MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Baada ya matishio ya kumwagika kwa damu Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, hatimaye jana damu imemwagika kweli huko Maswa ambapo dereva wa gari la mgombea wa CCM jimboni humo, ameuwawaw na wananchi wenye hasira.
Nimezungumza na Mgombea wa Chadema, John Magalle Shibuda, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, japo hakuthibisha maafa, bali ametoa upande wake wa story kuwa yeye akiwa Jukwani kwenye kampeni zake, akatuma gari lake la matangazo kutangulia kijiji kinachofuata.
Gari hilo likiwa njiani, lilivamiwa na gari la mgombea wa CCM wakitaka kuligonga ndipo likalikwepa na ikawa ndio salama yao, gari lile la mgombea wa CCM nalo likasisima, watu wakashuka na kuanza kuwashabulia hao kwenye gari la Chadema.
Kwa mujibu wa Shibuda, vijana wake wakapiga mayowe ya kuvamiwa, wanakijiji wakajitiokeza kuwasaidia ndipo waliotembeza hicho kichapo kwa dereva huyo.
Kwa vile Shibuda ni interested party, upande wake wa story lazima upatiwe balance ya upande wa pili wa CCM na hatimaye kuthibitishwa na authorities za Jeshi la polisi.
Naendelea kufuatilia upande wa pili na uthibitisho wa polisi, pia nafanya juhudi za kumtafuta mpiganaji Fredirick Katulanda ambaye siku zote husimama wima bila kuegemea upande wowote.
Update 1.
Nimefanikiwa kumpata mpiganaji Fredirick Katulanda, kwanza amenithibitishia ni kweli damu imemwagika kwa kifo kimetokea kweli.
Pia ni kweli John Shibuda, jana amelala mahabusu, leo ameachiliwa kwa dhamana ndogo na kurejea mikonani mwa polisi mpaka sasa.
Amenithibitishia kuwa polisi wamethibitisha tukio hilo.
Vesion ya CCM kwa mujibu wa Katulanda, gari la mgombea wa CCM na la Mgombea wa Chadema yalipishana, Gari Chadema wameshuka 'kuchimba dawa' gari la CCM wakajipitia zao (naasume walizomeana), baada ya kupita mtu mmoja kwenye gari ya CCM akadondosha kofia, hivyo gari la CCM likasimama mbele, aliyedondosha kofia akarudi nyuma kuifuata, ndipo wafuasi wa Chadema wakamdaka na kumtembezea kichapo, wenzao kuona hivyo wakarudi kumsaidia ndipo wakavamiwa na wafuasi wa Chadema na ndipo ikafuatiav piga nikupige iliyosababisho kifo cha dereva.
Katika hatua nyingine, Katulanda ameendelea kupasha kuwa Mgombea wa CCM kwa jimbo hilo, anatafutwa na polisi kwa kosa la kumshambulia OCD wa Maswa. RPC amesema tukio la kifo ni tukio jingine, na hilo la shumbulio kwa OCD ni tukio jingine na hayana uhusiano.
Bado nafuatilia taarifa rasmi toka kwa RPC Mwanza.
Tunaendelea.
Kuna dhana ya kisheria unaoitwa VICARIOUS LIABILITY.
Dhana hii inasema kwamba, mtu aliye chini ya ajira yako, au ajira ya kampuni yako, anaweza kusababisha ukashtakiwa iwapo katika utendaji wake wa kazi atasababisha madhara ya aina yoyote kwa mtu/watu wengine.
Lakini kwenye vyama vya siasa, dhana hii haipo, kwani masuala ya siasa ni ya kiimani zaidi, yaani, imani ya mtu mwenyewe, anavyotaka. Ni vigumu kujenga hoja kwamba, iwapo mwanachama wa chama cha siasa atafanya fujo, basi, kiongozi wa chama chake ataweza kukamatwa na kutiwa hatiani (kwa kosa la kusababisha vurugu, watu kuumizwa, mauaji, n.k.)
Hili la Shibuda, tujiulize: Kwani yeye ndiye aliyewatuma mashabiki na wanachama wa - nachelea kusema wafuasi - wa CHADEMA kufanya hizo fujo?