Safari yangu ya kumuona Maxence, nimejifunza mengi gerezani

Nilishasema Lumumba wengi wanafurahia sana hii hali.
Hapana huo ni uongo kabisa manake JF Ina vitu vingi sana vya maana ambavyo havina mringo WA upande wowote ila watu kama ndiye unayeharibu JF kwa kufanya kila kitu Ni cha kisiasa wakati so kweli.Kuliko uandike vitu vya uongo kama hivi Ni busara kukaa kimya.
 
Mkuu shukrani sana kwa mrejesho.
Asante pia kwa kutuwakirisha ningekuwepo nisingelikosa.
Inshallah bila shaka kesho atatoka na yatakwisha.
 
Habari wakuu, mie ni miongoni mwa tuliojaaliwa kumtembelea ndugu yetu Maxence Melo gereza la Keko. Nikiri sijawahi kufika gerezani ama kwa kushikwa ama kwenda kumtembelea mtu hivyo pamoja na kumuona Max nmejifunza hali ilivyo kwenye Magereza yetu japo sio kwa undani.

Nilifika wakanikagua na kisha nikaingia ndani, ukiingia na simu unaiacha kwa mlinzi ikiwa na ID. Ukifika unachukua namba na namba ilipofika nikaitwa ndani. Alietusindikiza akaishia mlangoni na ndani unasema jina. Nilichokiona pale chini watu wa magereza wanawajua sana watu wao na ni marafiki(Sijui watu wasipokuwepo).

Nilivyotaja jina, yule jamaa wa magereza akasema 'Huyu mtu kavunja rekodi leo' hivyo hongera kwetu sote tulioenda kisha akamuita mtu akanisindikiza juu na kuitiwa Maxence. Nilifika kwa Maxence nikamsalimu na kwa ujumla alikuwa na bashasha. Akasema anategemea kutoka lakini hata asipotoka kwa kuwa mambo yako sawa kwetu hata akilia sikukuu gerezani hewala.

Tukaongea mambo mawili matatu na miongoni mwa wachangiaji wa mawili matatu walikua watu wa magereza na nilienda na vitu kadhaa, akachukua kadhaa na vilivyobaki akasema nimpe jamaa aliempokea gerezani(Alikua sehemu ya chini) kwani yeye tayari ana vingi sana.

Wakati nasubiri kumuona Maxence nilipata nafasi ya kuongea na watu kadhaa ambao wameenda kuwaona na kuwapa chochote kitu ndugu zao, nilisikia hadithi kadhaa zilizopelekea watu kuwekwa ndani(Wote bado mahabusu). Najua ni stori za upande mmoja ila kuna watu wamekaa four good years bila hukumu, hebu fikiria kesi ikaisha halafu hana hatia!

Poleni kwa kuwachosha, ni mara yangu ya kwanza wakuu na nahisi washkaji wanaishi peace sana tofauti na tunavyosikia pia pongezi sana kwa askari wa magereza kama jinsi nilivyowaona leo ndio wako hivyo siku zote(Kuanzia mapokezi mpaka ndani).

NB: Gerezani sio kuzuri na anaenda yeyote, mahakama ziongezewe uwezo wa kusikiliza kesi ili wasiohusika waondoke, kumuweka mtu miaka minne bila hukumu kwangu ni zaidi ya hukumu kwani hasira ya mtu kunisingizia na kunisababishia maumivu naijua mwenyewe.

[HASHTAG]#Kesho[/HASHTAG] ntakuwa mahakamani
well analyzed story. highfive
 
Tumuombee asiwe na hatia ya aina yoyote, na ashinde kesi.

Nitafurahia sana kama atakuwa kaonewa na sio yeye ndiye mwenye kosa.

Japo mimi ni mwanachama wa CCM, lakini sipendi dhulma wala uchochezi. Kiongozi wangu akiwa amekosea sitamtetea lak8ni akiwa sawa nitasema.

Kwa hili sioni haki ya kutompa mdhamana, mtu anajulikana, ana mali na familia yake ipo hapa nchini.

Kuna wakati we are politically affiliated na kuna wakati we are nationalistic . Kwenye hili la Mello full justice has to be implemented, na kama hakupatikana na kosa lolote serekali imuombe msamaha.
 
Jela sio kubaya sana kama zamani, siku hizi ule ubabe wa kugeuzwa mke wa mtu umefanyiwa kazi.
Pia polisi wa pale wanakua fair, tatizo linakuja ukiwa jeuri. Na hilo la watu kukaa kitambo bila hukumu ni kawaida.
Ubaya wa Jela ni mmoja tu “KUKOSA UHURU”
Anyway hongera mkuu na wote ambao wamemtembelea boss.
[HASHTAG]#freedom4Mello[/HASHTAG]
You can kill a revolutionary but you can't kill the revolution... Struggles continue.
 
119 Reactions
Reply
Back
Top Bottom