Elections 2010 Sakata la mauaji ya Dereva wa CCM Maswa na hatima ya Shibuda

Baada ya matishio ya kumwagika kwa damu Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, hatimaye jana damu imemwagika kweli huko Maswa ambapo dereva wa gari la mgombea wa CCM jimboni humo, ameuwawaw na wananchi wenye hasira.

Nimezungumza na Mgombea wa Chadema, John Magalle Shibuda, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, japo hakuthibisha maafa, bali ametoa upande wake wa story kuwa yeye akiwa Jukwani kwenye kampeni zake, akatuma gari lake la matangazo kutangulia kijiji kinachofuata.

Gari hilo likiwa njiani, lilivamiwa na gari la mgombea wa CCM wakitaka kuligonga ndipo likalikwepa na ikawa ndio salama yao, gari lile la mgombea wa CCM nalo likasisima, watu wakashuka na kuanza kuwashabulia hao kwenye gari la Chadema.

Kwa mujibu wa Shibuda, vijana wake wakapiga mayowe ya kuvamiwa, wanakijiji wakajitiokeza kuwasaidia ndipo waliotembeza hicho kichapo kwa dereva huyo.

Kwa vile Shibuda ni interested party, upande wake wa story lazima upatiwe balance ya upande wa pili wa CCM na hatimaye kuthibitishwa na authorities za Jeshi la polisi.

Naendelea kufuatilia upande wa pili na uthibitisho wa polisi, pia nafanya juhudi za kumtafuta mpiganaji Fredirick Katulanda ambaye siku zote husimama wima bila kuegemea upande wowote.

Update 1.

Nimefanikiwa kumpata mpiganaji Fredirick Katulanda, kwanza amenithibitishia ni kweli damu imemwagika kwa kifo kimetokea kweli.
Pia ni kweli John Shibuda, jana amelala mahabusu, leo ameachiliwa kwa dhamana ndogo na kurejea mikonani mwa polisi mpaka sasa.
Amenithibitishia kuwa polisi wamethibitisha tukio hilo.

Vesion ya CCM kwa mujibu wa Katulanda, gari la mgombea wa CCM na la Mgombea wa Chadema yalipishana, Gari Chadema wameshuka 'kuchimba dawa' gari la CCM wakajipitia zao (naasume walizomeana), baada ya kupita mtu mmoja kwenye gari ya CCM akadondosha kofia, hivyo gari la CCM likasimama mbele, aliyedondosha kofia akarudi nyuma kuifuata, ndipo wafuasi wa Chadema wakamdaka na kumtembezea kichapo, wenzao kuona hivyo wakarudi kumsaidia ndipo wakavamiwa na wafuasi wa Chadema na ndipo ikafuatiav piga nikupige iliyosababisho kifo cha dereva.

Katika hatua nyingine, Katulanda ameendelea kupasha kuwa Mgombea wa CCM kwa jimbo hilo, anatafutwa na polisi kwa kosa la kumshambulia OCD wa Maswa. RPC amesema tukio la kifo ni tukio jingine, na hilo la shumbulio kwa OCD ni tukio jingine na hayana uhusiano.

Bado nafuatilia taarifa rasmi toka kwa RPC Mwanza.

Tunaendelea.


Kuna dhana ya kisheria unaoitwa VICARIOUS LIABILITY.
Dhana hii inasema kwamba, mtu aliye chini ya ajira yako, au ajira ya kampuni yako, anaweza kusababisha ukashtakiwa iwapo katika utendaji wake wa kazi atasababisha madhara ya aina yoyote kwa mtu/watu wengine.

Lakini kwenye vyama vya siasa, dhana hii haipo, kwani masuala ya siasa ni ya kiimani zaidi, yaani, imani ya mtu mwenyewe, anavyotaka. Ni vigumu kujenga hoja kwamba, iwapo mwanachama wa chama cha siasa atafanya fujo, basi, kiongozi wa chama chake ataweza kukamatwa na kutiwa hatiani (kwa kosa la kusababisha vurugu, watu kuumizwa, mauaji, n.k.)

Hili la Shibuda, tujiulize: Kwani yeye ndiye aliyewatuma mashabiki na wanachama wa - nachelea kusema wafuasi - wa CHADEMA kufanya hizo fujo?
 
Maelezo yanayotolewa na ccm na mamluki zake(polisi) yanatoa picha kwamba ccm wamebuni mbinu ya kuwaingilia washindani wao katika mikutano yao ili wapate sababu ya kuanzisha fujo. Yametokea hivyo huko hai, moshi mjini, Arusha, mwanza na sasa huko shinyanga ambapo mzaha wao umetumbua usaha. Ukichunguza majimbo yote ambayo ccm wameshajikatia tamaa ya kushinda ndiko wanakopandikiza huu upuuzi wao. Tunaomba watu wote wenye kupewa heshima na umma wa watanzania waikemee ccm kwa huu uchokozi wanaoupanga dhidi ya washindani wao. Mara zote ndio wao wanaingilia mikutano ya wengine. Huko mwanza jana gari ya ccm imevamia msafara wa mgombea wa chadema na polisi katika kujaribu kuwatetea katika upuuzi wao, wanasema eti yule dereva alikuwa anakimbia ajali aliyoifanya kugonga pikipiki ndio akajikuta ameuvamia msafara wa chadema. Huu ni uongo mweusi kama weusi ulivyo unaotungwa na afisa wa polisi wa ngazi ya juu.
 
Update 2.
Hii ni input ya mpiganaji, Fredrick Katulanda kwa hisani ya kulekwa 'wanabidii'
Jeshi la Polisi limemkamata mgombea wa Chadema John Shibuda kutokana
na afuasi wake kudaiwa kumpiga mpaka kufa dreva wa gari la mgombea wa
CCM Robert Simon Kisena wote wa jimbo la Maswa Magharibi.

Tunafualia zaidi kwani habari zineeleza kuwa mbali na shibuda watu
wengine 10 wanashikiliwa na polisi huku ikielezwa kuwa mgombea wa CCM
naye anasakwa na polisi kwa kumpiga OCD wa kituo cha Maswa akimtuhumu
kuwapendelea wapinzani ambao anadai kuwa wamemuua dreva wake.
 
Hii nchi hii.. kweli kuna watu wanaamini kabisa kuwa kila mmoja wa hivi vyama wangeweza kusema ndio wenye makosa? Really? Lakini kilichonichekesha ni hiyo stori ya kofia! Hii kofia iliyoanguka mbele ya wana Chadema wakiwa wana"chimba" dawa.. kofia hii ina uchokozi! Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi. Amin.
 
Ndugu yangu we ni mgeni wa huyol jamaa? huwa aha appreciate mchango wa mtu yoyote, na ndo maana unaona hajampa hata mtu mmoja thanx, yeye akiona habari ni nzuri anaichukua na kuibadiilisha jina as if yeye ndio aliyeandika na kuiweka kwenye mitandano mingine

Kituko, looks like you really know the guy ' SHY' copy and paste ya kwenda mbele!!!
 
Update 2.
Hii ni input ya mpiganaji, Fredrick Katulanda kwa hisani ya kulekwa 'wanabidii'
Jeshi la Polisi limemkamata mgombea wa Chadema John Shibuda kutokana
na afuasi wake kudaiwa kumpiga mpaka kufa dreva wa gari la mgombea wa
CCM Robert Simon Kisena wote wa jimbo la Maswa Magharibi.



Tunafualia zaidi kwani habari zineeleza kuwa mbali na shibuda watu
wengine 10 wanashikiliwa na polisi huku ikielezwa kuwa mgombea wa CCM
naye anasakwa na polisi kwa kumpiga OCD wa kituo cha Maswa akimtuhumu
kuwapendelea wapinzani ambao anadai kuwa wamemuua dreva wake.

Hapo kwenye bold naomba kusaidiwa. Inakuwaje wafuasi wafanye mauaji, kukamatwa akamatwe mgombea? Hivi mtoto akifanya kosa mzazi anaadhibiwa badala yake? Me confused hapa asee.
 
Kuna dhana ya kisheria unaoitwa VICARIOUS LIABILITY.
Dhana hii inasema kwamba, mtu aliye chini ya ajira yako, au ajira ya kampuni yako, anaweza kusababisha ukashtakiwa iwapo katika utendaji wake wa kazi atasababisha madhara ya aina yoyote kwa mtu/watu wengine.

Lakini kwenye vyama vya siasa, dhana hii haipo, kwani masuala ya siasa ni ya kiimani zaidi, yaani, imani ya mtu mwenyewe, anavyotaka. Ni vigumu kujenga hoja kwamba, iwapo mwanachama wa chama cha siasa atafanya fujo, basi, kiongozi wa chama chake ataweza kukamatwa na kutiwa hatiani (kwa kosa la kusababisha vurugu, watu kuumizwa, mauaji, n.k.)

Hili la Shibuda, tujiulize: Kwani yeye ndiye aliyewatuma mashabiki na wanachama wa - nachelea kusema wafuasi - wa CHADEMA kufanya hizo fujo?

Heshima kwako Mwanahaki,

Hii ndiyo faida ya JF lipo darasa la nguvu .nimekugongea thenkyu
 
Hapo kwenye bold naomba kusaidiwa. Inakuwaje wafuasi wafanye mauaji, kukamatwa akamatwe mgombea? Hivi mtoto akifanya kosa mzazi anaadhibiwa badala yake? Me confused hapa asee.

Heshima Kwako Asprin.

Mkuu ebu pitia bandiko la Mwanahaki.
 
Inna lillahi wa inna ilaihi raji'un

The bottom line is mwanachama wa CCM ameuliwa na wanachama wa Chadema.

Words matters. Mwambieni mgombea wenu kwamba he has to be responsible for inflammatory words he says kwenye majukwaa. Most of them are false, without being fact checked by our media. Mpaka NEC and others waje kukanusha, its too late!
 
Selous, yes Shibuda yuko chini ya ulinzi, ila pia anashikiliwa kiuheshimiwa heshimiwa, jana amelala selo, leo asubuhi akaruhusiwa kwenda home kupata breakfast ya nguvu na kujipiga soap soap na kurejea mikononi mwa polisi. Mpaka nilipoongea nae, alikuwa bado ameshikiliwa ila pia anaruhusiwa kupiga simu etc.

Usishangae hizi ndizo hizo doble standards kwenye mahabusu zetu. Wale mafisadi wa EPA kabla hawajakamatwa, mahabusu maalum zilikarabatiwa pale gereza la Ukonga, wakafunga viyoyozi na plasma TV kubwa ukutani, halafu wanaletewa misosi na cataring ya New Africa hoteli, mahabusu wale wanachagua wangependa kula nini. Wanaangaliwa afya zao Regency Hospital kwa kubebwa na yale magari ya Knikt Support, ndio hivyo hatulingani kama vidole. Bado nafuatilia taarifa ya RPC.

Ebwanaeee.. I wish ningeweza kuwa fisadi...
 
Pole kwa dereva aliyefariki!
CCm WAJUE KUWA mbinu wanazotumia kupaka matope watu zinaanza kudhihirika...Sasa makusudi wamemtoakafara huyo dereva ili kuiundia lawama chadema...wameumia!
 
Radhi siombi msimamo wangu ni huo aandike habari zake kwa umakini sio kwa ushabiki yeye ni mzoefu wa haswa televisheni anajua anachofanya

Kwani sisi wageni nawewe? Tunakujua sana akili zako ndivyo zinavyo kutuma
 
wANACHI NI WEREVU WAMEONA WATANZANIA WANAVYO PASULIWA MAFUVU YA VICHWA NA GREEN GUARD ,
 

heshima kwako pasco,

mkuu napenda kusoma mabandiko yako huko balanced sana.

Ukiona hivyo ujue ccm maji yako shingoni hawana ustaharabu hata chembe.inashangaza kidogo hapa arusha dr batilda anapewa upendeleo wa kijinga,akimaliza mkutano anasindikiwa na msafara wa magari mengi hakuna polisi wa kumzuia,lema akisindikizwa inakuwa nongwa.mji wa arusha hauna barabara za kuhimili misafara ya wagombea ubunge laiti polisi wangezuia misafara ya wagombea wote ningewaelewa.

ngongo umeshawahi kunywa biha mpaka ukaroha?
 
Afadhali hiyo kura moja ya ccm imepungua. Mungu hamtupi mja wake

baina
user-offline.png
Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join DateTue Oct 2010Posts5Thanks0Thanked 1 Time in 1 Post Rep Power0




Mkuu baina kwanza karibu sana jukwaani
Leo nilipo kuwa naipitia hii post nimekuta members wanajadiliana kwa hoja na kuweka mbele utu na tofauti zao mbele, pamoja na tofauti zao sijaona matusi wala kuvunjiana utu jambo ambalo hapa JF ndio mwongozo wetu
Lakini mkuu hii post yako inaondoa dhana nzima ya ugreat thinker hapa jf, nilipo isoma sikuamini ulicho andika ilibidi nirudie tena na tena.
nakushauri ifute haraka sana, najua hujavunja sheria za jf lakini umeonyesha jinsi upeo wako wa kufikiri ulivyo mdogo, lakini nisikulaumu pengine ulipitiwa
Mwisho isome tene kwa umakini post yako, kisha vaa viatu vya mke, watoto,ndugu na jamaa wa marehemu, kisha linganisha na kura moja waliopoteza CCM. kwako wewe hii ni Mungu haja mtupa mja wake
SHAME ON U
 
Jamani mbona hamjatupa updates za mpiganaji Shibuda? Bado yuko ndani? Kafunguliwa mashitaka gani? Atakuwepo Dodoma novemba kuapishwa?
 
Back
Top Bottom