KICHAKA
Member
- Jun 17, 2009
- 58
- 9
Ikiwa leo jaji ocampo kataja majina sita ya watuhumiwa wa uvunjaji wa amani Kenya, ni wazi kukosekana kwa Uhuru Kenyata na Ruto katika kinyang'anyiro hicho kunatoa mwanga kuwa safari ya Raila Odinga ni nyeupe. Kama hilo litakuwa hivyo ni wazi siasa za Kenya hazitakuwa na nguvu licha ya kuwepo katiba mpya na hivyo upo uwezekano wa kufunza nchi nyingine kama Tanzania ambazo nazo baadhi ya viongozi wake wengi wakiwa katika CDM waliamua kwa makusudi kuanza kuiga aina hiyo ya siasa. Kufuatia hali hii ni wazi kuwa Tanzania haitakuwa na kazi ya kubaini waanzilishi wa siasa za vitimbi kama nchi itaingia katika machafuko mwaka 2015 kwa kuwa sura na matendo yao yameanza kujionyesha mapema kabla ya wakati. Ni wazi hili ni funzo kubwa na linaweza kuchukua miaka kama waliolenga kutumia mbinu hii watakapokuwa na kazi ya kuumiza vichwa kutafuta njia nyingine.