Sakata la Mahujaji: Utendaji ATCL na Yaliyojiri Hadi Leo Hii

mhhh sasa hii kazi kweli kweli


Mahujaji Dar: Kumbe hakuna aliyepaa jana!

2007-12-12 16:34:22
Na Sabato Kasika na Sharon Sauwa, Jijini


Licha ya taarifa njema zilizoripotiwa leo asubuhi kuwa baadhi ya mahujaji waliokwama katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini wamepaa jana kwenda Makka, ukweli ni kwamba hakuna hujaji hata mmoja aliyesafiri.

Badala yake, imefahamika kuwa mahujaji hao wameendelea kusota tena usiku wa jana na kupewa matumaini mengine kuwa huenda wangeanza kuondoka leo.

Akizungumza na Alasiri leo asubuhi, mmoja wa viongozi wa msafara huo wenye mahujaji zaidi ya 1,000, Sheikh Saleh Issa wa wakala wa Hajji Trust, amesema yeye na mahujaji wengine zaidi ya 300 walipanda ndege mishale ya saa 4:00 usiku jana na kukaa kwenye siti zao.

Akieleza zaidi, Sheikh Issa akasema badala ya safari kuanza, wakastukia wakishushwa ndani ya ndege hiyo kutokana na maelezo kuwa kuna taratibu fulani za ndege hiyo kutua Jijini Jeddah kule Saudi Arabia hazikuwa zimetimizwa.

``Tulielezwa kuwa hakukuwa na kibali cha kuingilia Jeddah? pia tukaelezwa mambo mengine kadhaa yaliyowalazimu wahusika kutushusha na kuahirisha safari,`` akasema Sheikh Issa.

Hata hivyo, Sheikh Issa akasema waliambiwa kuwa masuala yote tata kuhusiana na safari ya ndege hiyo yangekamilishwa mapema, hivyo leo wangeweza kusafiri huku mahujaji wengine wakiendelea kusubiri.

Kiongozi mwingine wa msafara huo ambao pia una baadhi ya mahujaji toka nchi jirani ikiwemo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC), Sheikh Ali Mia, amesema kilichotokea hadi wakashushwa, ni kutokamilika kwa baadhi ya taratibu ikiwemo ya kibali na pia, kutekelezwa kwa kanuni za kimataifa kuhusiana na usafiri wa anga.

Akifafanua, akasema Sheikh Ali kuwa abiria walipanda kwenye ndege hiyo mishale ya saa 3:00 na ilipotimu saa 4:30 usiku wakaambiwa washuke kwani ni ukiukwaji wa kanuni, usiotaka abiria awe kwenye ndege zaidi ya saa moja bila kupaa.

``Hayo ni baadhi ya yale tuliyoyasikia? tunaendelea kuomba na bila shaka, kama Mungu amepanga kuwepo kwa safari hii, inshallah itakuwepo tu,`` akasema Sheikh Ali.

Hata hivyo, kuna taarifa kuwa mwisho wa kuingia ndege za mahujaji nchini Saudi Arabia ni kesho, na kwamba baada ya hapo hakuna itakayoruhusiwa kuingi nchini humo.

Sakata la kukwama kwa mahujaji hao limeanza tangu Desemba 3 mwaka huu ambapo badala ya kusafirishwa na ndege waliyolipia na kuingia nayo mkataba ya ATC, mahujaji hao wakaambiwa wasubiri kwani ndege iliyotazamiwa ni mbovu.

Kuanzia hapo, wakawa wakipigwa danadana kila kukicha hadi Serikali ilipoingilia suala hilo na kutaka wasafirishwe kwa ndege nyingine zilizokodiwa nchi za Ureno na Hispania.

Katika hatua nyingine, viongozi kadhaa wa kitaifa waliendelea kufika katika uwanja huo ili kuwapa pole mahujaji hao akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa, Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Abbas Kandoro.


SOURCE: Alasiri
 
"If I had served my God as diligently as I did my king, He would not have given me over in my grey hairs." Thomas Cardinal Wolsey (1473-1530), Archbishop of York, Lord Chancellor and Chief Aide to King Henry VIII.

KITHUKU,
YAANI SAHIHI YAKO NIMEIPENDA TU SANA! SASA HIZO MVI SII AMEKUWA MZEE? JE WAPEWE VIJANA BADALA YA WAZEE? HA HA HA HA?

Asante kwa kupenda sahihi yangu. Kama umesoma historia ya Europe (England mumo ndani), utakuwa ushasikia habari ya Mfalme Henry VIII, ambaye alikuwa fisadi-kiwembe (alioa mara 6), na ndiye aliyeanzisha Church of England na kuwa mkuu wake wa kwanza. Kabla ya uamuzi wake huo, alikuwa ameweka masuala yote ya nchi chini ya mamlaka ya Cardinal Wolsey, ambaye alijisahau kabisa, badala ya kumtumikia Mungu akawa anamtumikia mfalme Henry! Na kwa kupenda kwake ufahari na kujionesha kwa watu kwamba ni mcha Mungu, Mfalme Henry alitaka kumpa talaka "halali" mkewe Malkia Catherine ili amwoe kimada wake aliyeitwa Ann Boleyn. Ndipo Cardinal Wolsey aliyekuwa na madaraka makubwa katika kasri ya mfalme alipopewa jukumu la kufuatilia talaka hiyo, na kuhakikisha inapatikana toka Vatican, ili aweze kumwoa Ann Boleyn "kihalali". Bahati mbaya Pope Clement aliyekuwapo wakati huo, akakataa katakata kutoa ruhusa hiyo ya talaka, na ndipo kwa ushawishi wa kimada wake Ann, mfalme akavunja uhusiano na Vatican, akajisimika kuwa mkuu wa kanisa, na akamgeuzia kibao Cardinal Wolsey, akamfukuza kazi na baadae akaamuru akamatwe kwa kosa la uhaini. Hayo maneno yaliyoko kwenye hiyo sahihi yangu aliyasema Cardinal Wolsey siku anakamatwa, akijutia muda wake na bidii kubwa aliyotumia kumtumikia Mfalme Henry VIII kuliko alivyomtumikia Mungu, akisema laiti angemtumikia Mungu kama alivyomtumikia Mfalme, Mungu asingemuacha katika siku za uzee wake (ndiyo hizo "grey hairs"). Nadhani hali kama hizi zipo hadi leo hii, kwa hiyo tuna mengi ya kujifunza, ndio maana nayatumia haya maneno kwenye sahihi yangu.
 
Safari ya Mahujaji yaiva

2007-12-12 09:24:47
Na Eshy Mushi

Hatimaye, kundi la kwanza la Mahujaji zaidi ya 1,000 waliokuwa wamekwama kwa siku nane kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, jana lilifanikiwa kuondoka kwenda kuhiji Mecca, Saudi Arabia.


Mahujaji hao walipanga kusafiri Desemba 3, mwaka huu lakini walikwama na kuendelea kusota kwenye viwanja vya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa muda wote huo.

* SOURCE: Nipashe

This is unforgivable! Yaani mtu aliyegharamia safari yake anacheleweshwa kwa siku zote hizo? Imagine tangu tarehe 3, ni karibu siku 9! Jamani, this is extremely unfair, na yeyote anayewatetea hao ATC sitamwelewa kamwe! Ucheleweshaji wa siku 1 au 2 nadhani ungevumilika, tunaosafiri mara kwa mara tunaelewa mambo haya hutokea na mashirika husika huwajibika ipasavyo. Lakini siku 9! This is utterly ridiculous, unacceptable by any description on earth! Nasubiri kuona hatua itakayochukuliwa, na namshauri anayehusika asiogope kutuhumiwa udini kwani huu ulikuwa utaratibu wa KIBIASHARA, si wa kidini. Sidhani kama ATC walikuwa wanajitolea sadaka kusaidia mahujaji, ingekuwa hivyo tungelalamika udini. Lakini ATC walichangamkia nafasi ya biashara kusafirisha abiria hao, na imekiuka mkataba na kuwadhalilisha abiria wake. Mwungwana kaka yetu JK kwa kuwa alishaingilia kati hili suala, namwomba amalizie, asiishie tu kukodisha ndege imetoka, no! Ni suala la kutetea haki za watumiaji wa hivi vyombo. Kama watu zaidi ya 1,000 wanaweza kufanyiwa uzembe kiasi hicho na yakapita hivihivi, sijui nikiwa peke yangu na mke wangu tumedhulumiwa nani atakayetutetea? Anzia hapa, lazima tujenge utamaduni wa uwajibikaji na kuwatetea raia wetu. Narudia: Nasubiri kuona hatua atakayochukua mheshimiwa Rais katika sakata hili.
 
kwa uwezo wake muumba mbingu na ardhi kundi la mwanzo kwa mujibu wa bbc limeshaondoka na nnaomba wote wasafiri kwa salama
 
Waziri Mkuu Mhe. Lowassa ameahirisha kwa muda safari yake ya kwenda Bukoba kwenye sherehe ya siku ya Uvuvi duniani ili kubakia jijini Dar, ili aweze kushughulikia sakata la mahujaji ambao wamepiga kambi Uwanja wa ndege. Waziri Mkuu anataka kuhakikisha kuwa mahujaji wote wanaondoka kama ilivyotakiwa.
 
Waziri Mkuu Mhe. Lowassa ameahirisha kwa muda safari yake ya kwenda Bukoba kwenye sherehe ya siku ya Uvuvi duniani ili kubakia jijini Dar, ili aweze kushughulikia sakata la mahujaji ambao wamepiga kambi Uwanja wa ndege. Waziri Mkuu anataka kuhakikisha kuwa mahujaji wote wanaondoka kama ilivyotakiwa.

ndio vizuri, ndivyo inavyotakiwa kiongozi kujali wananchi wake
 
Hii ni aibu kabisa ya serikali, ni dalili ya kushindwa kazi hao wahusika. Kama inahitajika waziri mkuu kwenda kufanya kazi hiyo, kuna haja gani ya kuwa na waziri katika sekta hiyo? Vipi kuhusu wakurugenzi sijui na kina nani huko wanatumalizia bure hela zetu kuwagharimia marupurupu kibao, wa nini wote hawa? Nitashangaa sana kama hatua za kinidhamu hazitachukuliwa katika tukio hili. Nitashangaa mno, nasema tena!
 
Waziri Mkuu Mhe. Lowassa ameahirisha kwa muda safari yake ya kwenda Bukoba kwenye sherehe ya siku ya Uvuvi duniani ili kubakia jijini Dar, ili aweze kushughulikia sakata la mahujaji ambao wamepiga kambi Uwanja wa ndege. Waziri Mkuu anataka kuhakikisha kuwa mahujaji wote wanaondoka kama ilivyotakiwa.

haya ndiyo mambo yanayoniudhi

mara tunaambiwa ohhh tusichanganye DINI na SIASA huku serikali iko involved na mambo ya kidini utafikiri nini sijui

Hii ni mess ya waislam na ATC na probably baraza kuu na Hajj trust sasa waziri mkuu anahirisha mambo muhimu ya serikali ili ili awaccomodate waislam

Najua ni un popular opinion humu JF lakini huu ni unafiki wa hali ya juu kabisa

sitoshangaa serikali ikaanza kutumia kodi za wasio waislam na wasio na dini ili kuwafurahisha hawa watu

 
Hii ni aibu kabisa ya serikali, ni dalili ya kushindwa kazi hao wahusika. Kama inahitajika waziri mkuu kwenda kufanya kazi hiyo, kuna haja gani ya kuwa na waziri katika sekta hiyo? Vipi kuhusu wakurugenzi sijui na kina nani huko wanatumalizia bure hela zetu kuwagharimia marupurupu kibao, wa nini wote hawa? Nitashangaa sana kama hatua za kinidhamu hazitachukuliwa katika tukio hili. Nitashangaa mno, nasema tena!

mambo haya na serikali wapi na wapi au nyie mnapenda mambo haya ya kuwafuturisha kisha kuacha kufanya shughuli za kitaifa ili watafutiwe usafiri wa kwenda kuhiji

jamani acheni haya mambo ya kufuata mikumbo tuuu

waziri anahusiana nini na kuwasafirisha hawa watu huko wanakotaka kwenda?

whats next?

wapewe na pocket money? kama waliweza kuandamana kupinga mabucha ya nguruwe wameshindwa vipi kwenda kuweka kambi ofisi za Tanesco pale mjini?

 
at whose expense?
hivi kodi zetu kazi yake ni kuwasafirisha watu kwenda kuhiji au? kesho wakitaka wanunuliwe kanzu serikali itakubali au ndio mamabo ya political correctness?

Kwani hao waliokosa Usafiri hawalipi Kodi?? Au wewe pekee ndio unajiona mlipa Kodi, gimme a break.
 
Halafu serikali inatuambia tusichanganye dini na siasa wakati yenyewe imejaa UDINI both overtly na covertly. Sasa wanatumia pesa za walipa kodi ili kuwafurahisha hawa watu.

Mbona waislam wakilalamika mambo ya muhimu hawa viongozi hawaonekani? this is beggars belief jinsi wanavyofuja kodi za wasiowaislam ili kuwa PC!
 
Halafu serikali inatuambia tusichanganye dini na siasa wakati yenyewe imejaa UDINI both overtly na covertly. Sasa wanatumia pesa za walipa kodi ili kuwafurahisha hawa watu.

Mbona waislam wakilalamika mambo ya muhimu hawa viongozi hawaonekani? this is beggars belief jinsi wanavyofuja kodi za wasiowaislam ili kuwa PC!
Hawa abiria wote wamelipa nauli karibia $2400 kwa hiyo safari, na kampuni iliyokuwa na jukumu la kuwasafirisha ni ATC ambayo ni Shirika la Serikali. Asilimia kubwa ya hawa watu ni Watanzania na walipa kodi ile wa nchi, Lowassa au Kikwete kama viongozi wa nchi wana haki sawa kabisa ya kuwasaidia wananchi wao ambao wako kwenye matatizo. Unajua watu wengine kama nyinyi kazi yenu kuandika PUMBA TU HUMU ndani bila ya kufikiria.
 
Kwani hao waliokosa Usafiri hawalipi Kodi?? Au wewe pekee ndio unajiona mlipa Kodi, gimme a break.

lakini serikali si huwa inasema :


TUSICHANGANYE DINI NA SIASA?

HAINA DINI

INAWACHAGULIA WAISLAM VIONGOZI

HAITAKU KUWEPO KWA KADHI

INASEMA MAMBO YA KAISARI MWACHIE KAISARI

Nakubali hawa watu huwa wanalipa kodi ili wapate huduma za jamii kama ilivyo kwenye social contract baina ya watawala na watawaliwa. Sasa serikali kutumia kodi za wananchi ili kuwa accomodate waislam ni jambo ambalo kwa kweli naona halikutakiwa kuwepo kabisa

Serikali yetu ni ya kisecular lakini mbona iko heavily involved na mambo ya kidini?

Nyimbo ya Taifa imekaa kidini dini tuuu

sasa kama si unafiki ni nini hicho?

Hao ATC wana mapesa kibao tuu na kama issue ilikuwa btn ATC na waislma then serikali ikae pembeni lakini siyo Serikali nzima kuhamia AIRPORT...huku ikiacha mamabo ya kitaifa pembeni
 
Huu uongozi una shaka sana

Ina maana ikitokea treni la kwenda mwanza likakosa na watu tayari wanaticketi zao mkononi hii ina implies kwamba WAZIRI MKUU ataacha safari za kitaifa na kuwatafutia usafiri mbadala watu hawa??/
LOWASA NA SERIKALI YAO NI AKINA ZEROOOOOOOOOOOOOOOOO
 
Hawa abiria wote wamelipa nauli karibia $2400 kwa hiyo safari, na kampuni iliyokuwa na jukumu la kuwasafirisha ni ATC ambayo ni Shirika la Serikali. Asilimia kubwa ya hawa watu ni Watanzania na walipa kodi ile wa nchi, Lowassa au Kikwete kama viongozi wa nchi wana haki sawa kabisa ya kuwasaidia wananchi wao ambao wako kwenye matatizo. Unajua watu wengine kama nyinyi kazi yenu kuandika PUMBA TU HUMU ndani bila ya kufikiria.

Lakini serikali si huwa inasema :


TUSICHANGANYE DINI NA SIASA?

HAINA DINI

INAWACHAGULIA WAISLAM VIONGOZI

HAITAKU KUWEPO KWA KADHI

INASEMA MAMBO YA KAISARI MWACHIE KAISARI

Nakubali hawa watu huwa wanalipa kodi ili wapate huduma za jamii kama ilivyo kwenye social contract baina ya watawala na watawaliwa. Sasa serikali kutumia kodi za wananchi ili kuwa accomodate waislam ni jambo ambalo kwa kweli naona halikutakiwa kuwepo kabisa

Serikali yetu ni ya kisecular lakini mbona iko heavily involved na mambo ya kidini?

Nyimbo ya Taifa imekaa kidini dini tuuu

sasa kama si unafiki ni nini hicho?

Hao ATC wana mapesa kibao tuu na kama issue ilikuwa btn ATC na waislma then serikali ikae pembeni lakini siyo Serikali nzima kuhamia AIRPORT...huku ikiacha mamabo ya kitaifa pembeni

Mbona watanzania wengine walipa kodi wakikwama safari zisizo za kidini na ATC hao watawala huwa hawaonekani airport?





 
Waziri Mkuu Mhe. Lowassa ameahirisha kwa muda safari yake ya kwenda Bukoba kwenye sherehe ya siku ya Uvuvi duniani ili kubakia jijini Dar, ili aweze kushughulikia sakata la mahujaji ambao wamepiga kambi Uwanja wa ndege. Waziri Mkuu anataka kuhakikisha kuwa mahujaji wote wanaondoka kama ilivyotakiwa.

Hii ni aibu sana. Ni kweli hao ndugu zetu wa kwenda Mecca wanateseka sana na ni wajibu wa ATC kuwapatia ufumbuzi haraka sana. lakini Waziri mkuu ni mtu mkubwa sana na si sahihi kufanya kazi kama kiranja wa zamu hapo airport. Sijui kama mwenyewe anajua hilo.

Kwa nini wasiuwajibishe uongozi wa ATC? Au kwa nini asimwachie hiyo kazi waziri anaehusika na usafiri na mawasiliano.
Hiyo kazi wangemwachia japo Kandoro amalizane nayo au meya wa jiji.

Labda kama kuna madili mengine anataka kufanya hapo ikulu baada ya Jk kuondoka.

Kwa upande mwingine ni kama anatuonyesha kuwa sekta ya uvuvi sio ya maana sana.
 
Hii ni aibu sana. Ni kweli hao ndugu zetu wa kwenda Mecca wanateseka sana na ni wajibu wa ATC kuwapatia ufumbuzi haraka sana. lakini Waziri mkuu ni mtu mkubwa sana na si sahihi kufanya kazi kama kiranja wa zamu hapo airport. Sijui kama mwenyewe anajua hilo.

Kwa nini wasiuwajibishe uongozi wa ATC? Au kwa nini asimwachie hiyo kazi waziri anaehusika na usafiri na mawasiliano.
Hiyo kazi wangemwachia japo Kandoro amalizane nayo au meya wa jiji.

Labda kama kuna madili mengine anataka kufanya hapo ikulu baada ya Jk kuondoka.

Kwa upande mwingine ni kama anatuonyesha kuwa sekta ya uvuvi sio ya maana sana.


SERIKALI YETU INAPENDA KUCHANGANYA DINI NA SIASA

its that simple

serikali hiii huwa inawachagulia waislam wafunge mwezi wa Ramadhani lini na wafungue lini na waswali lini

The bottom line waislam esp waislam wa BAKWATA na serikali wanajuana
 

lakini serikali si huwa inasema :


TUSICHANGANYE DINI NA SIASA?

HAINA DINI

INAWACHAGULIA WAISLAM VIONGOZI

HAITAKU KUWEPO KWA KADHI

INASEMA MAMBO YA KAISARI MWACHIE KAISARI

Nakubali hawa watu huwa wanalipa kodi ili wapate huduma za jamii kama ilivyo kwenye social contract baina ya watawala na watawaliwa. Sasa serikali kutumia kodi za wananchi ili kuwa accomodate waislam ni jambo ambalo kwa kweli naona halikutakiwa kuwepo kabisa

Serikali yetu ni ya kisecular lakini mbona iko heavily involved na mambo ya kidini?

Nyimbo ya Taifa imekaa kidini dini tuuu

sasa kama si unafiki ni nini hicho?

Hao ATC wana mapesa kibao tuu na kama issue ilikuwa btn ATC na waislma then serikali ikae pembeni lakini siyo Serikali nzima kuhamia AIRPORT...huku ikiacha mamabo ya kitaifa pembeni

ATC ni shirika la Serikali na viongozi wake huteuliwa na Rais kwa hiyo bosi wao Mkuu ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hakuna kipengele kinachosema kuwa Mtanzania akipata matatizo katika masuala yake yanayohusiana na dini basi asisaidiwe kisa tu serikali yetu haichanganyi dini na siasa. Mbona Mrema na Lowassa walienda kusuluhisha migogoro kibao ya kule ARUSHA kwenye KKKT kwenye Dayosisi ya Meru?? Hayo yote ni majukumu ya serikali hasa yanapotea matatizo yanayowahusu wananchi wake na sioni tatizo lolote.
 
Back
Top Bottom