea...unless kama utaleta wataalamu wapime kabla uwepo wa maji ambayo hiyo nayo ni gharama nyingine bado ya uchimbaji....haujaweka na vifaa vitakavyotumika ktk uvunaji wa hayo maji,

usisahau kuna umeme utatumika kuvuta hayo maji hadi juu.

hii serikali nashindwa kuielewa, inaacha kukusanya tozo kwenye mambo makubwa yenye hela nyingi na ambayo hayataumiza wananchi wake kama kwenye madini na mafuta inataka kuja kuwaumiza wananchi huku chini.

ili la tozo mimi nalikataa kabisa.
 
Mbona wenye Magari tunalipa kodi wakati kuna Magari ya Serikal?

Wenye Visima nanyi pambaneni Na hali zenu!
 
Gari sio muhimu kwako Ila Ni muhimu Kwa Binadamu Mwenye akili TIMAMU
Kiukweli siamini kama hii id inaweza kufananisha umuhimu wa gari na maji kisha ikaona gari ni muhimu.

Labda na wewe upo high. Who knows!!
 
Kiukweli siamini kama hii id inaweza kufananisha umuhimu wa gari na maji kisha ikaona gari ni muhimu.

Labda na wewe upo high. Who knows!!

Jitahidi Kuwa Na akili Hata Kama huna

Tunafananisha 'ownership' ya Gari Na 'ownership' ya kisima sio maji

Serikali imetoza kodi kisima sio maji Kama ambavyo inatoza kodi gari sio usafiri

Kama Ni kufananisha Basi ningefananisha Maji Na usafir sio maji Na Gari

Kuna tofauti ya maji Na kisima Kama ilivyo kuna tofauti ya gari Na usafiri

Najua hujanielewa
 
Jitahidi Kuwa Na akili Hata Kama huna

Tunafananisha 'ownership' ya Gari Na 'ownership' ya kisima sio maji

Serikali imetoza kodi kisima sio maji Kama ambavyo inatoza kodi gari sio usafiri

Kama Ni kufananisha Basi ningefananisha Maji Na usafir sio maji Na Gari

Kuna tofauti ya maji Na kisima Kama ilivyo kuna tofauti ya gari Na usafiri

Najua hujanielewa
Kiukweli sijakuelewa tangu ulipoamua kusema akili sina.

Kwa kusoma posts zako nimejua kua umenizidi baadhi ya vitu na kujua historia ya nchi yetu.

Na nikafikiri unatakiwa kunizidi busara pia.

Gari ni nini basi kama halifanyi kilicholengwa nacho ambacho ni usafiri?

Kisima kama hakitoi maji je?

Ikiwa hoja yako ni kulipia gari na si usafiri.
Gari lako likiharibika ukalipaki kwa miaka miwili utalilipia road license na tozo zingine?

Ikiwa hoja yako ni tunalipia kisima na siyo maji.
Kama nilichimba kisima ila kimekauka miaka miwili nyuma nitatakiwa kukilipia?

Badala yake umeamua kumuita kila mtu hana akili.
 
Kiukweli sijakuelewa tangu ulipoamua kusema akili sina.

Kwa kusoma posts zako nimejua kua umenizidi baadhi ya vitu na kujua historia ya nchi yetu.

Na nikafikiri unatakiwa kunizidi busara pia.

Gari ni nini basi kama halifanyi kilicholengwa nacho ambacho ni usafiri?

Kisima kama hakitoi maji je?

Ikiwa hoja yako ni kulipia gari na si usafiri.
Gari lako likiharibika ukalipaki kwa miaka miwili utalilipia road license na tozo zingine?

Ikiwa hoja yako ni tunalipia kisima na siyo maji.
Kama nilichimba kisima ila kimekauka miaka miwili nyuma nitatakiwa kukilipia?

Badala yake umeamua kumuita kila mtu hana akili.


Kisima Cha chini ya Mita 15 Na kisichotumia Miundombinu Kama Pump hakitozwi kodi japo kinatoa maji Kama kile ambacho kina Miundombinu n.k, hapo ndio ujifunze Kuwa msingi wa kutozwa kodi sio kutoa maji ndio sababu japo vyote vinatoa Maji lakin vipo vinavyotozwa kodi Na visivyotozwa kodi

Baiskeli Na gari vyote vinatoa huduma ya usafiri lakin Baiskeli haitozwi kodi Kama gari , Kama hoja ingekuwa Ni usafiri ndio unatozwa kodi Basi vyote gari Na Baiskeli vingetozwa kodi

Najua Bado hujanielewa Kwa Kuwa inahitaji kulipa ada , kukaa darasani kufundishwa Na kufanya Mtihani Na kupata majibu ili kuelewa Masuala ya Taxation
 
Kiukweli sijakuelewa tangu ulipoamua kusema akili sina.

Kwa kusoma posts zako nimejua kua umenizidi baadhi ya vitu na kujua historia ya nchi yetu.

Na nikafikiri unatakiwa kunizidi busara pia.

Gari ni nini basi kama halifanyi kilicholengwa nacho ambacho ni usafiri?

Kisima kama hakitoi maji je?

Ikiwa hoja yako ni kulipia gari na si usafiri.
Gari lako likiharibika ukalipaki kwa miaka miwili utalilipia road license na tozo zingine?

Ikiwa hoja yako ni tunalipia kisima na siyo maji.
Kama nilichimba kisima ila kimekauka miaka miwili nyuma nitatakiwa kukilipia?

Badala yake umeamua kumuita kila mtu hana akili.
vijana wa lumumba akili zao wote sawa...huoni hata kule bungeni kila kitu wao hupayuka NDIOOOO.
 
Back
Top Bottom