Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambae pia ni kaimu Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Said Meck Sadick sijui yupo kwa maslahi ya nani. Tuna nina wasiwasi viongozi wanaopelekwa mikoa mingine ambao si wazawa wa eneo husika wanakua na agenda za makusudi wa kuwadumaza wenyeji. Au huenda uwezo wao kiutendaji umekua mdogo na kuwa mzigo kwenye siasa zenye ushindani zinazoendelea. Uwezo wa kiutendaji wa mkuu huyu umeonekana kuwa mdogo hata wakati wa suala ya mabomu ya gongolamboto alivyolishughulikia. Mkuu huyu amewalazimisha wakulima wa ufuta mkoani Lindi kuuza mazao yao kwa bei ya shs 1,000/-kupitia mfumo wa stakabadhi badala ya shs1,200/- – 1,500/- kwa kilo, ni kwa maslahi ya nani? Ni kwa Maendeleo ya wakulima? auya kwake? Mkuu huyu wa mkoa alituma askari wakiwa na silaha na risasi za moto kwa ajili kuwalazimisha wakulima wasiuze kwa bei hiyo na atakaekaidi ametishia atauwawa. Wakulima hawa kipindi cha kilimo walikwenda serikalini kuomba msaada wa askari waje kuuwa wanyama waharibifu walioharibu mazao kama ufuta na serikali ilisema haina risasi ya kuwaulia. Sasa iweje wakati wa kuuza mazao yao yaliyobaki serikali inawafata wakiwa na risasi za moto kwa ajili ya kumuua mtu yeyote atakae kaidi amri ya huyu mkuu wa mkoa. Mkuu huyu ambae ni mwenyekiti wa Kamati ya ushauri ya maendeleo ya mkoa wa Lindi imelikataa pendekezo la wabunge la kutaka zao la ufuta liondolewe katika utaratibu wa kuuzwa kwa mfumo wa stakabadhi ya mazao ghalani kwa kuwa unawanyonya na badala yake wauze kwa wafanya biashara. Mapendelekezo hayo yamekataliwa kwa kuwa tu wabunge ni wa chama cha upinzani CUF.Mimi nikiwa mpenda maendeleo nadhani Mkuu huyu ni mzigo kwa CCM na anawalizimisha watu kuwa masikini.