Sakata la UDA: Dodoso katika mtazamo wa kisheria

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,196
25,516
Naanzia pale panapoelezwa kuwa aliyekuwa Meya wa Jiji, Dr. Didas Masaburi aliuza kihalali hisa za UDA,asilimia 51,kwa kampuni ya Simon Group. Imesemwa kuwa Meya alikuwa na mamlaka yote ya kuuza hisa husika.

Kwanza,hisa za UDA ni moja ya mali za Halmashauri ya jiji. Mali yoyote ya jiji hupatikana au kuondolewa kwa ridhaa ya vikao halali vya Baraza la Madiwani la Jiji. Kununuliwa au kuuzwa kunapaswa kuwa na baraka za Madiwani kutokana na kikao.

Pili,Meya au Naibu Meya anatenda kadiri ya maamuzi ya kikao cha Madiwani. Kinyume chake,halifanywi jambo halali. Kuhusu la hisa za UDA,ushahidi pekee unaotakiwa ni azimio la Baraza la Madiwani wa jiji kuuza hisa zao za UDA. Kama hakuna,Meya hawezi kuwa ameuza kihalali.

Kuondoa mjadala,maazimio yaanikwe.
 
Naanzia pale panapoelezwa kuwa aliyekuwa Meya wa Jiji, Dr. Didas Masaburi aliuza kihalali hisa za UDA,asilimia 51,kwa kampuni ya Simon Group. Imesemwa kuwa Meya alikuwa na mamlaka yote ya kuuza hisa husika.

Kwanza,hisa za UDA ni moja ya mali za Halmashauri ya jiji. Mali yoyote ya jiji hupatikana au kuondolewa kwa ridhaa ya vikao halali vya Baraza la Madiwani la Jiji. Kununuliwa au kuuzwa kunapaswa kuwa na baraka za Madiwani kutokana na kikao.

Pili,Meya au Naibu Meya anatenda kadiri ya maamuzi ya kikao cha Madiwani. Kinyume chake,halifanywi jambo halali. Kuhusu la hisa za UDA,ushahidi pekee unaotakiwa ni azimio la Baraza la Madiwani wa jiji kuuza hisa zao za UDA. Kama hakuna,Meya hawezi kuwa ameuza kihalali.

Kuondoa mjadala,maazimio yaanikwe.

Point za Msingi sana.Sasa Jiji chini ya UKAWA wanapaswa kwenda Mahakamani kupinga dhuluma hii na sio kuliongelea kisiasa
 
Pili,Meya au Naibu Meya anatenda kadiri ya maamuzi ya kikao cha Madiwani. Kinyume chake,halifanywi jambo halali. Kuhusu la hisa za UDA,ushahidi pekee unaotakiwa ni azimio la Baraza la Madiwani wa jiji kuuza hisa zao za UDA. Kama hakuna,Meya hawezi kuwa ameuza kihalali.

Ninakubaliana na wewe mia kwa mia.

Ila majitu ya CCM, kwani ilikuwa inaelewa wala kujali utawala wa sheria nini? Ndio maana bila ya Udikteta rafiki kama wa JPM hawawezi kunyooshwa, na nchi ikawa safi.

Yule Jecha kule Zanzibar si alifanya maamuzi kama haya haya tu?
 
Msajili wa Hazina katika hili ameonekana wazi kuwa sio mlinzi tena wa mali za umma ambazo zimewekwa chini yake Bali ni mwizi au anayeshirikiana na wezi.
Magufuli ajue wazi kaachiwa mchwa eti utunze ghala la nafaka, na asipomshughulikia asije kuta anaambiwa serikali yake inalipia kodi majengo ya Ikulu kwani yalishauzwa kisheria siku nyingi
 
Msajili wa Hazina katika hili ameonekana wazi kuwa sio mlinzi tena wa mali za umma ambazo zimewekwa chini yake Bali ni mwizi au anayeshirikiana na wezi.
Magufuli ajue wazi kaachiwa mchwa eti utunze ghala la nafaka, na asipomshughulikia asije kuta anaambiwa serikali yake inalipia kodi majengo ya Ikulu kwani yalishauzwa kisheria siku nyingi
Ameteuliwa ili kuwalinda wakwapuaji
 
[QUOTE="Utatu, post:

Yule Jecha kule Zanzibar si alifanya maamuzi kama haya haya tu?
[/QUOTE]

Umenikuna na.hiyo quote yako. Ya Jecha kule Zanzibar wanayakubali.

Ya Didas Masaburi huku bara hawayakubali. Bila kufuata principal na sheria tena tulizojiwekea wenyewe tutayumba sana.
 
Point za Msingi sana.Sasa Jiji chini ya UKAWA wanapaswa kwenda Mahakamani kupinga dhuluma hii na sio kuliongelea kisiasa
Usiwe unakua mwili na kuacha kukua kiakili, hisa za uda unajua zimeuzwa mwaka gani? Jaribu kuficha upuuzi mbele za jamii wewe.
 
Wanajitahidi sana kuficha wizi wa mali ya uma uliofanywa na familia ya mfalme, huyu anae tetea wezi Maggufuli asipo mtumbua nitaunga mkono hoja ya mama Tibaijuka kuwa MAFISADI HASWA HAWAGUSWI,.
 
Mafuru ni jasiri mali inaonekana ya wizi kabisa kabisa anaitetea kuwa si ya wizi..
Hapa kuna walakini. Walioshika nafasi hiyo kabla yake walikuwa wakina nani? Bila shaka yeye anaripoti alichokikuta kwenye documents. Hiyo ndiyo loop hole yake.
 
Hivi mnajua serikali iliidhamini UDA kuchukua mkopo wa bilioni 108 kutoka benki ya NMB kwa ajili ya kuendesha mradi wa DART?

Swali:Kama una UDA ilikuwa imebinafsishwa,kwanini serikali tena idhamini kampuni binafsi kuchukua mkopo benki?
 
Mkuu Salary Slip kuna maswali mengi sana kuhusu hili sakata na cha mkushangaza huyu alijinadi kwamba atapambana na mafisadi na Waziri Mkuu wake wanalikwepa mchana kweupe na kujifanya kama hawajalisikia hili sakata na hii inasababishwa na wahusika wakuu wa hili sakata. CCM ni ile ile na ahadi za kupambana na ufisadi nchini ni usanii tu.

Hivi mnajua serikali iliidhamini UDA kuchukua mkopo wa bilioni 108 kutoka benki ya NMB kwa ajili ya kuendesha mradi wa DART?

Swali:Kama una UDA ilikuwa imebinafsishwa,kwanini serikali tena idhamini kampuni binafsi kuchukua mkopo benki?
 
Back
Top Bottom