Sakata la Makinikia: Kuna aibu inatunyemelea

Kinachotafutwa hapa ni sifa za kisiasa na ndio maana wameanza kugeuza maneno kuwa wapinzani wanatetea wawekezaji.

Mbowe na Katibu Mkuu wa chama walipaswa walichukue hili jambo na chama kilitolee tamko kupitia mkutano wa waandishi wa habari na pia watoe press release kwenye vyombo vya habari kuelezea historia nzima ya wapinzani katika hii vita.
Ni kweli kuwa wananchi wengi wanapotoshwa kuhusu dhana nzima ya vyama vya upinzani. Wanalishwa imani potofu na chuki dhidi ya vyama vya upinzani. Ukweli no kuwa vyama vya upinzani vina majukumu ya kutoa mawazo mbadala kwenye masuala nyeti na upinzani wamekuwa wakifanya hayo kwa ueledi mkubwa. Kwa hiyo upinzani ujipange kuzima hizi propaganda chafu dhidi ya vyama vya upinzani.
 
Kuna wakati kontena la makinikia lilizama bandarini, hao jamaa walitumia zaidi ya dollar milioni kumi kuliopoa.
Swali langu, kulikua na zahabu kiwango gani humo?

Mkuu dollar milioni kumi unaijua lakini?, lina uzito gani kwamba vifaa vya nchi hii vimeshindwa ikabidi viagizwe vingine?
 
d5a21844fa333739ee5b761427b2cb05.jpg
Huyu babu ndiye akiyekuwa anasoma ripoti kwa speed ya kumpita Kitwanga?
 
Rais wenu anawaambia malori 304 yamejaa dhahabu, mbulula wa magazeti nao wakaingia mkumbo wa kuandika,hivi dhahabu yenye ukubwa wa tofali ni kg ngapi? Kujaza gari ya Tani 7 je ni dhahabu kg ngapi? Hivi hata washauri wake hamumstui jamaa kuwa analeta mahesabu ya kitoto?
 
Kuna wakati kontena la makinikia lilizama bandarini, hao jamaa walitumia zaidi ya dollar milioni kumi kuliopoa.
Swali langu, kulikua na zahabu kiwango gani humo?
Dollar za Zimbabwe au Marekani?

Dollar za Marekani milioni kumi kwa bei ya dhahabu ya leo ( about $40 per g) unanunua dhahabu kilo 250.

Pure gold. 25 tons.

That is $10, 000, 000 ÷ $40/g =250, 000 g. That is 250 kg

Hilo kontena lilikuwa na gold bars au nini?

Unafahamu density ya dhahabu?

Unafahamu ujazo wa container la futi 40?

Container la futi 40 lina 67.7 meter cube.

Gold ina density ya 19.32 g/ cm cube. Thats 19320 g / m cu.

That's 19.32 kg / m cube.

Thats about 1308 kg per 67.7 meter cube (19.32 x 67.7).

1308 kg at 40 US $ per gram, todays price = 1,308,000 × 40 = 52.32 million USD.

(10÷52.32) x 100 = 19.11

Sasa hilo container lilikuwa limejaa pure gold karibu 20% ya ujazo wake?
 
Kwani Chadema miaka ile wakati wanapiga kelele mchanga usisafirishwe walikua wanatakwimu kiasi gani cha madini kipo katika kontena..
 
Hawa jamaa kweli watakuwa wametuibia lakini findings za kamati hizi kuhusu viwango vya madini na hasara tuliyopata, mimi binafsi zinanipa mashaka sana na ninaona tunaweza kuja kuumbuka hapo baadae.

Ni hivi,kama mchanga tu unaweza kuwa na madini ya thamani ya trilioni mpaka 380.9 kwa kiwango cha juu kwa miaka hiyo 19,ni wazi nchi zenye rasilimali madini duniani na zenye mikataba mizuri zingekuwa ni nchi tajiri sana katika huu ulimwngu.

Cha kujiuliza, kama hiyo ni thamani ya makinikia tu,madini yenyewe(matofali ya dhahabu) yatakuwa na thamani kiasi gani kwa miaka yote hiyo?

Alafu kingine cha kujiuliza ni kwanini findings za kamati hizi mbili za sasa na ile ya Jaji Bomani zitofautiane katika data za viwango vya madini tu lakini zifanane katika matokeo mengine ikiwemo na mapendekezo?Tukumbuke hata hadidu za rejea zimeonekana kufanana kwa maelezo ya Lissu aliyoyatoa Bungeni jana huku akiwa na ripoti ya Jaji Bomani mkononi.

Kubiwa ni kweli tumeibiwa lakini hivyo viwango vya madini vilivyotajwa katika hizo ripoti inabidi tujiulize mara mbili mbili kama kweli vina uhalisia na hali ya nchi zingine zenye migodi tena kutuzidi.

Hizi ripoti hawa mabwana wanaweza kuzitafsiri kama ni defamatory kwao na hivyo tunaweza kuwa sued for defamation japo wametubia unless tuthibitishe usahihi wa hivyo viwango vya madini.
THIS IS A REASONED ARGUMENT! BRAVO SLIP! NADHANI HAUKO HAPA NCHINI, MAANA UKIWA HAPA AKILI INAKUFA WANABAKI WACHACHE KAMA AKINA LISU!
 
Rais wenu anawaambia malori 304 yamejaa dhahabu, mbulula wa magazeti nao wakaingia mkumbo wa kuandika,hivi dhahabu yenye ukubwa wa tofali ni kg ngapi? Kujaza gari ya Tani 7 je ni dhahabu kg ngapi? Hivi hata washauri wake hamumstui jamaa kuwa analeta mahesabu ya kitoto?
Rais wenu anawaambia malori 304 yamejaa dhahabu, mbulula wa magazeti nao wakaingia mkumbo wa kuandika,hivi dhahabu yenye ukubwa wa tofali ni kg ngapi? Kujaza gari ya Tani 7 je ni dhahabu kg ngapi? Hivi hata washauri wake hamumstui jamaa kuwa analeta mahesabu ya kitoto?
Hii ya Malori bila shaka itakuwa imeshangaza dunia.
 
Mkuu katika hali ya kutafuta majibu na kujiuliza kama ulivyofanya
wewe,nilifanikiwa kumpata mtu ambaye amewahi kuwa mfanyakazi
wa kiwanda kimojawapo cha madini miongoni mwa makampuni haya.

Niweke baadhi ya mambo aliyonieleza na kunifumbua macho.
Alisema kiwanda alichokuwa anafanyia kazi kilikuwa
kinalishwa tani 800 za udongo kwa saa moja,na kumbuka
kama hakuna itilafu kiwanda kinatembea masaa 24.

Swali langu la kwanza: Je kama ni hivyo ni kwa nini
makontena ya mchanga kama yanavyotajwa kusafirishwa
ni kidogo ukilinganisha na kiasi cha mchanga unaoingizwa kwenye mashine?
JIBU: Si mchanga wote unachukuliwa kama makinikia,
kuna udongo unaochambuliwa na kutupwa kama makapi.
Dhahabu inatolewa na mchanga wenye thamani(wenye mabaki ya madini)
ndio hukusanywa kama makinikia.

Swali la pili:Je ni kiasi gani cha dhahabu mlikuwa
mnazalisha kwenye hatua ya mwisho?
Mara nyingi ni mche mmoja kwa siku wenye 25kgs.
japo kiwango hiki kimetofautiana na mwingine
niliyemhoji akasema kwa wiki ilikuwa inasafirishwa/siyo inazalishwa bali inasafirishwa
miche kati ya 4-7(yenye 25kgs kila mmoja) yenye 93% pure gold.

Kutokana na maelezo hayo,binafsi nikaona
kuwa makinikia siyo mchanga kama wengi tulivyodhani/aminishwa.
Bali ni mabaki ya madini ambayo kiwanda hakikuweza
kuya-extract.Udongo/makapi kwa kiwango kikubwa yanatupwa
hapa nchini.
Kwa mantiki hiyo,hayo makontena yenye huo so called mchanga ni
malighafi kama mali nyingine na siyo makapi.

Hivyo kiuzalendo,tujadiliane kwa moyo mweupe
na asiwepo wa kubezwa.Rais amefanya jambo jema kuchukua
hatua,Wapinzani nao ikiwezekana waombwe msamaha kwa
kile walichokiibua bungeni kuhusu jambo hili wakabezwa
na leo tunaamka baada ya kuibiwa sana.
Hili likifanyika wote tushikamane kumuunga mkono Rais
katika vita hii ya kiuchumi.
Kwa imani yangu hakuna anayempinga rais katika hili,
ila wengi wanasikitika,kuona jambo walilosema kama onyo
miaka mingi leo ndo linaonekana baada ya taifa kupata hasara kubwa.

Ushauri wangu:Ni kweli tumeishapata hasara itoshe,
kwa sasa tushikamane,ili kizazi kijacho kisiendelee
kupata hasara,na ili tufanikiwe,kubeza wapinzani kusiendelee
maana kunaamsha hasira.Na kumbeza rais kusiwepo
maana ameanzisha jambo ambalo awamu zote zilizopita
hakuna aliyewahi kulianzisha.
Asanteni
TUPE WASIFU WA HUYO MTU ULIMUULIZA
 
Hawa jamaa kweli watakuwa wametuibia lakini findings za kamati hizi kuhusu viwango vya madini na hasara tuliyopata, mimi binafsi zinanipa mashaka sana na ninaona tunaweza kuja kuumbuka hapo baadae.

Ni hivi,kama mchanga tu unaweza kuwa na madini ya thamani ya trilioni mpaka 380.9 kwa kiwango cha juu kwa miaka hiyo 19,ni wazi nchi zenye rasilimali madini duniani na zenye mikataba mizuri zingekuwa ni nchi tajiri sana katika huu ulimwngu.

Cha kujiuliza, kama hiyo ni thamani ya makinikia tu,madini yenyewe(matofali ya dhahabu) yatakuwa na thamani kiasi gani kwa miaka yote hiyo?

Alafu kingine cha kujiuliza ni kwanini findings za kamati hizi mbili za sasa na ile ya Jaji Bomani zitofautiane katika data za viwango vya madini tu lakini zifanane katika matokeo mengine ikiwemo na mapendekezo?Tukumbuke hata hadidu za rejea zimeonekana kufanana kwa maelezo ya Lissu aliyoyatoa Bungeni jana huku akiwa na ripoti ya Jaji Bomani mkononi.

Kubiwa ni kweli tumeibiwa lakini hivyo viwango vya madini vilivyotajwa katika hizo ripoti inabidi tujiulize mara mbili mbili kama kweli vina uhalisia na hali ya nchi zingine zenye migodi tena kutuzidi.

Hizi ripoti hawa mabwana wanaweza kuzitafsiri kama ni defamatory kwao na hivyo tunaweza kuwa sued for defamation japo wametubia unless tuthibitishe usahihi wa hivyo viwango vya madini.
Tafuta mtu mmoja tu anayefanya kazi mgodi wowote Tanzania afu muulize contractor company hata moja inavyolipwa afu uje ulete mrejesho. Ni zaidi ya hizo pesa ndugu.
 
TUPE WASIFU WA HUYO MTU ULIMUULIZA
Sijui kama itasaidia maana waliotajwa
kuhujumu nchi wasifu wao ni wa kutisha.
Hata mh. rais alisema BOT kuna PhD 17.
cha msingi na wewe fanya utafiti wako
wafanyakazi wa migodi hii tena processing room
wapo mitaani,tunaishi nao
 
Sijui kama itasaidia maana waliotajwa
kuhujumu nchi wasifu wao ni wa kutisha.
Hata mh. rais alisema BOT kuna PhD 17.
cha msingi na wewe fanya utafiti wako
wafanyakazi wa migodi hii tena processing room
wapo mitaani,tunaishi nao
Isije ikawa ni hearsay stories ya watu wa vijiweni, need credible source. Sikatai post yako, hapana, tunataka uhakika wa source kama ni credible


Ona hii sasa ( ni uzi nimekopi JF for easy of reference, na uzi link nimeiweka chini.)
Nimeshangaa ile kamati ya pili iliyosheheni walimu wa chuo kikuu wameshindwa kutofautisha ACCACIA kama brand name iliyosajiliwa huko nje ikiwa na sub contract na Bulyanhulu Gold mine Tanzania.

Cha kusikitisha kwenye ile kamati alikuwepo mtu wa TRA tena afisa mwandamizi anayejua kodi hawakusanyi kwa jina la ACCACIA kama brand name bali wanakusanya kama Bulyanhulu Gold mine.

Kwa ufupi nina mashaka na uelewa wa huyu Profesa anayefundisha mambo ya Oligopolistic competition huko chuo kikuu,Kamati imemdanganya Raisi kweupe kuwa ACCACIA as brand name inafanya kazi kinyume cha sheria,

Profesa ameshindwa kuelewa ACCACIA sio kampuni bali wanafanya kazi na sub contractors kama Bulyanhulu Gold mine na zingine nyingi zilizopo huko mgodini
Kamati ya Profesa Osoro na uelewa wa Multinational Corporatios
 
Sasa unadhani mamlaka ya bandari wangekubali uache kontena lako kwenye bandari likaharibu propela za meli?

Unajua gharama za kuharibu propela ya meli ? Au unadhani mamlaka ya bandari wangekubali uache kontena karibu na mahali meli zinapaki? Ili ziligonge zianguke?
Daah!! Umenipa elimu kubwa nafikiri wengine tunachangia bila tafakari
 
Hawa jamaa kweli watakuwa wametuibia lakini findings za kamati hizi kuhusu viwango vya madini na hasara tuliyopata, mimi binafsi zinanipa mashaka sana na ninaona tunaweza kuja kuumbuka hapo baadae.

Ni hivi,kama mchanga tu unaweza kuwa na madini ya thamani ya trilioni mpaka 380.9 kwa kiwango cha juu kwa miaka hiyo 19,ni wazi nchi zenye rasilimali madini duniani na zenye mikataba mizuri zingekuwa ni nchi tajiri sana katika huu ulimwngu.

Cha kujiuliza, kama hiyo ni thamani ya makinikia tu,madini yenyewe(matofali ya dhahabu) yatakuwa na thamani kiasi gani kwa miaka yote hiyo?

Alafu kingine cha kujiuliza ni kwanini findings za kamati hizi mbili za sasa na ile ya Jaji Bomani zitofautiane katika data za viwango vya madini tu lakini zifanane katika matokeo mengine ikiwemo na mapendekezo?Tukumbuke hata hadidu za rejea zimeonekana kufanana kwa maelezo ya Lissu aliyoyatoa Bungeni jana huku akiwa na ripoti ya Jaji Bomani mkononi.

Kubiwa ni kweli tumeibiwa lakini hivyo viwango vya madini vilivyotajwa katika hizo ripoti inabidi tujiulize mara mbili mbili kama kweli vina uhalisia na hali ya nchi zingine zenye migodi tena kutuzidi.

Hizi ripoti hawa mabwana wanaweza kuzitafsiri kama ni defamatory kwao na hivyo tunaweza kuwa sued for defamation japo wametubia unless tuthibitishe usahihi wa hivyo viwango vya madini.


!
!
Ndio aina ya maprofesa wetu wale.
 
Dollar za Zimbabwe au Marekani?

Dollar za Marekani milioni kumi kwa bei ya dhahabu ya leo ( about $40 per g) unanunua dhahabu tani 25.

Pure gold. 25 tons.

Hilo kontena lilikuwa na gold bars au nini?

Unafahamu density ya dhahabu?

Unafahamu ujazo wa container la futi 40?

Container la futi 40 lina 67.7 meter cube.

Gold ina density ya 19.32 g/ cm cube. Thats 19320 g / m cu.

That's 19.32 kg / m cube.

Thats about 1308 kg per 67.7 meter cube (19.32 x 67.7).

1308 kg at 40 US $ per gram, todays price = 1,308,000 × 40 = 52.32 million USD.

(10÷52.32) x 100 = 19.11

Sasa hilo container lilikuwa limejaa pure gold karibu 20% ya ujazo wake?
Mkuu tani moja ina kilo ngapi? kwa mahesabu yangu dola elfu kumi inanunua kilo 275 ya dhahabu
kwa gharama ya shilingi milioni themanini kwa kilo.Huenda nimekosea naomba nisahihishe.
 
Back
Top Bottom