Qwy
JF-Expert Member
- Nov 23, 2018
- 6,238
- 31,148
Kwakuwa hatujawa na sheria ya time limit kwenye contracts basi hukuna jinsi bali ni kukubaliana na mambo yalivyo mpaka sheria zitakapobadilishwa.Ulilosema ni sawa, lakini si unaona kuwa tatizo linaanzia hapo? Hiyo mikataba ya muda mrefu inatakiwa ipigwe marufuku. Mtoto wa miaka kumi na nane anapotaka kujaribu kujaribu usanii wa muziki eti anapewa mkataba wa miaka kumi, na kwa vile yuko desparate, anakubali tu, je ikitokea kuwa baada ya miaka mitatu anataka abadili uelekeo labda aingie kwenye siasa au biashara nyingine utamzuia? Kumbuka hawa vijana bado wana opportunities nyingi sana za kujaribu maishani. Mikataba hiyo ya miaka kumi ni kama kifungo cha maendeleo yao. Kuwe na limita ya umri wa mkataba, labda miaka mitatu mitatu renewable. Huwezi kusikia mchezaji wa mpira kapewa mkataba wa miaka kumi, nilizoma mikataba hiyo ya miaka kumi kwa wasanii wa Tanzania tu.
Rejea issue ya Harmonise maelezo ya Fela ni kuwa mkataba haumfungi,yuko huru kutoka wakati wowote anaotaka ila ombi lake ni kuwa aage kiustaarabu ili kusiwepo mazingira ya beef baina yake na WCB lakini nionavyo kama ni kweli ametoka itakuwa ni faida kwake akitengeneza beef.
Beef itamsaidia kwani haters wa Diamond na haters wa WCB automatically watageuka fans wa Harmonise, ila ikitokea hiyo Kiba ndiyo atakuwa amepotea jumla.