Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
na Mwandishi wetu
MKUU wa Wilaya ya Masasi, Nape Nnauye, amewashauri Watanzania kuacha itikadi za vyama, kuungana kwa pamoja na kuandamana ili kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro (ICC) dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ya kuilipa kampuni ya Dowans sh bilioni 185.
Nnauye alitoa ushauri huo jana kupitia mtandao wa face book ambapo alionyeshwa kukerwa na hukumu hiyo iliyotolewa hivi karibuni na mahakama hiyo.
Hivi kwa nini Watanzania wasiungane kwa pamoja hata kama ni kwa maandamano kupinga hukumu ya kuwalipa Dowans 185 bilioni , bila kujali itikadi zetu, tulinde pesa za kodi zetu, alisema Nape kwa njia ya mtandao.
Hukumu hiyo iliyotolewa Novemba 15 mwaka huu, imezua mjadala mkubwa nchini huku baadhi ya wananchi wakisema hali hiyo imesababishwa na viongozi wazembe na wasio na uchungu na nchi.
Katika hukumu hiyo, TANESCO iliamriwa na ICC kuilipa Dowans fidia ya sh bilioni 185 kutokana na kuvunja mkataba wake wa kuzalisha umeme bila ya kufuata taratibu.
Shirika hilo lilitangaza kuvunja mkataba wa Dowans Agosti mosi, 2008 ikiwa ni mwaka mmoja kabla ya mkataba huo kumalizika.
Awali, serikali kupitia TANESCO mwaka 2006 iliingia mkataba uliodaiwa kuwa na harufu ya rushwa kwa ajili ya kuzalisha megawati 100 za umeme na kampuni ya Richmond Development LLC ili kuiokoa nchi na giza kwa kukosa umeme kulikotokana na ukame.
Mjadala wa mitambo ya Dowans, uliwahi kuligawa taifa kwa kipindi kirefu mwaka 2008 baada ya Kamati Teule ya Bunge chini ya Uenyekiti wa Dk. Harrison Mwakyembe, kutoa taarifa ya kuchunguza uhalali wa kampuni ya Richmond na mkataba baina yake na serikali.
Kutokana na taarifa iliyowasilishwa bungeni Februari mwaka 2008 aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alijiuzulu ikiwa ni ishara ya kuwajibika kama kiongozi mkuu wa ofisi yake iliyodaiwa kushiriki katika kuiwezesha Richmond kushinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.
Wakati wa mjadala huo, aliyekuwa Mkurugenzi wa TANESCO, Dk. Idris Rashid, aliishauri serikali kuinunua mitambo hiyo jambo lililoungwa mkono na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Kabwe Zitto (CHADEMA), huku akipingwa vikali na wenzake ndani na nje ya chama chake.
Hata hivyo, Bunge lilikataa kupitisha pendekezo la ununuzi wa mitambo ya Dowans likisema kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004 inayokataza serikali au taasisi zake kununua mitumba.
Uamuzi huo wa ICC ulitolewa na jopo la majaji watatu chini ya uenyekiti Gerald Aksen na wasuluhihi Swithin Unyantwali na Jonathan Parker.
Jopo hilo liliamuru TANESCO ilipe fidia ya zaidi ya sh bilioni 36 na riba ya asilimia 7.5 kwa mwaka inayofikia kiasi cha zaidi ya sh bilioni 26 tangu Juni 15 mwaka huu, hadi fidia hiyo itakapolipwa.
Kadhalika, jopo hilo liliamuru malipo ya sh bilioni 60 na riba ya asilimia 7.5 ambayo ni sawa na sh bilioni 55 kuanzia Juni 15, 2010 hadi wakati wa malipo.
Katika uamuzi huo, jopo hilo lilisisitiza kuwa ada na gharama za wasuluhishi wa ICC na utawala ni sh bilioni moja zinatakiwa kulipwa na pande zote.
MKUU wa Wilaya ya Masasi, Nape Nnauye, amewashauri Watanzania kuacha itikadi za vyama, kuungana kwa pamoja na kuandamana ili kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Usuluhishi wa Migogoro (ICC) dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) ya kuilipa kampuni ya Dowans sh bilioni 185.
Nnauye alitoa ushauri huo jana kupitia mtandao wa face book ambapo alionyeshwa kukerwa na hukumu hiyo iliyotolewa hivi karibuni na mahakama hiyo.
Hivi kwa nini Watanzania wasiungane kwa pamoja hata kama ni kwa maandamano kupinga hukumu ya kuwalipa Dowans 185 bilioni , bila kujali itikadi zetu, tulinde pesa za kodi zetu, alisema Nape kwa njia ya mtandao.
Hukumu hiyo iliyotolewa Novemba 15 mwaka huu, imezua mjadala mkubwa nchini huku baadhi ya wananchi wakisema hali hiyo imesababishwa na viongozi wazembe na wasio na uchungu na nchi.
Katika hukumu hiyo, TANESCO iliamriwa na ICC kuilipa Dowans fidia ya sh bilioni 185 kutokana na kuvunja mkataba wake wa kuzalisha umeme bila ya kufuata taratibu.
Shirika hilo lilitangaza kuvunja mkataba wa Dowans Agosti mosi, 2008 ikiwa ni mwaka mmoja kabla ya mkataba huo kumalizika.
Awali, serikali kupitia TANESCO mwaka 2006 iliingia mkataba uliodaiwa kuwa na harufu ya rushwa kwa ajili ya kuzalisha megawati 100 za umeme na kampuni ya Richmond Development LLC ili kuiokoa nchi na giza kwa kukosa umeme kulikotokana na ukame.
Mjadala wa mitambo ya Dowans, uliwahi kuligawa taifa kwa kipindi kirefu mwaka 2008 baada ya Kamati Teule ya Bunge chini ya Uenyekiti wa Dk. Harrison Mwakyembe, kutoa taarifa ya kuchunguza uhalali wa kampuni ya Richmond na mkataba baina yake na serikali.
Kutokana na taarifa iliyowasilishwa bungeni Februari mwaka 2008 aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alijiuzulu ikiwa ni ishara ya kuwajibika kama kiongozi mkuu wa ofisi yake iliyodaiwa kushiriki katika kuiwezesha Richmond kushinda zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura.
Wakati wa mjadala huo, aliyekuwa Mkurugenzi wa TANESCO, Dk. Idris Rashid, aliishauri serikali kuinunua mitambo hiyo jambo lililoungwa mkono na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Kabwe Zitto (CHADEMA), huku akipingwa vikali na wenzake ndani na nje ya chama chake.
Hata hivyo, Bunge lilikataa kupitisha pendekezo la ununuzi wa mitambo ya Dowans likisema kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004 inayokataza serikali au taasisi zake kununua mitumba.
Uamuzi huo wa ICC ulitolewa na jopo la majaji watatu chini ya uenyekiti Gerald Aksen na wasuluhihi Swithin Unyantwali na Jonathan Parker.
Jopo hilo liliamuru TANESCO ilipe fidia ya zaidi ya sh bilioni 36 na riba ya asilimia 7.5 kwa mwaka inayofikia kiasi cha zaidi ya sh bilioni 26 tangu Juni 15 mwaka huu, hadi fidia hiyo itakapolipwa.
Kadhalika, jopo hilo liliamuru malipo ya sh bilioni 60 na riba ya asilimia 7.5 ambayo ni sawa na sh bilioni 55 kuanzia Juni 15, 2010 hadi wakati wa malipo.
Katika uamuzi huo, jopo hilo lilisisitiza kuwa ada na gharama za wasuluhishi wa ICC na utawala ni sh bilioni moja zinatakiwa kulipwa na pande zote.