fredmlay
JF-Expert Member
- Apr 30, 2008
- 1,849
- 388
Nianze kwa kupongeza jamii ya wanamageuzi nchini kote kwa kuiwezesha CDM kufanikiwa kushinda kiti cha Ubunge Arumeru Mashariki, Viti vya udiwani kirumba Mwanza, Kiwira Mbeya na Lizaboni Songea. Ni ushindi mkubwa na wa kishindo..
Safari ndio kwanza imeanza tusibweteke lengo letu ni kufika bandarini salama yaani kuikomboa nchi toka utawala wa kifisadi.. Tulishuhudia mengi kupitia hizi chaguzi ndogo na kwakweli zimefungua wengi akili na kujionea jinsi utawala dhalimu unavyotumia lugha chafu (LL, Tyson, MN, nk), ubabe na kejeli (BWM), nguvu ya pesa (EL, OleM nk). Matukio yote haya yametufungua macho watanzania wengi na kujua umuhimu wa mageuzi katika maendeleo ya nchi yetu. Kwa mfano fedha iliyokuwa ikitumika kuwapatia waendesha Boda Boda kwenye misafara ya kampeni zingetosha kabisa kutatua angalau kero ya maji/madawati/madawa kwenye kata moja, lakini badala yake zinatumika kurubuni wapiga kura ili udhalimu uendelee kutawala.
Humu jamvini kulikuwa na mitazamo tofauti na lugha za kejeli, mimi binafsi napenda kukumbana na mitazamo tofauti kwani ndiyo inayokufanya kujitathmini na kutafuta mbinu bora zaidi za mafanikio, lakini hatuwezi kuwasahau kwa uchache wana-jamvi wafuatao:- Rejao, Pasco, Ritz, MS na Mtumishi aliyesema yeye atajinyonga CDM wakishinda AM..!Sijui kama tayari ni marehemu lakini nasubiri kusikia mshabiki wa mafisadi kajinyonga kwa Siyoi kuukosa ubunge. Hawa walijua mila, walijua hitaji la wana AM, walijua mafanikio mazuri kwa miaka 50 AM chini ya magamba, walijua umuhimu wa ndoa kwenye ubunge, walijua vema kuwalamba miguu watawala dhalimu sijui ni kwa kiasi gani cha malipo..!
Haya yote ni mapito hivyo yatusaidie kusonga mbele daima.. huu ni mwanzo tu wa M4C hivyo hatuna haja ya kubweteka, safari ni ngumu inahitaji kujitoa mhanga ili kufanikiwa kufika bandarini salama,
Rai yangu kwa wanamageuzi na viongozi kwa ujumla.. nguvu zetu sasa zielekezwe vijijini zaidi na ukanda wa Pwani wote pamoja Dar ambayo imekuwa nyuma kwenye mageuzi nchini. Tukifanikiwa hili tutarajie mashabiki wengi wa magamba/mafisadi kujinyonga.
Mungu ibari Tanzania, ibariki CDM na wanamageuzi wote..:A S-omg:
Safari ndio kwanza imeanza tusibweteke lengo letu ni kufika bandarini salama yaani kuikomboa nchi toka utawala wa kifisadi.. Tulishuhudia mengi kupitia hizi chaguzi ndogo na kwakweli zimefungua wengi akili na kujionea jinsi utawala dhalimu unavyotumia lugha chafu (LL, Tyson, MN, nk), ubabe na kejeli (BWM), nguvu ya pesa (EL, OleM nk). Matukio yote haya yametufungua macho watanzania wengi na kujua umuhimu wa mageuzi katika maendeleo ya nchi yetu. Kwa mfano fedha iliyokuwa ikitumika kuwapatia waendesha Boda Boda kwenye misafara ya kampeni zingetosha kabisa kutatua angalau kero ya maji/madawati/madawa kwenye kata moja, lakini badala yake zinatumika kurubuni wapiga kura ili udhalimu uendelee kutawala.
Humu jamvini kulikuwa na mitazamo tofauti na lugha za kejeli, mimi binafsi napenda kukumbana na mitazamo tofauti kwani ndiyo inayokufanya kujitathmini na kutafuta mbinu bora zaidi za mafanikio, lakini hatuwezi kuwasahau kwa uchache wana-jamvi wafuatao:- Rejao, Pasco, Ritz, MS na Mtumishi aliyesema yeye atajinyonga CDM wakishinda AM..!Sijui kama tayari ni marehemu lakini nasubiri kusikia mshabiki wa mafisadi kajinyonga kwa Siyoi kuukosa ubunge. Hawa walijua mila, walijua hitaji la wana AM, walijua mafanikio mazuri kwa miaka 50 AM chini ya magamba, walijua umuhimu wa ndoa kwenye ubunge, walijua vema kuwalamba miguu watawala dhalimu sijui ni kwa kiasi gani cha malipo..!
Haya yote ni mapito hivyo yatusaidie kusonga mbele daima.. huu ni mwanzo tu wa M4C hivyo hatuna haja ya kubweteka, safari ni ngumu inahitaji kujitoa mhanga ili kufanikiwa kufika bandarini salama,
Rai yangu kwa wanamageuzi na viongozi kwa ujumla.. nguvu zetu sasa zielekezwe vijijini zaidi na ukanda wa Pwani wote pamoja Dar ambayo imekuwa nyuma kwenye mageuzi nchini. Tukifanikiwa hili tutarajie mashabiki wengi wa magamba/mafisadi kujinyonga.
Mungu ibari Tanzania, ibariki CDM na wanamageuzi wote..:A S-omg: