Safari za mabasi: Tuelimishane maandalizi muhimu kabla ya safari ndefu

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,028
Toilet paper - Siwezi kujisafisha na yale maji ya vyoo vya kuchimbia dawa.

Vidonge vya Fragyly (endapo tumbo likizingua) na panadol (kichwa kikiuma)

Sinunuagi chakula njiani, huwa kinapkwa asubuhi nakiweka kwenye hotpot

Maombi, haya ni muhimu kabla na baada ya safari.

Kuchaji simu / power bank kwa ajili ya mawasiliano ya uhakika.

Begi lenye nguo na vituvingine navyoweza kununua upya hata vikipotea naliweka kule chini ya bus, kuna kabegi kengine huwa nawekea laptop, pesa, nyaraka, leseni, vyeti, n.k hili huwa nalichunga mwenyewe ndani ya basi.

Vizawadi zawadi, endapo ntafikia kwa ndugu rafiki au jamaa, Ni nani asiependa zawadi, Napenda kununu kitu ambacho napoishi ni bei rahisi ila nakoenda ni ghali ama ni adimu.
 
Sasa kama Hununui chakula njiani flagilly za nini ? Duuh nawazia hilo hot pot lake unavyolipakatia na kulichunga njiani...
 
We mbona bado unaishi maisha ya enzi za Ujima sana, yani bado unasafiri umeweka chakula kwenye mabakuli, bado unaweka hela kwenye vibegi......acha mambo kizamani bana.

Kiume unatakiwa ile alfajiri unaamkia kwenye Basi uko mtungi wa hatari ukioneshwa siti yako tu unauchapa usingizi, ukija kuamka saa 8 hivi mchana mnakaribia kufika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye bus ununue kuku lako la kuchoma fresh kabisa na sijui kwanini hakukosekani wale wadada huambia mtoto nenda kwa uncle 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Back
Top Bottom