Sakata la Umeme: Gharama za IPTL juu Zaidi ya Mara 6 Kulingana na Dowans

Si mmekwisha ambiwa kuwa mitambo mipya imekwisha agizwa lakini itachukua miezi 12?

Naona hiyo mitambo mipya inaanza kusukwa toka A ndiyo maana inachukua miezi 12
 
Mkuu wangu wewe ni msomi mzuri sana na bila shaka unaelewa vizuri maana haswa ya msemo Usipoziba Ufa utajenga ukuta...
Kwa maana kwamba muda na gharama za kuziba ufa ni ndogo sana ukilinganisha na ujenzi wa Ukuta mzima.. Lakini inapotokea kwamba gharama kuziba huo Ufa zinazidi zile za ujenzi wa Ukuta kwa nini wananchi wasithubutu kuuliza?..
Nitarudia kusema kuwepo kwa IPTL na Dowans ni ktk kuziba ufa ulotokea katika mahitaji ya Umeme wetu, wala sii moja ya mikakati ya kuendeleza Umeme nchini, tunaziba pale palipobomoka..

Mkandara:

Suala la umeme ni la matumizi ya technologia. Mwaka huu kwa wanaofatilia masuala ya technologia wanaelewa kuwa India imeweza kupeleka chombo cha anga kuzunguka mwezi na kutuma picha nzuri ambazo zinatumiwa na taasisi nyingi tu hata katika nchi zilizoendelea.

Program ya Aerospace ilianza India mwaka 1963, nchi hiyo ikiwa changa. Lakini leo tunaona matunda yake.

Kwa kutumia mfano wa India, lazima Tanzania ijifunze kuwa sustainable programs ndizo zitakazoinua nchi.

Kwa kutumia mtaji wa niliyosema hapo juu na mfano wa India, watanzania watakiwa kuelewa kuwa suala la nishati ni la matumizi ya technologia, linahitaji sera za uhakika ambazo mpaka sasa hivi tumeshindwa kuzipanga. Kilichobakia ni wananchi kulalamikia au kushabikia serikali kwa ufumbuzi wa matatizo kwa kutumia adhoc solutions.
 
Zakumi,

Bila shaka matumizi ya Umeme ni matumizi ya technologia, lakini ni muhimu kufahamu kwamba asili yake ilitokana na mahitaji ya nguvu hizo ktk uzalishaji..Kwa hiyo unapotaka nguvu hizo kuimarisha ama kuboreshwa kwake ndiko kunasukuma ubunifu kwa sababu hakuna kitu kinachoweza buniwa na kutengenezwa pasipo kuwepo mahitaji yake.

Mkuu wangu maendeleo ni hatua, hatuwezi kufanana na India wala kujifananisha nao kwani wao wapo mbali na tofauti kimaendeleo, na mazingira yetu ni tofauti kabisa kupima mahitaji baina yetu..Maendeleo sii mbio za marathon, hatushindani isipokuwa kila mmoja wetu anajaribu kuboresha maisha yake kwa kuweka vitendea kazi kwa kila hatua ambazo zinalingana na mahitaji.

Sisi sote tunahitaji Umeme iwe Marekani, India au Tanzania, lakini tofauti kubwa inakuja kutokana na hatua tulizofikia sote ktk mahitaji ya Umeme huo..We are not travelling on the same route kila mmoja wetu anatakiwa kutengeneza barabara yake ya maendeleo kulingana na mazingira yake..hivyo pamoja nakwamba malengo yetu ni sawa kufika huko kwenye maendeleo, sisi sote hatuendi ktk chombo kimoja wala route moja, maderava pia ni tofauti..Na kwa kuongezea tu hata mazingira yaliyotuzunguka ni tofauti.

Wakati Marekani wanajikita ktk kubadilisha kabisa matumizi ya nguvu hizo kutoka mafuta lakini hawana shida ya umeme kwani tayari wamekwisha fikia kima sawa na mahitaji yao, sisi ndio kwanza tumegeuza shingo zetu kwa matatizo kukana mahitaji hayo na hao India wao hawana kiza kama chetu, wamejikita zaidi ktk kuboresha nguvu hizo zipate kukidhi mahitaji yao..

Hivyo mikakati baina yetu haiwezi kuwa sawa hata kidogo na priority pia haziwezi kuwa sawa. waache India wapeleke mtu mwezini na wazunguke sana tu lakini sisi hatuwezi kuiga India wakati mahitaji yao yamefika hatua nyingine kabisa. Ndio maana muda mwingi nimeutumia hapa kujaribu kufafanua nafasi ya IPTL na Dowans kuwa hivi ni vibatari.. ni vibatari vilivyoletwa baada ya umeme kukatika kwa lugha yenu wanasema A solution on Emergency situation..

Tanzania inahitaji umeme usiopungua Mw 2000 ambao nchi kama Marekani au India ni sehemu ndogo sana ya mahitaji yao ukitaka kulinganisha, na takwimu zinaonyesha wazi kwamba umeme wetu unawahudumia asilimia chini ya 10 kama sii 12 tu ya wananchi wote meaning tulichoanacho kinatakiwa kuongezeka kwa asilimia 90 kama sio 100..Kifupi ni aibu tupu. sasa leo hii hata hizo asilimia 10 hawapati umeme tumefikia kuwasha vibatari hivi ili turudi ktk asilimia 10 hadi 12 wenye umeme (on emergency situation) which is acceptable, lakini ajabu ni kwamba inaonyesha wazi kabisa kwamba hivi vibatari are there to stay kutokana na contracts zilizosainiwa. Na kibaya zaidi kisiasa inatumiwa kama ndio malengo ya mahitaji yetu ya umeme nchini..

Kwa jinsi navyoijua nchi yangu, viongozi wake nafahamu fika kwamba hapa ndio tumefika.. Nchi itaendelea kutumia vibatari, wakati India wanafikiria kwenda mwezini, meaning wao wanapiga hatua kwenda mbele sisi ndio kwanza gari letu limekatika central bolts tunataka kufunga na kamba..

Na hapa ndipo ubishi wote ulipo sasa hivi, kama kawaida ya wadanganyika tunapoteza muda mwingi kujadiliana jinsi ya kuondoka tunaelewa fika kwamba wakifunga kamba hizo joint, gari litaondoka tulipokwama lakini hakuna uhakika wa kufika tunakotaka kwenda. Na kama niliyosema toka mwanzo Hiyo ndio imetoka! gari letu la maendeleo litaendeshwa hivyo hivyo kwa kuunganisha unganisha hadi tufike huko tunakokwenda kwa baraka zake Mungu.

Mkuu hakuna kitu kama kukubali makosa, kisha unaweza jifunza kutokana na makosa hayo ndio faida ya makosa ya awali, kisha tuwe wepesi kujirekebisha. Tatizo la Wadanganyika hata kukubali makosa ni haramu...Tazama ya Lowassa na viongozi wote tunaowafahamu hakuna hata mmoja alokubali makosa. Kila siku wana sababu ya njye ya makosa, sana husingizia Amri ya Mungu kitu ambacho kina kufuru ndani yake..Yawezekana kabisa kuwa hizi adha zote zinatokana na adhabu za kufuru zetu tunazozifanya kwani hakuna kufuru mbaya kama Muumini akimshirikisha Mungu kuliko yule asiyeamini kabisa kutomshirikisha Mungu (somo jingine).

Mkuu binafsi nimechoka na nchi yangu, naipenda sana lakini hizi habari za nchi kutokuwa na Umeme ktk karne hii ni kama viwe niko ndotoni.
 
Umeme kupata sawa, lakini naona swala zima linachukuliwa kisiasa zaidi kuliko kisayansi na mantiki. Sawa na kutaka kuonekana mshindi mahakamani kwa gharama ya kukufilisi ili umshinde mwizi wa kuku wako.

Hivi bado tuko kwenye enzi za kuamini kwamba mawazo mazuri lazima yatoke kwa wanaCCM? Kabwe na wanasheria wanasema taifisha dowans na hakuna kitu cha kudaiwa, lakini serikali inashupaza shingo ati hilo halitakuwa. Kumbe serikali ina pesa nyingi namna hiyo, ilingojea nini kuweka mambo sawa kwa mapema zaidi?

Leka
 
Watanzania mna-bore na mko negative sana na ndio maana hamuendelei. JK alipoamuru kuwashwa kwa mitambo, mnalalamika kuwa mawazo yalikuwa ya Zitto Kabwe.

Gharama za IPTL zinaanza kuonekana, mnalalamika kuwa gharama ni kubwa sana.

Hakuna modernity inayoshuka kutoka mbinguni kama chakula cha wana w Israel. Acheni kulalamalalama.

The presenter of this thread (TK) made a min Cost - Benefit analysis which is really sensible and gives a guidance for any decision maker. Tanzania needs power, and during this period emergence power is crucial but not at unjustifiable costs.
 
sawa wana solve problem, lakini najiuliza hivi ni kwa nini wale ambao wamesabisha tufike hapa hawajatiwa mbaroni tuu? wale wenye mamlaka ya kufanya maamuzi ambao walijua kwamba mitambo ya Dowans sio suluhu kwa sababu ni ya kitapeli na iko kwenye kesi lakini wakaendelea kutetea kwamba inunuliwe badala ya kununua mitambo mipya mara moja.

Walijua kwamba kiangazi huwa kinakuja kila mwaka katika miezi hii lakini hawakufanya juhudi yoyote ya kununua mitambo mipya kana kwamba mitambo pekee hapa duniani iendeshwayo kwa gesi ni ya Dowans tu.

Kama JK ameweza kuamuru mitambo ya IPTL iwashwe mara moja anashindwa nini kuamuru watu wanaosabisha hasara yote hii na usumbufu wote huu wasikamatwe mara moja na kufunguliwa mashtaka?


TELL HIM AND ASK HIM NOT TO COME WITH CHEAP QUESTIONS LIKE THE ONE SHE HAS ASKED. wE ALWAYS HAVE TO BE SERIOUS ON MATTERS OF NATION'S INTEREST. WE ARE NOT READY TO SEE THE GOVNT ACQUIRING DOWANS. tHRE HAVE BEEN KIND OF BEING IRRESPONSIBLE FOIR SOME TANESCO AND GOVT EPLOYEES CHARGED WITH THE TASK OF ENSURING THAT THE COUNTRY HAS EMOUGH POWER.

DOWANS NO! DOWANS NO!
 
Hii Tanesco ipo kibiashara au inatoa huduma? Kama kweli wanafanya biashara tangia kuanzishwa kwake hivi sasa tungetegemea wanamiliki mitambo ya gas ya kuzalisha MW 500 ambazo zingekidhi mahitaji. Na hayo makampuni ya kijanja yasingekuwepo na wanasiasa wasingesogeza pua zao Tanesco na umeme ungekuwa bei poa.
 
The presenter of this thread (TK) made a min Cost - Benefit analysis which is really sensible and gives a guidance for any decision maker. Tanzania needs power, and during this period emergence power is crucial but not at unjustifiable costs.

Mna-bore tu hakuna cha kujitetea. Kama unaona cost ni unjustifiable, basi acheni kutumia umeme na uone matokeo yake katika sekta zote.
 
Hii Tanesco ipo kibiashara au inatoa huduma? Kama kweli wanafanya biashara tangia kuanzishwa kwake hivi sasa tungetegemea wanamiliki mitambo ya gas ya kuzalisha MW 500 ambazo zingekidhi mahitaji. Na hayo makampuni ya kijanja yasingekuwepo na wanasiasa wasingesogeza pua zao Tanesco na umeme ungekuwa bei poa.

Gimme a Break!!!!!!!!!! Ni kampuni gani la kiserikali au taasisi nililowahi kufanya kazi kwa ufanisi? Kama hakuna kwanini unataka Tanesco iwe Exceptional.
 
Back
Top Bottom