Sakata la Dr. Masau: Msimamo wa Serikali na Hatima ya Taasisi ya Moyo (THI)

zile links hazijajibu maswali ndio maana nikahitaji maelezo zidi

Unafikiri kwenye hizo habari nilizoweka wanazungumzia nini? Uliona mahala popote mtu analalamika? Uliona mahali popote kuna malumbano kati ya THI na Wizara? Kama hukuona basi hakuna jinsi ya kukusaidia kwenye hili.
 
Jamani bongo si mnaielewa?? NI top down approach! unaanzia kwa wakubwa juu!LOBBYING SKILLS!!! Masau anatuma barua Wizarani????Yeye yupo Dar ni kwa nini asiipeleke mkononi akahakikisha Mh Waziri analielewa ombi lake na ana nakala?Na apewe appointment nyingine ya kufuatilia? Kazi ibakie ya utekelezaji??BONGO MNAIJUA LAKINI? SI AJABU HATA BARUA YENYEWE HAIJAFUNGULIWA
He needs to play it cool and smart! Sasa kuweka listi ya mabingwa wa kizungu itasaidia nini? NGO smart zinaweka mpaka audited report YA KILA MWAKA!He has to show how many people have benefitted so far etc. Jinsi gani anavyozitumia hizo donations. CREDIBILITY jamani.

Mimi sina wasiwasi na ubingwa wake ....ila usimamizi wa hiyo taasisi?????mmmh ..

Tunaoweza kumsaidia hata mawazo tumsaidie jamani!!!!
 
Unajua unapoanzisha kitu kama hiki ni muhimu ukawa na watu "credible" kusaidia taasisi. Kwa mfano uliiona safu ya board of directors ya Haki Elimu? Did u see how they dealt with the goverment?
Sasa Bodi ya THI imefanya nini?Imesaidiaje katika hili. Zaidi sana tunachokiona ni Dr Masau analumbana na Wizara ya Afya kwa kutumia vyombo vya habari etc...lobbying skills zinahitajika hapa.....Sasa huyo dada anasaidiaje hapa...? Si ndio anayefanya admin ya THI....watu wanakopwa mishahara , ukabila , upendeleo etc.Nina contacts na watu kadhaa waliowahi kufanya kazi na taasisi hii wanasema it run like a "personal property"!Na wengi wameondoka

Unafikiri wanaompinga wanachukuliaje hili? Ukiamua kupambana usiachie loopholes kama hizi.Isitoshe kuna tetesi kuwa success rate ya operesheni zake ni ndogo(sina data!)
I am a big suppoter of Dr Masau lakini asafishe nyumba yake kwanza.Mimi nafikiri inawezekana kabisa watanzania kuchangia hili annually ....Hapo anapojaribu kupagusa pa eti badala ya India wagonjwa waje kwake.....ni pagumu....(Rupia zimeshatembea).

Atafute njia nyingine ya ku raise funds to prove skeptics his skeptics wrong .
Kwa kweli wewe unamjua hasa Dr Masau kwani yote unayoyasema ni ya kweli kuna wafanyakazi hata mshahara hawalipi.Kuna kipindi serikali ilimuidhinishia documents fulani ambazo taasisi moja ya nje ilitaka imsaidie Fedha Lakini ilibidi serikali kupitia wizara ya afya iidhinishe aliidhinishiwa na kama kumbukumbu zangu ni nzuri alipewa Dola 350,000 ili awasaidie watanzania kuwapatia matibabu hayo ya moyo,Je anaweza kuwaeleza Umma wa Watanzania alizitumiaje hizo fedha?Na kama kuna watanzania waliofaidika na hizo fedha ikiwemo kupatiwa matibabu bure kwenye hiyo taasisi ni wangapi na awainishe hadharani?Kuna matembezi ya mshikamano yaliyofanywa na taasisi yake na kupatikana kiasi cha fedha za kitanzania milioni 169 je hizi nazo alizitumiaje au watanzania ambao ni wagonjwa walifaidika vipi na fedha hiyo?Hivi kama ameshindwa kutoa mchanganyuo wa fedha ya kwanza ambayo wizara ilimsainia ili taasisi fulani ulaya impe kwanini atake tena wizara ifanye kitu kile kile bila ya kutoa mchanganuo wa awali?
Hivi lengo kuu la kuanzishwa THI ilikuwa ni nini?Ninavyoelewa wakati anaomba msaada wa kuanzisha hiyo taasisi lengo lilikuwa kuwasaidia watanzania ambao ni masikini na ndiyo maana kila kitu alipewa bure sasa kwanini yeye anawalipisha watanzania tena siyo kuchangia gharama bali gharama ni kubwa yaani million tano wakati India ni Karibu nusu ya hiyo kuanzia nauli hadi matibabu,sasa kwanini hili asilione kuwa ni tatizo na akarekebisha kama ameamua taasisi kuendesha kibiashara basi afanye biashara bila ya kumtegemea mtu au serikali na kama taasisi ni kusaidia basi asaidie halafu serikali nayo ichangie kwani tunaona serikali inasaidia hata hospitali za misheni kwenye sehemu ambazo Hakuna Hospitali za wilaya na zinaitwa Designated Hospital.Nitaendelea baadae kwasasa inatosha!
 
Halafu hiyo title ya Serikali imemwangusha???
Kwani alikuwa na mkataba gani nao???? All I can say about THI ni kulalamika kila siku na Dr Masau anajua kulalama na vyombo vya habari
Kwanza alianza "kulia vyombo vinaozea bandarini....akapewa tax exemption....
Sasa analilia ruzuku...KWANI ALIAHIDIWA NINI NA HIYO SERIKALI?ILIYOMWANGUSHA?Ku complain tuuuuu! AGANGAMAE! Hata kama ni kwenda kumwona JK akamwone sio kuchanganya siasa na profession.
Mimi sijawahi kumwona huyo Masau hata siku moja akajieleza kwa ufasaha, kinagaubaga anachokifanya, na anachohitaji asaidiwe. Mbona MEWATA wamefanikiwa?
Halafu he is there alone? Is he the only doctor. Hataki kushirikiana na wenzake ndio maana wana mfix!
 
sasa hizi hoja nzuri... nani anayeweza kunipa habari za upande wa pili wa suala hili? Natarajia kuzungumza na Dr. Masau Jumamosi.. na nitambana kwa haya maswali..
 
Sasa allifanya nini na hizo USD 350,000 au anatumia umaskini wa watanzania kujinufaisha??????Wana JF kabla hatu deal na jambo we need to scrutinize the issue throughly.....Mnaona issue inavyobadilika hapa??????????????
 
Na umwambie aache kulalamika......afanye vitu vyake....Na asichangaye profession na politics....sasa Salma Kikwete amemsaidiaje?
Ni kwani asimkaribishe Mh Waziri au naibu wake tena ana bahati ni mtaaluma wa Afya....awaeleze mafanikio yake na matatizo yake.
Yeye anataka ku misuse "mob sympathy" na kuichanganya na "kuwajibika".
Na hayo mafanikio yake aweke kwenye website plus the audited reports! Zote. Website yenyewe iko tu....ki laiser faire....na ashirikiane na wataalam wenzake. Tunajua ana utaalam sana ila awe pamoja na wenzake hata kama watampa moral support tu.
He has poor admin skills he cannot be the doctor and the funds administrator at the same time. Aangalie a good way of strenghtening institute HR!Mpe pongezi sana kwa kazi nzuri!
 
Kuna kipindi aliomba msaada ubalozi wa Japan wa Usafiri kwa ajili ya kubebea wagonjwa na Ubalozi wa Japan ukampatia gari la wagonjwa sasa muulize na hilo watanzania wanafaidikaje na hii misaada anayoomba kwa migongo yao kwamba anataka kuwasaidia halafu akipewa anataka kuwauzia Huduma?
Hapa anaenda kinyume na dhamira kuu ya uanzishwaji wa hiyo Taasisi lengo lilikuwa nzuri kabisa Lakini utekelezaji umeingia dosari.Hiyo Taasisi imeandikishwa Tanzania na Marekani na Nchi zote mbili ina msamaha wa kodi,sasa kwanini anauza Huduma kwa bei ghali sana?Kule vifaa vyote amepewa bure na kama kuna sehemu alitakiwa kulipia tax alisamehewa Na bado kuna taasisi ambazo zipo tayari kumsaidia kifedha ikiwemo ile ya Ujerumani Ila kwa sharti la serikali kushirikishwa na serikali ilishawahi kufanya hivyo mara moja ili kufanikisha hizo funds kupatiwa Dr Masau lakini haelezi amezifanyia nini?Sasa kama hadi leo hajaeleza bayana amezifanyia nini au ni kwanini anawatoza wananchi fedha za matibabu wakati lengo la taasisi ni kutoa msaada kwa walalahoi?Sipendezwi serikali inavyopeleka wagonjwa India na kumuacha mzawa akifukuzia tender lakini mzawa huyu inabidi aamue moja aidha kufanya biashara au kutoa msaada kama dhumuni la uanzishwaji wa taasisi hiyo ulivyolenga.Na kama ni biashara abwereshe mazingira yake kuanzia safu ya utaalamu na gharama Na kama ni kutoa msaada basi afanye hivyo angalau kwa wazawa kuchangia huduma kwa mwenye kuweza na Bure kwa wasioweza kwani misaada inayombwa inaombwa kwa mgongo wa walalahoi.
 
KNKCU, si hayo mnayomwaga hapa. Inabidi Moderator aongeze "alama ya kuuliza" kwenye heading ya hii post maana ilivyo sasa inaonekana kama kauli ya uhakika.
 
Haha,

Pole Mzee Mwanakijiji, fine am doing the 4 u. Anyway, hata mimi nilidhani ulikuwa unamaanisha kweli hivyo nikabakia kusoma tuuuu!

Carry on, it's changed now!
 
THIentry.jpg

jengo jipya la taasisi ya moyo Tanzania
Is this the recent hospital? Au hii ndio ile ya Mikocheni???
 
Mzee Mwanakijiji

Kwa vile inaonekana kuna ugumu fulani wa kusoma kilichoandikwa (labda sababu ya wingi wa maandishi na kutokupangiliwa vizuri) nimerudi kwenye ukurasa wa kwanza na kuhighlite ni nini kinazungumziwa. Natumaini itawasaidia. Vinginevyo sina jinsi nyingine.
KNKCU, si hayo mnayomwaga hapa. Inabidi Moderator aongeze "alama ya kuuliza" kwenye heading ya hii post maana ilivyo sasa inaonekana kama kauli ya uhakika.

Ndio sababu mimi nimeshindwa kuchangia hapa maana source zangu hazikuweza kujibu upesi. Ilianza na Prof. Ikaenda kuwa Dr. what next...............Udaku?
 
sasa hizi hoja nzuri... nani anayeweza kunipa habari za upande wa pili wa suala hili? Natarajia kuzungumza na Dr. Masau Jumamosi.. na nitambana kwa haya maswali..

Upande wa pili gani si ndio huo???? majibu ya Mh naibu yanaelezea upande wa gov...au unataka info gani tena?
 
Majibu ya Mhe. Naibu hayahusiani na madai ya sasa ya Dr. Masau. Nilitaka kupata mtu ambaye anaujuzi wa mambo ya THI ambaye anaweza kuzungumza bila kuogopa na hivyo kuweza kubalance nitachozungumza na Dr. Masau. Hivi sasa ni maneno yenu wewe na KNKCU na sijui yana ukweli kiasi gani maana sijaona madai mnayoyatoa mahala popote kwenye maandishi. Hakuna mfanyakazi aliyejitokeza hadharani na kusema Dr. Masau hawalipi mshahara, na hakuna mahali ambapo wizara imesema hapo THI pana daktari mmoja tu? Wala madai ya ukabila sijaona mahala popote isipokuwa kwenye maneno yako. Hivyo, ningepata mtu ambaye anajua kwa hakika kinachoendelea. Hata taswira anayoiacha KNKCU kuhusu uwezekano wa kuwepo kwa matumizi mabaya ya fedha kitu ambacho hata kwenye maandishi yako unaashiria, sijawahi kuona hata kiongozi au wizara ikiulizia.

Madai ya wizara yamehusiana na vifaa na uwezo wa taasisi hiyo zaidi kuliko nani anatoa huduma hiyo. Kama serikali ingekuwa na mashaka juu ya nafsi ya Dr. Masau bila ya shaka wangesema hivyo. Na kama wangetaka ripoti ya matumizi ya fedha ya taasisi hiyo bila ya shaka wangepewa. Tatizo liko wapi? Hapa ndipo ninapotaka upande wa pili!
 
Back
Top Bottom