Safari za Treni ya Mwendokasi kuanza Agosti mwaka huu, 2021

Status
Not open for further replies.

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,087
6,567
Hayo yamesemwa na Waziri wa ujenzi na uchukuzi Leonard Chamriho. Ameyasema haya baada ya kamati ya kudumu ya bunge ya miundo mbinu kutembelea na kukagua ujenzi wa mradi wa Sgr kipande cha Dodoma mpaka Dar es salaam.

Hivyo amesema kuwa safari za Dar mpaka Morogoro zitaanza mwezi Agost baada ya mabehewa kuwasili mwezi Juni mwaka huu.

Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge wameridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo. Na wanaona umaenda sawa.

Mbali na haya ikumbukwe mradi huu ulitarajiwa kuanza mwezi Aprili mwaka huu na ahadi ya kuanza safari za Dar es Salaam kwenda Morogoro alizitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea huu mradi mwaka jana.

Kipande cha Dar- Moro kilitarajiwa kuanza safari zake Novemba 2019 lakini mpaka hii leo mwaka 2021 hakuna dalili zozote kuanza.

====

KANUSHO:

=====

Thread 'Kanusho la taarifa ya kuanza kwa huduma za safari za treni za kisasa Dar es Salaam - Morogoro' Kanusho la taarifa ya kuanza kwa huduma za safari za treni za kisasa Dar es Salaam - Morogoro
 
Jamani mbona mnatuchanganya?. Mtu wangu wa karibu kitengo kanidokeza nisisumbuke na kuangaika na uvumi unaoendelea mtandaoni TISS wameamua kucheza na akili za watu kupotezea ishu ya mahindi kukataliwa Kenya.

Kigogo na Chahali ole wenu Jiwe azinduke
Big NO. Hayo mahindi yalikuwa na impact gani mpaka ufanyike ujinga kama huu? NO. Huyo mtu labda anafanya kitengo cha wauza chips
 
Natamani sana kuishuhudia hiyo siku ya uzinduzi! Maana bado sijasahau zile shamra shamra za kupokea bombardier na dreamliner.
 
Hayo yamesemwa na Waziri wa ujenzi na uchukuzi Leonard Chamriho. Ameyasema haya baada ya kamati ya kudumu ya bunge ya miundo mbinu kutembelea na kukagua ujenzi wa mradi wa Sgr kipande cha Dodoma mpaka Dar es salaam...
Wa Kuizindua yupo au atakuwepo muda huo kwa mujibu wa Majaliwa yake Israeli?
 
Uzunduzi wa mwendokasi nilizunguka rerminal zote tena bure siku nzima.

Mungu aniweke hai uzinduzi wa SGR nipige root za dar moro dar moro huku nikinywaaa pepsiiii baridiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii buuuuuureeeeeeeeeeeee
 
Treni ndiyo usafiri wa uhakika
Sgr itaokoa sana muda
Safi sana

Ova
Ndugai aka Ebola anasema SGR ni Sawa na kufunga tera la ng'ombe mbele ya ng'ombe badala ya kulifunga nyumba! (kweli watanzania ni wapole Sana, nchi nyingine leo bungeni pasingekalika kwa maandamano)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom