Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
WanaJF nimekuwa nikifuatilia mambo mbalimbali tangia ujio wa Babu wa Loliondo. Ufuatiliaji wangu umejikita zaidi juu ya watu wanaoenda kwa Babu. Ni jambo ambalo haliwezi kupingika kwamba makundi ya watu wanaoenda kwa Babu yanadhihirisha kwamba hamkani si shwari Tanzania; Watanzania karibu wote tu wagonjwa: Si Mawaziri, viongozi wa Serikali, Majaji, Wabunge, Madiwani, nk. Wote ni wagonjwa, si tumewaona ama kusikia kuwa wameenda kwa babu na kupata kikombe kinachoaminika kuponya magonjwa sugu yakiwemo UKIMWI, Kansa na Kisukari. Kuna wengine wanasema wamekunywa kwa sababu ya curiosity tu!!! Siamini kama ni curiosity kwa kuwa Babu alishasema kwamba dawa yake si kinga bali wainywe wagonjwa tu: Hii imenifanya niamini kwamba wanaoenda na kunywa kikombe basi wote ni WAGONJWA!
Suala langu hapa sasa ni kwamba kama sote tu wagonjwa, inakuwaje viongozi wenye mamlaka watumie rasilimali za serikali (Mashangingi na huenda Per diem) kwenda kunywa dawa ilihali wafanyakazi wengine wa serikali na wananchi wengine ambao si wafanyakazi wakihangaika ki vyao kujitafutia usafiri (FUSO hayaaa, Mabasi mikweche, hayaaa) kwa gharama zao kuelekea Loliondo? Kama serikali imeamini (Mimi siamini) kwamba ile ni tiba kama ilivyo ya Muhimbili na viongozi wake wanaenda kupata tiba hiyo kwa gharama za serikali, ni kwa nini isiandae utaratibu wa kiwafikisha wagonjwa huko kwa babu kwa gharama za serikali kama ambavyo viongozi wanaenda kwa gharama za serikali? TUTAFAKARI
Suala langu hapa sasa ni kwamba kama sote tu wagonjwa, inakuwaje viongozi wenye mamlaka watumie rasilimali za serikali (Mashangingi na huenda Per diem) kwenda kunywa dawa ilihali wafanyakazi wengine wa serikali na wananchi wengine ambao si wafanyakazi wakihangaika ki vyao kujitafutia usafiri (FUSO hayaaa, Mabasi mikweche, hayaaa) kwa gharama zao kuelekea Loliondo? Kama serikali imeamini (Mimi siamini) kwamba ile ni tiba kama ilivyo ya Muhimbili na viongozi wake wanaenda kupata tiba hiyo kwa gharama za serikali, ni kwa nini isiandae utaratibu wa kiwafikisha wagonjwa huko kwa babu kwa gharama za serikali kama ambavyo viongozi wanaenda kwa gharama za serikali? TUTAFAKARI