Sakata la kampuni ya kuweka rangi kwenye mafuta: Mikataba ulikuwa umebakiza muda gani kuisha na hawawezi kutupeleka mahakamani kwa kuuvunja mkataba?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Japo inadaiwa kuwa kampuni husika imetupiga hela nyingi (bilion 5 mpaka 7 kwa mwezi) lakini ukweli ni kuwa walikuwa wanatupiga kupitia mikataba tuliyoingia nayo wenyewe huku tukiwa na akili zetu timamu (hizo hela hawajatupora kwa mtupu wa bunduki)

Kwahiyo, kama tumevunja mkataba kinyume na makubaliano, basi upo uwezekano wa hawa mabwana kutushita, wakatushinda na tukalazimika kuwalipa mabilioni ya hela kama fidia kwa kuvunja mkataba.

Vile vile ilikuwa busara watanzania tukaelezwa mkataba husika ulikuwa umebakiza muda gani kumalizika kwani wanasiasa wetu hawa huwa wanafanya maamuzi pengine bila hata kuwa na taarifa za kutosha kuhusu jambo husika.

Tusishangile ushindi wa uwanjani wakati huenda kanuni za mchezo zimekiukwa kwani wenzetu hawa wanaweza kuja kupata point za mezani.

Time will tell.
 
Mkataba uliisha. Kampuni ilikuwa inapewa mkataba kila baada ya miaka 3 baada ya kushinda tender. Kumbuka hiyo kampuni ina miaka zaidi ya 10 ikifanya hiyo kazi.

Hivi karibuni mkataba wao uliisha, tender ikatangazwa wakawa wameshinda Intertek ( soma "The Citizen" )

Ila haijulikana ni nini kilitokea Intertek hawakupewa tender ( yasemekana kulikuwa na mazingira ya rushwa), hivyo hiyo kampuni ikawa bado inaendelea tu huku ikisubiri kitakachoamuliwa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom