Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Jeshi la Polisi liko matatani. Polisi wetu wanawaona wananchi kama maadui zao kiasi kwamba hakuna ile heshima ya polisi kwa raia. Tumeyaona Nyamongo, tumeona Songea na sasa yametokea tena Mwanza. Na hatujasahau yaliyotokea Arusha mwaka mmoja uliopita. Kuna dharau ya aina fulani ambayo inaendana na ubabe wa polisi. Kwa mfano, majibu ya polisi kwenye matukio ya Arusha, Songea na Mwanza yamejadaa dharau (contempt) ya wananchi.
Lakini baya zaidi ni kuwa hakuna mfumo mzuri wa kushughulikia polisi wanapofanya au kutuhumiwa kufanya mambo mabaya ambayo mengine yanapakana na uhalifu. Kwa muda wote huu wa Said Mwema na Mkuu wa "Operesheni na Mafunzo" Bw. Chagonja kumekuwepo matukio mengi sana ya uvunjaji wa haki za raia, matumizi makubwa ya nguvu dhidi ya raia wasio na silaha na kukosekana kwa umakini katika kushughulikia maandamano au mikusanyiko mikubwa ya watu.
Kwa kadiri tumeendelea kuwaachilia hawa watu kwa vile wao ni "polisi" ndivyo wanavyozidi kusimamia jeshi with impunity. Hivi ndivyo lilivyokuwa jeshi la Polisi la Hosni Mubarak. Lilikuwa jeshi ambalo lilikuwa linaweza kufanya lolote, kwa yeyote na bila kuulizwa. Leo hii wabunge wawili wamepigwa mapanga "mbele ya polisi" kama walivyodai wenyewe na polisi hawashtuki? Yaani, polisi wale wale wanaotuhumiwa kusimamia kupigwa kwa wabunge wa JMT ndio wameachwa kujichunguza wenyewe? Halafu hao hao wanasema ndio wanataka waje kuwahoji wabunge wanaowatuhumu na Makao Makuu ya POlisi imeshindwa kutoa tamko hata la kuonesha uzito? Ni dharau gani hii kina Mwema na Chagonja wanayo?
Kamati ya Bunge ya Usalama chini ya Lowassa - anayesremwa kuwa ni kiongozi mwenye nguvu- iko wapi? Hatujawahi kuisikia hata mara moja kuwaita viongozi wa polisi kuwahoji juu ya mambo haya na sasa wabunge wa CDM wamepigwa na Lowassa (Mwenyekiti) hajaonesha hata uongozi wa kutaka kuwatembelea hawa wabunge au kwenda Mwanza au hata kujaribu kuonana na wakuu wa jeshi? Au anafikiria ni usalama wa vitu gani ambao kamati yake inausimamia?
Viongozi wa CDM niliwahi kuwaambia kuwa wanavyoendelea kulilea jeshi la polisi na kulilalamikia tu ndivyo linavyozidi kuthubutu kuwa wakali (it becomes more hostile) kwa viongozi wa upinzani. Binafsi naamini wakati umefika wa viongozi wa CDM kuitisha maandamano makubwa tu ya kupinga ubovu na uzembe wa Jeshi la POlisi kwani hadi hivi sasa ni wao CDM ndio wanakiona cha moto dhidi ya mkono wa askari wa Mwema.
Jeshi hili ni la raia (civilian police force) na hivyo nilazime lilazimishwe kujifunza kuheshimu na kujali raia. Siyo polisi wanapoenda kwenye nyumba ya mtu wanaanza kuvunja na kuingia kwa nguvu wakati hawana waranti ya kufanya upekuzi au wanatumia silaha za moto dhidi ya raia wasio na silaha yoyote.
Nani atathubutu kusema kuwa Mwema na Chagonja waondolewe?
Lakini baya zaidi ni kuwa hakuna mfumo mzuri wa kushughulikia polisi wanapofanya au kutuhumiwa kufanya mambo mabaya ambayo mengine yanapakana na uhalifu. Kwa muda wote huu wa Said Mwema na Mkuu wa "Operesheni na Mafunzo" Bw. Chagonja kumekuwepo matukio mengi sana ya uvunjaji wa haki za raia, matumizi makubwa ya nguvu dhidi ya raia wasio na silaha na kukosekana kwa umakini katika kushughulikia maandamano au mikusanyiko mikubwa ya watu.
Kwa kadiri tumeendelea kuwaachilia hawa watu kwa vile wao ni "polisi" ndivyo wanavyozidi kusimamia jeshi with impunity. Hivi ndivyo lilivyokuwa jeshi la Polisi la Hosni Mubarak. Lilikuwa jeshi ambalo lilikuwa linaweza kufanya lolote, kwa yeyote na bila kuulizwa. Leo hii wabunge wawili wamepigwa mapanga "mbele ya polisi" kama walivyodai wenyewe na polisi hawashtuki? Yaani, polisi wale wale wanaotuhumiwa kusimamia kupigwa kwa wabunge wa JMT ndio wameachwa kujichunguza wenyewe? Halafu hao hao wanasema ndio wanataka waje kuwahoji wabunge wanaowatuhumu na Makao Makuu ya POlisi imeshindwa kutoa tamko hata la kuonesha uzito? Ni dharau gani hii kina Mwema na Chagonja wanayo?
Kamati ya Bunge ya Usalama chini ya Lowassa - anayesremwa kuwa ni kiongozi mwenye nguvu- iko wapi? Hatujawahi kuisikia hata mara moja kuwaita viongozi wa polisi kuwahoji juu ya mambo haya na sasa wabunge wa CDM wamepigwa na Lowassa (Mwenyekiti) hajaonesha hata uongozi wa kutaka kuwatembelea hawa wabunge au kwenda Mwanza au hata kujaribu kuonana na wakuu wa jeshi? Au anafikiria ni usalama wa vitu gani ambao kamati yake inausimamia?
Viongozi wa CDM niliwahi kuwaambia kuwa wanavyoendelea kulilea jeshi la polisi na kulilalamikia tu ndivyo linavyozidi kuthubutu kuwa wakali (it becomes more hostile) kwa viongozi wa upinzani. Binafsi naamini wakati umefika wa viongozi wa CDM kuitisha maandamano makubwa tu ya kupinga ubovu na uzembe wa Jeshi la POlisi kwani hadi hivi sasa ni wao CDM ndio wanakiona cha moto dhidi ya mkono wa askari wa Mwema.
Jeshi hili ni la raia (civilian police force) na hivyo nilazime lilazimishwe kujifunza kuheshimu na kujali raia. Siyo polisi wanapoenda kwenye nyumba ya mtu wanaanza kuvunja na kuingia kwa nguvu wakati hawana waranti ya kufanya upekuzi au wanatumia silaha za moto dhidi ya raia wasio na silaha yoyote.
Nani atathubutu kusema kuwa Mwema na Chagonja waondolewe?