Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Mkurugenzi akanusha vigogo kupewa viwanja Arusha
Imeandikwa na John Mhala, Arusha;
Tarehe: 3rd December 2010
MKURUGENZI wa Halmashauri ya Arusha, Wilayani Arumeru, Halifa Hida, ametoa ufafanuzi juu ya malalamiko ya ugawaji wa viwanja vilivyoko eneo la Burk, na kusema kuwa hakuna kigogo yeyote aliyepata kiwanja zaidi ya kimoja kama uvumi ulivyozagaa nje na ndani ya halimashauri hiyo.
Hida aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake, kuhusiana na malalamiko hayo yanayoendelea kutolewa juu ya ugawaji wa viwanja hivyo unaodaiwa kuuziwa vigogo wa serikali huku majina ya wakazi wa wilaya hiyo yakikatwa.
Alisema viwanja hivyo vimetolewa kwa mujibu wa sheria na kila aliyepatiwa fomu ya maombi alifuata sheria kama walivyotangaza katika vyombo mbalimbali vya habari.
Aidha aliongeza kuwa malalamiko mengi yanayotolewa na baadhi ya wananchi yamekuwa hayana tija, kwani majina ya watu wanaodaiwa ni vigogo waliomba viwanja hivyo kwa kufuata taratibu zote zinazohitajika.
Aliongeza kuwa uuzwaji wa viwanja hivyo haukuwa na siri ama masharti yoyote
yaliyoonesha kuzuia mtu yoyote asiye mkazi wa eneo hilo kutouziwa kiwanja.
Alisema, katika ugawaji huo hakuna ufisadi uliotumika wala kashfa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kuwa ugawaji wa viwanja hivyo umetawaliwa na ufisadi na kwamba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) inachunguza suala hilo.
Akijibu hoja kwa nini tangazo la viwanja hilo lilitolewa kwa wiki mbili na
lisikatizwe kwa wiki moja mara baada ya kutimia idadi ya watu walioomba kulingana
na idadi ya viwanja hivyo 700, alisema kuwa, sheria hairuhusu.
"Kama umetangaza siku 14 lazima upokee maombi siku 14 hata kama yatakuwa yamevuka malengo, kama jinsi ilivyotokea kwa kupokea maombi ya watu zaidi ya 20,000. "
Alisema hata hivyo watu waliokosa wasikate tamaa, kwani wote watapatiwa viwanja kwa mujibu wa taratibu zitakapokamilikaa za upimaji wa maeneo ya wazi ya Lakilaki na Gomba Estate wilayani humo.
Hida alisema lengo kubwa linalofanya na halmashauri hiyo ni kuhakikisha wanapunguza ujenzi holela kwa kuzungumza na wenye mashamba makubwa ili kuyanunua na kuyagawa kwa wananchi wenye shida ya ardhi.
Malalamiko hayo yamekuja kufuatia wananchi wengi waliomba viwanja hivyo kwa kulipia Sh. 10,000 kwa fomu ya maombi, kukatwa majina yao na majina yaliyorudi kuwa ni ya vigogo wa serikali na wafanyabiashara kutoka mikoa mbalimbali nchini.
Imeandikwa na John Mhala, Arusha;
Tarehe: 3rd December 2010
MKURUGENZI wa Halmashauri ya Arusha, Wilayani Arumeru, Halifa Hida, ametoa ufafanuzi juu ya malalamiko ya ugawaji wa viwanja vilivyoko eneo la Burk, na kusema kuwa hakuna kigogo yeyote aliyepata kiwanja zaidi ya kimoja kama uvumi ulivyozagaa nje na ndani ya halimashauri hiyo.
Hida aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake, kuhusiana na malalamiko hayo yanayoendelea kutolewa juu ya ugawaji wa viwanja hivyo unaodaiwa kuuziwa vigogo wa serikali huku majina ya wakazi wa wilaya hiyo yakikatwa.
Alisema viwanja hivyo vimetolewa kwa mujibu wa sheria na kila aliyepatiwa fomu ya maombi alifuata sheria kama walivyotangaza katika vyombo mbalimbali vya habari.
Aidha aliongeza kuwa malalamiko mengi yanayotolewa na baadhi ya wananchi yamekuwa hayana tija, kwani majina ya watu wanaodaiwa ni vigogo waliomba viwanja hivyo kwa kufuata taratibu zote zinazohitajika.
Aliongeza kuwa uuzwaji wa viwanja hivyo haukuwa na siri ama masharti yoyote
yaliyoonesha kuzuia mtu yoyote asiye mkazi wa eneo hilo kutouziwa kiwanja.
Alisema, katika ugawaji huo hakuna ufisadi uliotumika wala kashfa kama inavyodaiwa na baadhi ya watu kuwa ugawaji wa viwanja hivyo umetawaliwa na ufisadi na kwamba Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) inachunguza suala hilo.
Akijibu hoja kwa nini tangazo la viwanja hilo lilitolewa kwa wiki mbili na
lisikatizwe kwa wiki moja mara baada ya kutimia idadi ya watu walioomba kulingana
na idadi ya viwanja hivyo 700, alisema kuwa, sheria hairuhusu.
"Kama umetangaza siku 14 lazima upokee maombi siku 14 hata kama yatakuwa yamevuka malengo, kama jinsi ilivyotokea kwa kupokea maombi ya watu zaidi ya 20,000. "
Alisema hata hivyo watu waliokosa wasikate tamaa, kwani wote watapatiwa viwanja kwa mujibu wa taratibu zitakapokamilikaa za upimaji wa maeneo ya wazi ya Lakilaki na Gomba Estate wilayani humo.
Hida alisema lengo kubwa linalofanya na halmashauri hiyo ni kuhakikisha wanapunguza ujenzi holela kwa kuzungumza na wenye mashamba makubwa ili kuyanunua na kuyagawa kwa wananchi wenye shida ya ardhi.
Malalamiko hayo yamekuja kufuatia wananchi wengi waliomba viwanja hivyo kwa kulipia Sh. 10,000 kwa fomu ya maombi, kukatwa majina yao na majina yaliyorudi kuwa ni ya vigogo wa serikali na wafanyabiashara kutoka mikoa mbalimbali nchini.