Safari ya Mwisho ya Abdallah Kassim Hanga Kabla ya Safari ya Mwisho

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,853
30,197
PICHA YA ABDALLAH KASSIM HANGA AKIBARIZI MSASANI BEACH KWENYE NYUMBA YA OSCAR KAMBONA

Hakuna kitabu kilichoeleza historia ya Hanga na Oscar Kambona kwa siku chache Hanga lipokuwa anakaa nyumbani kwa Kambona London kama kitabu cha Dr. Harith Ghassany, ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.’’

Hanga alikuwa anatokea Conakry Guinea anarudi Tanzania akafikia nyumbani kwa Kambona.

Kambona akamsihi Hanga asirudi Tanzania abakie hapo hapo Uingereza kwani taarifa zake alizokuwanazo Kambona hazikuwa nzuri.

Hanga hakukubali ushauri wa Kambona akashikilia lazima arudi.

Kambona kwa kutaka Hanga abadilishe mawazo yake akawaita vijana wawili kutoka Zanzibar waliokuwa pale London waje wamsaidie katika kumshawishi ‘’mzee’’ wao abakie London.

Katika vijana hawa alikuwa Ahmed Rajab.

Kambona hakufanikiwa juu ya juhudi hizi alizofanya.

Qadar ya Allah ilikuwa imekwishapita Hanga alikuwa ameandikiwa kuuliwa Zanzibar.

Hilo ndilo lililokuja kuwa.
Haikuwa Kambona peke yake aliyemuonya.

Endelea kusoma.

Kuna mtu alinisikia Radio Kheri nafanya kipindi kuhusu historia ya Zanzibar na nikamweleza Hanga.

Huyu bwana akanitafuta ili anieleze mengi kuhusu Hanga kwani wakijuana vizuri Zanzibar toka udogo wao.

Tulikutana na akanieleza kisa cha Hanga kinachofanana na yale yaliyotokea London nyumbani kwa Kambona.

Huyu bwana anasema kuwa kulikuwa na vijana kiasi waliokimbilia Dar es Salaam baada ya mapinduzi kutafuta kazi na kuanza maisha mapya.

Yeye alikuwa mmoja wa hawa vijana wa Kizanzibari na alipata kazi katika kampuni moja ya ndege.

Ikawa kila ndege yake ikitua Dar es Salaam yeye anakuwa uwanjani kuipokea.

Anasema siku moja alikuwa uwanja wa ndege kupokea ndege yake akamuona mke wa Hanga, Bimkubwa pale uwanjani.

Akamfuata kumsalimia na kumuuliza mbona yuko pale.

Bimkubwa akajibu, ‘’Kassim anakuja leo nimekuja kumpokea.’’

‘’Mimi nilishtuka sana kwa kuwa sisi vijana kutoka Zanzibar tuliokuwa Dar es Salaam tulikuwa kila siku tunakutana na kupashana habari zinazotoka Zanzibar na taarifa kuhusu Hanga zilikuwa zinatisha.

Huu ulikuwa wakati watu wanakamatwa na kupelekwa jela utasikia fulani kakamatwa jana usiku, fulani inahofiwa kauliwa na taarifa nyingi mfano wa hizo zilizokuwa zinatisha sana.''

Mpashaji wangu anasema yeye aliingia hadi ndani ya ndege kumlaki Hanga.

Akamuomba wale chakula pamoja pale uwanjani yeye na mkewe Bimkubwa kisha ndiyo wende zao.

Alimpatia nafasi Hanga na kumtahadharisha kuwa wala asitoke pale uwanja wa ndege kwenda nyumbani bali abakie pale pale na arudi London na ndege ile ile na kimya kimya.

Mpashaji wangu akanieleza kwa masikitiko makubwa kuwa Hanga alimkatalia.

Wakaagana Hanga akaondoka na mkewe.

Yaliyomfika Hanga yanafahamika.
Kalamu ya Allah ilkikuwa imeshaandika kalamu imenyanyuliwa na wino umekauka.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Hanga akiwa Msasani Beach alipokuwa anakaa kwenye nyumba ya Oscar Kambona.

Ilikuwa bila shaka kutoka nyumba hii ndipo alipochukuliwa kupelekwa Ukonga Prison nakutoka hapo akarejeshwa Zanzibar.

1669353044458.png
 
Hakika siku ya mwisho tutaona mengi. Pengine walioonewa wataamka wakilia na kukumbuka uasi dhidi yao. Uasi dhidi ya uhai wao.
Kwani walikua Ni wenye kustahili yaliyowapata?
Watauliza kwa watesi wao.
Na kwa hakika siku inakuja! Siku ya suluhisho la kila sintofahamu.
Akina sie pengine tutashangaa.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
PICHA YA ABDALLAH KASSIM HANGA AKIBARIZI MSASANI BEACH KWENYE NYUMBA YA OSCAR KAMBONA

Hakuna kitabu kilichoeleza historia ya Hanga na Oscar Kambona kwa siku chache Hanga lipokuwa anakaa nyumbani kwa Kambona London kama kitabu cha Dr. Harith Ghassany, ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.’’

Hanga alikuwa anatokea Conakry Guinea anarudi Tanzania akafikia nyumbani kwa Kambona.

Kambona akamsihi Hanga asirudi Tanzania abakie hapo hapo Uingereza kwani taarifa zake alizokuwanazo Kambona hazikuwa nzuri.

Hanga hakukubali ushauri wa Kambona akashikilia lazima arudi.

Kambona kwa kutaka Hanga abadilishe mawazo yake akawaita vijana wawili kutoka Zanzibar waliokuwa pale London waje wamsaidie katika kumshawishi ‘’mzee’’ wao abakie London.

Katika vijana hawa alikuwa Ahmed Rajab.

Kambona hakufanikiwa juu ya juhudi hizi alizofanya.

Qadar ya Allah ilikuwa imekwishapita Hanga alikuwa ameandikiwa kuuliwa Zanzibar.

Hilo ndilo lililokuja kuwa.
Haikuwa Kambona peke yake aliyemuonya.

Endelea kusoma.

Kuna mtu alinisikia Radio Kheri nafanya kipindi kuhusu historia ya Zanzibar na nikamweleza Hanga.

Huyu bwana akanitafuta ili anieleze mengi kuhusu Hanga kwani wakijuana vizuri Zanzibar toka udogo wao.

Tulikutana na akanieleza kisa cha Hanga kinachofanana na yale yaliyotokea London nyumbani kwa Kambona.

Huyu bwana anasema kuwa kulikuwa na vijana kiasi waliokimbilia Dar es Salaam baada ya mapinduzi kutafuta kazi na kuanza maisha mapya.

Yeye alikuwa mmoja wa hawa vijana wa Kizanzibari na alipata kazi katika kampuni moja ya ndege.

Ikawa kila ndege yake ikitua Dar es Salaam yeye anakuwa uwanjani kuipokea.

Anasema siku moja alikuwa uwanja wa ndege kupokea ndege yake akamuona mke wa Hanga, Bimkubwa pale uwanjani.

Akamfuata kumsalimia na kumuuliza mbona yuko pale.

Bimkubwa akajibu, ‘’Kassim anakuja leo nimekuja kumpokea.’’

‘’Mimi nilishtuka sana kwa kuwa sisi vijana kutoka Zanzibar tuliokuwa Dar es Salaam tulikuwa kila siku tunakutana na kupashana habari zinazotoka Zanzibar na taarifa kuhusu Hanga zilikuwa zinatisha.

Huu ulikuwa wakati watu wanakamatwa na kupelekwa jela utasikia fulani kakamatwa jana usiku, fulani inahofiwa kauliwa na taarifa nyingi mfano wa hizo zilizokuwa zinatisha sana.''

Mpashaji wangu anasema yeye aliingia hadi ndani ya ndege kumlaki Hanga.

Akamuomba wale chakula pamoja pale uwanjani yeye na mkewe Bimkubwa kisha ndiyo wende zao.

Alimpatia nafasi Hanga na kumtahadharisha kuwa wala asitoke pale uwanja wa ndege kwenda nyumbani bali abakie pale pale na arudi London na ndege ile ile na kimya kimya.

Mpashaji wangu akanieleza kwa masikitiko makubwa kuwa Hanga alimkatalia.

Wakaagana Hanga akaondoka na mkewe.

Yaliyomfika Hanga yanafahamika.
Kalamu ya Allah ilkikuwa imeshaandika kalamu imenyanyuliwa na wino umekauka.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Hanga akiwa Msasani Beach alipokuwa anakaa kwenye nyumba ya Oscar Kambona.

Ilikuwa bila shaka kutoka nyumba hii ndipo alipochukuliwa kupelekwa Ukonga Prison nakutoka hapo akarejeshwa Zanzibar.

View attachment 2426886
asante angalau umenipa mwanga kidogo kuhusu huyu mtu.
Allah akuongezee maisha marefu zaidi
 
Hakika Mzee Mohamed, wewe ni Maktaba tosha kabisa ya kutupatia mengi ya kihistoria yaliyotokea katika nchi hii! Mwenyezi Mungu akuongezee umri mrefu zaidi.
 
PICHA YA ABDALLAH KASSIM HANGA AKIBARIZI MSASANI BEACH KWENYE NYUMBA YA OSCAR KAMBONA

Hakuna kitabu kilichoeleza historia ya Hanga na Oscar Kambona kwa siku chache Hanga lipokuwa anakaa nyumbani kwa Kambona London kama kitabu cha Dr. Harith Ghassany, ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.’’

Hanga alikuwa anatokea Conakry Guinea anarudi Tanzania akafikia nyumbani kwa Kambona.

Kambona akamsihi Hanga asirudi Tanzania abakie hapo hapo Uingereza kwani taarifa zake alizokuwanazo Kambona hazikuwa nzuri.

Hanga hakukubali ushauri wa Kambona akashikilia lazima arudi.

Kambona kwa kutaka Hanga abadilishe mawazo yake akawaita vijana wawili kutoka Zanzibar waliokuwa pale London waje wamsaidie katika kumshawishi ‘’mzee’’ wao abakie London.

Katika vijana hawa alikuwa Ahmed Rajab.

Kambona hakufanikiwa juu ya juhudi hizi alizofanya.

Qadar ya Allah ilikuwa imekwishapita Hanga alikuwa ameandikiwa kuuliwa Zanzibar.

Hilo ndilo lililokuja kuwa.
Haikuwa Kambona peke yake aliyemuonya.

Endelea kusoma.

Kuna mtu alinisikia Radio Kheri nafanya kipindi kuhusu historia ya Zanzibar na nikamweleza Hanga.

Huyu bwana akanitafuta ili anieleze mengi kuhusu Hanga kwani wakijuana vizuri Zanzibar toka udogo wao.

Tulikutana na akanieleza kisa cha Hanga kinachofanana na yale yaliyotokea London nyumbani kwa Kambona.

Huyu bwana anasema kuwa kulikuwa na vijana kiasi waliokimbilia Dar es Salaam baada ya mapinduzi kutafuta kazi na kuanza maisha mapya.

Yeye alikuwa mmoja wa hawa vijana wa Kizanzibari na alipata kazi katika kampuni moja ya ndege.

Ikawa kila ndege yake ikitua Dar es Salaam yeye anakuwa uwanjani kuipokea.

Anasema siku moja alikuwa uwanja wa ndege kupokea ndege yake akamuona mke wa Hanga, Bimkubwa pale uwanjani.

Akamfuata kumsalimia na kumuuliza mbona yuko pale.

Bimkubwa akajibu, ‘’Kassim anakuja leo nimekuja kumpokea.’’

‘’Mimi nilishtuka sana kwa kuwa sisi vijana kutoka Zanzibar tuliokuwa Dar es Salaam tulikuwa kila siku tunakutana na kupashana habari zinazotoka Zanzibar na taarifa kuhusu Hanga zilikuwa zinatisha.

Huu ulikuwa wakati watu wanakamatwa na kupelekwa jela utasikia fulani kakamatwa jana usiku, fulani inahofiwa kauliwa na taarifa nyingi mfano wa hizo zilizokuwa zinatisha sana.''

Mpashaji wangu anasema yeye aliingia hadi ndani ya ndege kumlaki Hanga.

Akamuomba wale chakula pamoja pale uwanjani yeye na mkewe Bimkubwa kisha ndiyo wende zao.

Alimpatia nafasi Hanga na kumtahadharisha kuwa wala asitoke pale uwanja wa ndege kwenda nyumbani bali abakie pale pale na arudi London na ndege ile ile na kimya kimya.

Mpashaji wangu akanieleza kwa masikitiko makubwa kuwa Hanga alimkatalia.

Wakaagana Hanga akaondoka na mkewe.

Yaliyomfika Hanga yanafahamika.
Kalamu ya Allah ilkikuwa imeshaandika kalamu imenyanyuliwa na wino umekauka.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Hanga akiwa Msasani Beach alipokuwa anakaa kwenye nyumba ya Oscar Kambona.

Ilikuwa bila shaka kutoka nyumba hii ndipo alipochukuliwa kupelekwa Ukonga Prison nakutoka hapo akarejeshwa Zanzibar.

View attachment 2426886

To be continue.....
 
PICHA YA ABDALLAH KASSIM HANGA AKIBARIZI MSASANI BEACH KWENYE NYUMBA YA OSCAR KAMBONA

Hakuna kitabu kilichoeleza historia ya Hanga na Oscar Kambona kwa siku chache Hanga lipokuwa anakaa nyumbani kwa Kambona London kama kitabu cha Dr. Harith Ghassany, ‘’Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru.’’

Hanga alikuwa anatokea Conakry Guinea anarudi Tanzania akafikia nyumbani kwa Kambona.

Kambona akamsihi Hanga asirudi Tanzania abakie hapo hapo Uingereza kwani taarifa zake alizokuwanazo Kambona hazikuwa nzuri.

Hanga hakukubali ushauri wa Kambona akashikilia lazima arudi.

Kambona kwa kutaka Hanga abadilishe mawazo yake akawaita vijana wawili kutoka Zanzibar waliokuwa pale London waje wamsaidie katika kumshawishi ‘’mzee’’ wao abakie London.

Katika vijana hawa alikuwa Ahmed Rajab.

Kambona hakufanikiwa juu ya juhudi hizi alizofanya.

Qadar ya Allah ilikuwa imekwishapita Hanga alikuwa ameandikiwa kuuliwa Zanzibar.

Hilo ndilo lililokuja kuwa.
Haikuwa Kambona peke yake aliyemuonya.

Endelea kusoma.

Kuna mtu alinisikia Radio Kheri nafanya kipindi kuhusu historia ya Zanzibar na nikamweleza Hanga.

Huyu bwana akanitafuta ili anieleze mengi kuhusu Hanga kwani wakijuana vizuri Zanzibar toka udogo wao.

Tulikutana na akanieleza kisa cha Hanga kinachofanana na yale yaliyotokea London nyumbani kwa Kambona.

Huyu bwana anasema kuwa kulikuwa na vijana kiasi waliokimbilia Dar es Salaam baada ya mapinduzi kutafuta kazi na kuanza maisha mapya.

Yeye alikuwa mmoja wa hawa vijana wa Kizanzibari na alipata kazi katika kampuni moja ya ndege.

Ikawa kila ndege yake ikitua Dar es Salaam yeye anakuwa uwanjani kuipokea.

Anasema siku moja alikuwa uwanja wa ndege kupokea ndege yake akamuona mke wa Hanga, Bimkubwa pale uwanjani.

Akamfuata kumsalimia na kumuuliza mbona yuko pale.

Bimkubwa akajibu, ‘’Kassim anakuja leo nimekuja kumpokea.’’

‘’Mimi nilishtuka sana kwa kuwa sisi vijana kutoka Zanzibar tuliokuwa Dar es Salaam tulikuwa kila siku tunakutana na kupashana habari zinazotoka Zanzibar na taarifa kuhusu Hanga zilikuwa zinatisha.

Huu ulikuwa wakati watu wanakamatwa na kupelekwa jela utasikia fulani kakamatwa jana usiku, fulani inahofiwa kauliwa na taarifa nyingi mfano wa hizo zilizokuwa zinatisha sana.''

Mpashaji wangu anasema yeye aliingia hadi ndani ya ndege kumlaki Hanga.

Akamuomba wale chakula pamoja pale uwanjani yeye na mkewe Bimkubwa kisha ndiyo wende zao.

Alimpatia nafasi Hanga na kumtahadharisha kuwa wala asitoke pale uwanja wa ndege kwenda nyumbani bali abakie pale pale na arudi London na ndege ile ile na kimya kimya.

Mpashaji wangu akanieleza kwa masikitiko makubwa kuwa Hanga alimkatalia.

Wakaagana Hanga akaondoka na mkewe.

Yaliyomfika Hanga yanafahamika.
Kalamu ya Allah ilkikuwa imeshaandika kalamu imenyanyuliwa na wino umekauka.

Picha hiyo hapo chini inamuonyesha Hanga akiwa Msasani Beach alipokuwa anakaa kwenye nyumba ya Oscar Kambona.

Ilikuwa bila shaka kutoka nyumba hii ndipo alipochukuliwa kupelekwa Ukonga Prison nakutoka hapo akarejeshwa Zanzibar.

View attachment 2426886
Kazi sana. Hii ilikuwa baada ya kifo cha Karume au kabla?
 
Kazi sana. Hii ilikuwa baada ya kifo cha Karume au kabla?
Ilikuwa kabla ya kifo cha Karume.

Siku moja wakati niko darasa la sita palifanyika maandamano makubwa sana ya 'kuupinga ushirazi'. Kama ilivyo kawaida wanafunzi wote tuliambiwa lazima tuhudhurie maandamano yale. Lengo lilikuwa kuwalaani Hanga na Othman Sharifu (hili tulikuja kulifahamu baadae). Inasemekana ndiyo siku 'waliyopotea'
 
mapinduzi ya zanzibar kwa ukaribu kabisa ni kama yalikuwa na umwagaji damu sana ila kutokana na mkono wa serikali yana onekana kama yalikuwa sio ya umwagaji damu.
 
Ilikuwa kabla ya kifo cha Karume.

Siku moja wakati niko darasa la sita palifanyika maandamano makubwa sana ya 'kuupinga ushirazi'. Kama ilivyo kawaida wanafunzi wote tuliambiwa lazima tuhudhurie maandamano yale. Lengo lilikuwa kuwalaani Hanga na Othman Sharifu (hili tulikuja kulifahamu baadae). Inasemekana ndiyo siku 'waliyopotea'
Kama ndivyo, huu mzigo anaubeba nani? Professor Mohammed Babu alinusurikaje?
 
mapinduzi ya zanzibar kwa ukaribu kabisa ni kama yalikuwa na umwagaji damu sana ila kutokana na mkono wa serikali yana onekana kama yalikuwa sio ya umwagaji damu.
Labda kwa wazawa wa nje ya visiwa vile, lakini wazanzibari wanajua vyema yaliyotendeka.

Lakini miaka imeshapita kwa hivyo lililobaki ni kuomba dua kwa Mwenyezi Mungu yasitokee tena kama yale.
 
Kama ndivyo, huu mzigo anaubeba nani? Professor Mohammed Babu alinusurikaje?
Baada ya mapinduzi Babu yeye alipelekwa bara na kupewa cheo cha uwaziri. Lakini alituhumiwa kuwa yeye ndiyo organiser wa lile kundi lililomuua Karume.

Alisalimika (yeye na Ali Mahfoudh) kwa vile walikamatwa bara na walifungwa bara.
 
Ilikuwa kabla ya kifo cha Karume.

Siku moja wakati niko darasa la sita palifanyika maandamano makubwa sana ya 'kuupinga ushirazi'. Kama ilivyo kawaida wanafunzi wote tuliambiwa lazima tuhudhurie maandamano yale. Lengo lilikuwa kuwalaani Hanga na Othman Sharifu (hili tulikuja kulifahamu baadae). Inasemekana ndiyo siku 'waliyopotea'
Ongea zaidi wewe ambae uliwepo wakati wake...

Binafsi nimejitahidi sana kusoma vyanzo mbalimbali juu ya siasa za ZNZ za wakati ule, na si haba, nilijifunza mengi mno.

Nilikuwa na rundo la telegrams za mawasiliano ya Wakoloni wakipashana yaliyokuwa yanajiri ZNZ... cjui nimeipotezea wapi hazina ile!

Simulizi ya Hanga ni moja ya simulizi mzuri na za kuhudhunisha ingawaje sikupenda hatua yake ya kumtelekeza mtoto alipoenda kusoma Russia.

Mwanzoni sikuamini taarifa hii lakini nilipofanya uchunguzi wa ziada, nikakuta kweli, na yule binti yake yule alikuja hadi ZNZ kuifahamu asili yake.
 
Ongea zaidi wewe ambae uliwepo wakati wake...
Enzi zile ilikuwa hakuna uhuru wa vyombo vya habari kwa hivyo habari zikizungumzwa kwa kunong'ona, halafu ukiwa mtoto ndiyo kabisa hutakiwi kuyasikia hayo yanayozungumwa kwa kificho. Mambo mengi tumekuja kuyajua baada ya kifo cha Karume na wengine kujaribu kuandika vitabu. Ama wale waliochukuliwa na wasiojulikana tulikuwa tunawajua baadhi yao ni ndugu au jirani zetu.

Hata mimi niliwahi kusoma zile declassified reports za CIA zilizokuwa kwenye mitandao pamoja na vitabu kama vya akina Amani Thani na wengine. Amani Thani anazo series zake kwenye youtube ukimsikiliza utapata picha ya mambo yaliyokuwa yakitendeka. Na kama unavyovijua visiwa vya Zanzibar watesaji wote walikuwa wanafahamika vizuri.
 
Enzi zile ilikuwa hakuna uhuru wa vyombo vya habari kwa hivyo habari zikizungumzwa kwa kunong'ona, halafu ukiwa mtoto ndiyo kabisa hutakiwi kuyasikia hayo yanayozungumwa kwa kificho. Mambo mengi tumekuja kuyajua baada ya kifo cha Karume na wengine kujaribu kuandika vitabu. Ama wale waliochukuliwa na wasiojulikana tulikuwa tunawajua baadhi yao ni ndugu au jirani zetu.

Hata mimi niliwahi kusoma zile declassified reports za CIA zilizokuwa kwenye mitandao pamoja na vitabu kama vya akina Amani Thani na wengine. Amani Thani anazo series zake kwenye youtube ukimsikiliza utapata picha ya mambo yaliyokuwa yakitendeka. Na kama unavyovijua visiwa vya Zanzibar watesaji wote walikuwa wanafahamika vizuri.

..panahitajika kuundwe TUME YA UKWELI HAKI NA MARIDHIANO ili ukweli wote wa yaliyojiri uwekwe wazi.

..hiyo itachora mstari kwamba MAOVU yaliyotokea hayana nafasi tena ktk jamii yetu.

..kwasababu tumeacha hali iwe kama ilivyo ndio maana tunashuhudia umwagaji damu ukitokea ktk kila uchaguzi mkuu wa Zanzibar.
 
..panahitajika kuundwe TUME YA UKWELI HAKI NA MARIDHIANO ili ukweli wote wa yaliyojiri uwekwe wazi.

..hiyo itachora mstari kwamba MAOVU yaliyotokea hayana nafasi tena ktk jamii yetu.

..kwasababu tumeacha hali iwe kama ilivyo ndio maana tunashuhudia umwagaji damu ukitokea ktk kila uchaguzi mkuu wa Zanzibar.
Wengi wameshaondoka duniani kwa hivi sasa. Baadhi wameandika vitabu na baadhi wameamua kunyamazia tu. Mfano:
  • Ali Muhsin Barwani
  • Amani Thani Ferooz
  • Khamis Abdulla Ameir (yu hai)
  • Abdurrahman Babu (kupitia Amrit Wilson)
  • Mohammed Ghassany (yu hai)
  • Ali Sultani Issa
  • Hashil Seif (yu hai)
  • Biubwa Amour Zahor (yu hai) - huyu kitabu chake kimeelemea zaidi kwenye historia ya maisha yake na ushiriki wake kisiasa kabla na baada ya mapinduzi.

Ukiondoa Ghassany hawa wengine walikuwa katika mrengo wa chama Umma Party au Zanzibar Nationalist Party kwa hivyo baadhi ya watu wanasema historia yao imeelemea upande wa upinzani. Lakini bado kuna vitu vingi vya kujifunza ndani yake.

Walioandika kwa upande wa ASP
  • Thabit Kombo - kitabu chake kilitoka baada ya kifo chake. Baadhi wanasema kuna nyongeza za mambo ambazo wana uhakika hazikutoka kwenye mdomo wake.
  • Ramadhani Mapuri - kitabu kimeacha mambo mengi hasa yanayohusu vyama vya upinzani vilivyokuwepo kabla ya mapinduzi na hivyo kuifanya historia kuwa ya upande mmoja.

Pia viko vya wazungu mfano M Loftchie (Background to Revolution) na Okello pia aliandika kitabu (nimekisahau jina)
 
Back
Top Bottom