Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Mpaka mpya wa Abyei
Sudan ya kusini na kaskazini zimesema kua zimekubali uamuzi wa Ma Jaji wa Mahakama ya Kimataifa juu ya mipaka.
Chini ya uamuzi huo wa Mahakama ya upatanishi eneo lenye visima vya mafuta la huko Abyei sasa limekabidhiwa mamlaka ya kaskazini.
Uamuzi huo umeweka mipaka mipya ya jimbo la Abyei ambalo katika kipindi kizima cha mgogoro wa miaka 22 lilikua kiini cha mvutano baina ya kaskazini na kusini.
Mipaka iliyopendekezwa baada ya mpango wa amani wa mwaka 2005 ilipingwa na viongozi wa kaskazini na hivyo ma jaji wa mahakama waliipuuza katika uamuzi wa sasa.
Hata hivyo waliamua kua sehemu kadhaa vikiwemo visima vya mafuta vya Heglig si sehemu ya Abyei.
Wadadisi wanasema kua ingawa jukumu la Mahakama ya The Hague lilikua juu ya mipaka ya Abyei na sio nani mmiliki wa ardhi hio, uamuzi huo utasaidia nani atamiliki visima vya mafuta.
SOURCE:BBC SWAHILI SERVICE