Sakata la Jairo, kamati teule ya bunge si halali!

Danyel

Member
Sep 2, 2011
10
4
Kumbukumbu za bunge zinaonesha kuwa hoja ya Mh Sendeka kuhusu kuundwa kwa kamati teule ya bunge kuchunguza sakata la Jairo iliungwa mkono baada ya kutolewa lakini haikuafikiwa kwa mujibu wa kanuni za bunge!

Licha ya Naibu Spika kurejea kuisoma kanuni kabla ya kuamua,hakuwahoji wabunge ili hoja iafikiwe au la, kama kanuni inavyotaka mara baada ya hoja kutolewa na kuungwa mkono.inawezekana alipitiwa kutokana na jazba au ni usanii,lakini vyovyote iwavyo kamati teule iliyoundwa si halali kwakuwa haikuridhiwa na bunge.kwa maana hiyo serikali inaweza ikaikataa repoti ya kamati hiyo endapo itagundua mapungufu yanayoidhalilisha.

Licha ya upungufu huo wa kikanuni vile vile kamati teule pia inakwenda kwenye uchunguzi ikiwa inajua aliyewatuma (bunge) anataka nini, hivyo basi kwa kuwa wao pia ni sehemu ya bunge watakuwa kama mshtaki,muendesha mashata na jaji.
Tafakari!!!!!!
 
Napenda thread ambazo ni rahisi kumuumbua au kumthibitisha ukweli mtoa mada kama hizi, kwani ni kiasi cha kuachana na kila kitu na kujikita kwenye reference.

Reference yetu hapa ni kanuni za Bunge. Ole Sendeka alitumia Kanuni 117 inayotumiwa kuunda Kamati teule za Bunge. Sitoi kwanza maoni yangu nisiwe biased hivo naanza kuwaachia wachangiaji waisome between words Kanuni hii. Inasema hivi:

**************************************************************************************************************
117.-(1) Kamati Teule inaweza kuundwa na Bunge kwa madhumuni maalumu kwa hoja mahsusi itakayotolewa na kuafikiwa.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, baada ya kujadili hoja yoyote, Bunge linaweza kuunda Kamati Teule kwa madhumuni ya kushughulikia jambo lolote lililotokana na hoja hiyo kwa utaratibu ufuatao:-

(a) Baada ya hoja iliyokuwa ikijadiliwa kuamuliwa, Mbunge yeyote mwenye nia ya kutoa hoja chini ya Kanuni hii anaweza kusimama mahali pake na kutoa taarifa ya mdomo kwamba anakusudia kutoa hoja ya kuunda Kamati Teule;

(b) Mbunge ambaye anakusudia kutoa hoja ya kuunda Kamati Teule atawasilisha taarifa ya hoja yake kwa maandishi kwa Katibu na hoja hiyo itashughulikiwa wakati unaofaa kwa kuzingatia mpangilio wa shughuli kama ulivyoainishwa chini ya Kanuni ya 30 (4).

**************************************************************************************************************

Kazi kwetu wanaJF kuonyesha tumekwenda shule na tunaweza kuleta mabadiliko.

Jadili.

 
Toka niliposikia kwamba uchunguzi wa Meremeta unafanywa na Lowasa, na kama hiyo haitoshi, ripoyti atakabidhiwa Luhanjo ili "aitendee haki"! Mimi na mambo yenu ya siasa, baaaasi!!!!
Naungana na ndugu yangu Rostam Aziziiii!!!
 
kumbukumbu za bunge zinaonesha kuwa hoja ya Mh Sendeka kuhusu kuundwa kwa kamati teule ya bunge kuchunguza sakata la Jairo iliungwa mkono baada ya kutolewa lakini haikuafikiwa kwa mujibu wa kanuni za bunge!

Licha ya Naibu Spika kurejea kuisoma kanuni kabla ya kuamua,hakuwahoji wabunge ili hoja iafikiwe au la, kama kanuni inavyotaka mara baada ya hoja kutolewa na kuungwa mkono.inawezekana alipitiwa kutokana na jazba au ni usanii,lakini vyovyote iwavyo kamati teule iliyoundwa si halali kwakuwa haikuridhiwa na bunge.kwa maana hiyo serikali inaweza ikaikataa repoti ya kamati hiyo endapo itagundua mapungufu yanayoidhalilisha.

Licha ya upungufu huo wa kikanuni vile vile kamati teule pia inakwenda kwenye uchunguzi ikiwa inajua aliyewatuma (bunge) anataka nini, hivyo basi kwa kuwa wao pia ni sehemu ya bunge watakuwa kama mshtaki,muendesha mashata na jaji.
Tafakari!!!!!!
Unalipwa malipo kiasi gani kuleta propaganda uchwara hapa JF?
 
Toka niliposikia kwamba uchunguzi wa Meremeta unafanywa na Lowasa, na kama hiyo haitoshi, ripoyti atakabidhiwa Luhanjo ili "aitendee haki"! Mimi na mambo yenu ya siasa, baaaasi!!!!
Naungana na ndugu yangu Rostam Aziziiii!!!

Unaungana na RA kwa kuvua gamba au kufanya nini?
 
Ata wasipochukua hatua yoyote kwa jairo hatuwezi kushangaa kwani serikali yetu ni jambo la kawaida
 
Hahahahaaaaaa,daaa umenichekesha sana mdau,maana tangu awamu ya kwanza ya jk hadi sasa ni kipindi cha kamat,enz ya mkapa TUME ZILITAMBA
Toka niliposikia kwamba uchunguzi wa Meremeta unafanywa na Lowasa, na kama hiyo haitoshi, ripoyti atakabidhiwa Luhanjo ili aitendee haki"! Mimi na mambo yenu ya siasa, baaaasi!!!!
Naungana na ndugu yangu Rostam Aziziiii!!!
 
Jairo thing should now be given a rest and we need to move on other crucial matters for the betterment of our country. Its beyond me that over a bimester, folks' minds have engaged themselves into discussing this creature as if we have ran out of very serious matters.
 
Nashangaa mtoa mada sijui alikuwa amesinzia...! kama unakumbuka, bahada ya mh Ole Sendeka kutumia kanuni ya 117, Naibu spika Job ndugai aliwahoji na wabunge wakakubali, hoja ikapita.

Hata pale aliposimama mh Mkono kuomba utaratibu, naibu spika alimwambia "hoja ikishatolewa uamuzi haipaswi kuzungumzwa tena"
Au mheshimiwa Mkono amekutuma uje umsemee hapa JF kuwa yeye hakuunga mkono hoja?
 
Unalipwa malipo kiasi gani kuleta propaganda uchwara hapa JF?

bila kufuata sheria,kanuni na taratibu mtaendelea kuwaona mafisadi wakiwa wanapeta mitaani.tuache unafiki wa kujifanya tuna hasira na mafisadi wakati huo huo tunawaachia milango ya kutokea.ni lazima kuwa makini kwenye sheria na kanuni ili wasipate upenyo wa kutokea
 
Wakuu ya kuunga mkono sijui ila hili la Bunge kuchunguza hata mimi nina mashaka kiasi. Mashaka yangu ni kwamba inaaminika ama inasemwa kwamba wizara huwa zinakusanya pesa kwa ajili ya kupitisha budget na huwa hizo pesa wanapewa wabunge (kwa kifupi wanahongwa). Na imesemwa kwamba Jairo alikusanya pesa kwa ajili ya kuwapa wabunge ili wapitishwe budhet ya Wizara yake. Imesemwa pia kwamba hii ni kawaida wizara hufanya hizvyo!! Sasa kama wanufaika wakubwa wa michango hii ni Ndg. Wabunge inakuwaje wao ndio wafanye uchunguzi huu? Tunategemea wajivue nguo kwa kusema kwamba kweli Wizara huwa zinakusanya pesa na kuwapa wabunge ili wapitishe budget zao? Hapa kuna tatizo tena tatizo kubwa la conflict of interest.
 
bila kufuata sheria,kanuni na taratibu mtaendelea kuwaona mafisadi wakiwa wanapeta mitaani.tuache unafiki wa kujifanya tuna hasira na mafisadi wakati huo huo tunawaachia milango ya kutokea.ni lazima kuwa makini kwenye sheria na kanuni ili wasipate upenyo wa kutokea

Mkuu umenena vyema. Jazba zinatupeleka pabaya tunashindwa kuziba mianya ya kisheria na kikanuni kesho unakuta mtu anatakaswa kwa upenyo mdogo tu!!
 
  • user-online.png
    Danyel


    Today 15:43

    #11

    Junior Member
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_pos.png
    reputation_highpos.png
    reputation_highpos.png
    reputation_highpos.png



    Join Date : 2nd September 2011

    Posts : 4

    Rep Power : 0




  • https://www.jamiiforums.com/members/kimbunga.html


  • https://www.jamiiforums.com/members/njowepo.html

 
Nashangaa mtoa mada sijui alikuwa amesinzia...! kama unakumbuka, bahada ya mh Ole Sendeka kutumia kanuni ya 117, Naibu spika Job ndugai aliwahoji na wabunge wakakubali, hoja ikapita. Hata pale aliposimama mh Mkono kuomba utaratibu, naibu spika alimwambia "hoja ikishatolewa uamuzi haipaswi kuzungumzwa tena" Au mheshimiwa Mkono amekutuma uje umsemee hapa JF kuwa yeye hakuunga mkono hoja?
sijakurupuka! tofautisha hoja kuungwa mkono na kuafikiwa.hoja inaungwa mkono kwa wabunge wasiopungua 10 kusimama ila ili iafikiwe na kuridhiwa na bubge ni lazima wabunge wahojiwe.naibu spika hakuwahoji!!! pengine Mh Mkono alitaka kuweka mambo ya kikanuni sawa lakini jazba za wabunge na Mh Naibu Spika zimeishia kukiukwa kwa kanuni.kaangalie record ya video au kasome hansadi! ili ulione kosa hilo,ndiyo maana nasema ama alipitiwa au ni usanii!
 
Kumbukumbu za bunge zinaonesha kuwa hoja ya Mh Sendeka kuhusu kuundwa kwa kamati teule ya bunge kuchunguza sakata la Jairo iliungwa mkono baada ya kutolewa lakini haikuafikiwa kwa mujibu wa kanuni za bunge!

Licha ya Naibu Spika kurejea kuisoma kanuni kabla ya kuamua,hakuwahoji wabunge ili hoja iafikiwe au la, kama kanuni inavyotaka mara baada ya hoja kutolewa na kuungwa mkono.inawezekana alipitiwa kutokana na jazba au ni usanii,lakini vyovyote iwavyo kamati teule iliyoundwa si halali kwakuwa haikuridhiwa na bunge.kwa maana hiyo serikali inaweza ikaikataa repoti ya kamati hiyo endapo itagundua mapungufu yanayoidhalilisha.

Licha ya upungufu huo wa kikanuni vile vile kamati teule pia inakwenda kwenye uchunguzi ikiwa inajua aliyewatuma (bunge) anataka nini, hivyo basi kwa kuwa wao pia ni sehemu ya bunge watakuwa kama mshtaki,muendesha mashata na jaji.
Tafakari!!!!!!
Classical epitome of a stupid thinker!
I rest my case.
 
Jairo thing should now be given a rest and we need to move on other crucial matters for the betterment of our country. Its beyond me that over a bimester, folks' minds have engaged themselves into discussing this creature as if we have ran out of very serious matters.
ufisadi is a very crucial and serious matter to discuss,hata tuwe na mipango mizuri kiasi gani kama ina mianya ya ufisadi na mafisadi wapo tusitegemee kupata ma matokeo mazuri ya mipango yetu.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom