Sakata la kuuzwa UDA: Kauli za Idd Simba, Masaburi, Kisena et al utata mtupu

Hivi Idd Simba huyu ndo yule aliyeyeyuka na matumaini ya watz kwenye NICO; Na yule wa vibali vya importation ya sukari vilivyomfukuzisha uwaziri Viwanda na Biashara ni Ndugu au ndo huyohuyo??
 
Ndugu yangu, Ni heri Jakaya Kikwete ambaye hajachukua na kuwa na Damu ya Mwanadamu mwilini Mwake, ila ni kuipa rasilimali ambazo atakufa na kuziacha na ametuacha sisi salama na umasikini wetu; Kuliko Huyo Rais Paul Kagame ambaye ana Damu za watu wengi ambao wani waaminifu na hawana hatia, kwasababu ya ulafi wa madaraka akaamua kuingia porini na kuua maadui zake; Heri Jakaya Kikwete simpendi lakini ameniacha huru nakufa na umasikini wangu

Labda hujasikia waliofunikwa kwenye machimbo kule Shy, na wengine wanaokufa kwa kukosa huduma kwenye hospitali zetu. Yaani anawaua huku nacheka. Hili Fisadi papa iko siku yake.
 
Mjanja kazidiwa ujanja na mjanja mwenzake. Muuza dhahabu feki kapewa pesa bandia.
 
tunachinjana wenyewe kwa wenyewe. huu ni sawa na uuaji kwani kwa kufanya hivyo maslahi na maisha ya watanzania wengi yako hatarini.
eee mwenyezi mungu wape moyo wa uoga wote wenye moyo wa namna hii!
kweli inaudhi, lakini TIME WILL TELL!

"Nchi hii tunaitafuna wenyewe siku tukiimaliza tutafunana wenyewe" Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Club ya Simba na Mbunge wa Tabora Mjini (CCM) Mh. Ismail Aden Rage. Anashangazwa na utajiri wa wafanyakazi wa serikali kumilki guest house 20, ukimuuliza chanzo cha mapato ya ujenzi wa miradi hiyo nini, hana cha kukupa? Mfanyakazi wa serikali anamiki mali kupita mfanyabiashara.
 
Uuzwaji wa UDA kwa Simon Group ni kwa faida ya walalahoi wa Dar es Salaam, watanzania ni watu wa ajabu sana, angekuwa ameuziwa mgeni msingekuwa na tatizo lolote lakini leo kauziwa mtanzania mwenzenu basi maneno kibao,lipi jema kwenu, acheni wivu,*
 
Hapa nenda www.usanii-tanzania.co.tz lakini haipo. Ni wazo tu. Hivi kukiwa na website ya kuchakachua ... I mean KUJADILI ... skendo zote za ubinafsishaji holela wa makampuni ya umma, watu si watapata pa kuongelea, na kulipua mabomu hayo? Na wenye kutangaza biashara zao je? Si watatangaza? Haya, sasa, mshapata dili, lihangaikieni!
 
"Moja, barua ni ya kughushi, kwa sababu Meneja wa UDA, Milanzi hakuandika barua wala hakukuwa na maagizo yoyote ya yeye kulipia hisa zake kupitia akaunti binafsi. Hilo jambo lisingewezekana.

"Lakini ieleweke kwamba muda mrefu kabla ya tukio hilo na katika shughuli ambazo hazihusiani hata kidogo na UDA, zilizotokana na ushauri wa jumla wa kibiashara aliotaka kutoka kwangu, alikuwa anastahili kulipa fedha zangu binafsi. Nilitoa amri ya kulipia katika akaunti yangu, alifanya hivyo kwa awamu tofauti kadri nilivyotoa maagizo."

Akizungumza mbele ya mwanasheria wake, Bw. Simba alipoulizwa iwapo watu hawawezi kuhoji mgongano wa maslahi ulio wazi katika suala hilo, la Simon Group kununua hisa katika shirika (UDA) ambalo yeye ni mwenyekiti wa bodi, huku pia wakati huo huo yeye akitoa ushauri wa kibiashara kwa kampuni iliyotaka kununua UDA, alisema;

"Ndiyo wanaweza kuhoji...lakini sasa mimi si mtumishi wa umma, pale UDA mimi si mwajiriwa. Mimi nauza maneno, natoa ushauri. Ukija kutaka ushauri siwezi kukutalia. Lakini kwenye bodi tulikuwa serious sana. Tatizo ni kwamba mwanzoni sikutilia maanani sana tabia ya Robert Kisena, kwa sababu mimi nilikuwa na hamu sana mzawa achukue UDA, siyo kila kitu nchi hii anachukua mwekezaji mgeni," alisema Bw. Simba.

Alisema kwamba inasikitisha kuona mpaka sasa serikali haijachukua hatua yoyote kuinusuru UDA, akionesha matumaini yake kwa CHC itachukua hatua za haraka kurejesha hali ya kawaida katika shirika hilo muhimu la usafiri Dar es Salaam, pia kwa kamati iliyoundwa kuchunguza suala hilo.

Wakati Bw. Simba akisema kuwa fedha zilizowekwa katika akaunti yake binafsi hazina uhusiano wowote na uuzwaji wa UDA, Bw. Kisena amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema kuwa hawakuwahi kuwa na shughuli nyingine tofauti na hiyo ya ununuzi wa shirika hilo la umma.

Akinukuliwa katika moja ya magazeti ya kila siku jana, Bw. Kisena alisema kuwa walilipa fedha hizo katika akaunti ya Bw. Simba, kama sehemu ya malipo ya ununuzi wa UDA, kutokana na maelekezo ya uongozi wa UDA, akisema kuwa anazo nyaraka zinazoonesha hivyo.

Hapo chacha
 
Uuzwaji wa UDA kwa Simon Group ni kwa faida ya walalahoi wa Dar es Salaam, watanzania ni watu wa ajabu sana, angekuwa ameuziwa mgeni msingekuwa na tatizo lolote lakini leo kauziwa mtanzania mwenzenu basi maneno kibao,lipi jema kwenu, acheni wivu,*

Mkuu,

Katika makubaliono ya mauzo ya UDA (ambayo hata hivyo hayatambuliwi kisheria), Simon Group Limited ilitakiwa kulipa Sh1.4 billion kwa shares 51. Hata hivyo Simon Group Ltd imelipa Sh285 million (asilimia 12 tuu ya malipo yote) na kukabidhiwa UDA. Unaona hili ni sasa sawa kabisa? Kwa vile basi ameuziwa mzawa basi unaona hilo ni sawa? Walalahoi wamepata faida gani hapo? Yaani wewe ni mtu wa ajabu sana. Hakuna cha wivu hapa. Tumewashika pabaya. Na bado mtasemana, tena sana.
 
Mkuu,

Katika makubaliono ya mauzo ya UDA (ambayo hata hivyo hayatambuliwi kisheria), Simon Group Limited ilitakiwa kulipa Sh1.4 billion kwa shares 51. Hata hivyo Simon Group Ltd imelipa Sh285 million (asilimia 12 tuu ya malipo yote) na kukabidhiwa UDA. Unaona hili ni sasa sawa kabisa? Kwa vile basi ameuziwa mzawa basi unaona hilo ni sawa? Walalahoi wamepata faida gani hapo? Yaani wewe ni mtu wa ajabu sana. Hakuna cha wivu hapa. Tumewashika pabaya. Na bado mtasemana, tena sana.

Mkuu sana ETM

UDA wameuza share 51% kwa Simon Group kwa gharama ya 1.2 bil makubaliano ilikuwa ni kwa Simon Group kulipa fedha hiyo kwa mikupuo kadhaa, aliyewaingiza mkenge watanzania ni mwenyekiti wala siyo Simon Group.

Mkuu UDA ina mali za zaidi ya 13.5 billion, viongozi wenu wameuza 51% shares at 1.2 bil, kweli.????..

Halafu watu badala ya kuhoji maswala ya msingi kama haya, mnaendekeza roho ya wivu, hapana siyo vizuri.
 
Ndugu yangu, Ni heri Jakaya Kikwete ambaye hajachukua na kuwa na Damu ya Mwanadamu mwilini Mwake, ila ni kuipa rasilimali ambazo atakufa na kuziacha na ametuacha sisi salama na umasikini wetu; Kuliko Huyo Rais Paul Kagame ambaye ana Damu za watu wengi ambao wani waaminifu na hawana hatia, kwasababu ya ulafi wa madaraka akaamua kuingia porini na kuua maadui zake; Heri Jakaya Kikwete simpendi lakini ameniacha huru nakufa na umasikini wangu

Unasahau kuwa JK ndiye aliykabidhiwa maisha watanzania wote na akaapa kuwalinda - wanapokufa Nyamongo, Arusha na kwingineko nani kawauwa? Siyo lazima yeye ashike Machine gun, hata kunyamazia uozo kama utapelekea kufa kwa raia wewe ndiye unayewajibika. Akikuacha umaskini na njaa yako ikikuua katikati ya asali na utajri wa rasilimali anazogawia wageni -nani kakuuwa?
 
Serikali inasubiri nini kuwakamata wote na kuwanyonga?ushaidi upo wazi so wanachunguza nini?

Utaambiwa kama una ushahidi upeleke .. teh teh The comedy ya TAKUKURU na Polisi yetu ni zaidi ya ze comedy.

Mtu anahusika kutika kuliuza shirika na mtu huyo huyo anahusika eti kutoa consultancy ya kulinunua shirika hlo hilo. Bado hapo watakumbia TAKUKURU na Polisi watakumbia hakuna ushahidi.


BTN

Jamani tueleezane kampuni ya Idd simba inatoa cosultancy gani ili nasi wazawa tunufaike na consultancy zake. na ofisi za hiii consultacy firm iko wapi tutafute uwezekanao wa kuwatembelea. tujue wapi tuanzie
 
Namkubuka sana Mh Iddi Simba na issue ya sukari za Jeshi bandarini kwenda kule Coca, nilijua mzee amestaafu kumbe anapiga kimya kimya
 
Idd Simba mwizi na Robert Kisena mwizi sijui kwanini hawakamatwi na kuwekwa lupango haraka sana ili kuanza kuwahoji kwa wizi waliotaka kuufanya.
 
Kumbukumbu zangu zinasema Mzee Kisena ni mmoja wa wanachama wandamizi wa CCM maana aligombea na Shibuda akamshinda... soma hapa utakumbuka kitu...."Mr Shibuda was on Thursday whisked away from his campaign rally at Kizungu soon after his supporters and those of his CCM rival clashed, leading to the death of Mr Steven Kwilasa, 26, who was said to have been the driver of the CCM candidate, Mr Robert Kisena."
 
Movie nyingine hiyoooooo, Tanzania raha sana! Mkuu wa kaya kesho anapanda pipa kuelekea ughaibuni kipitia middle east kula bata!!
 
Huyu babu hata sijui anagundu gani, uzee huu bado mwizi tu, nakumbuka aliwahi kuharibu akiwa waziri wa viwanda na biashara akajiuzulu kwa mkono wa mzindakaya, 'ukiishi kwa laana utakufa kwa laana tu!
 
hivi huyu Babake Saida Karumanga muliamua kumpa sekta muhimu wakati mnajua kuwa ni Mrundi/ Mkimbizi ili wawabakishie nini, huyu ni mzee wa Madili, si mnakumbuka kashfa ya sukari yeye na Mkuu wa Majeshi Mboma , jinsi walivyohujumu nchi kwa kuingiza sukari nyingi ya dili iliyosababisha Rais Mkapa amtoe kwenye wizara? Hamkumbuki kuwa ndiye Mwenye Miradi ya NICO ambayo ni utapeli mtupu, huyu ndiye aliyeutaka urais kwa kisingizio cha wazawa . Huyu ndiye Mamba bwana
 
Idd Simba mwizi na Robert Kisena mwizi sijui kwanini hawakamatwi na kuwekwa lupango haraka sana ili kuanza kuwahoji kwa wizi waliotaka kuufanya.

Hao Ni first class citizen no mater ufisadi waliofanya kufikishwa kwao hata polisi kuhojiwa uchumi wa nchi unaweza kuyumba. So ili uchumi undelee kukuwa wamewekewa taraibu zao mara wanapotakakiwa kucgunguzwa au kuhojiwa.

hayo mambo ya kukamatana ni kwa ajili ya 3rd class citizen.
 
Back
Top Bottom