Profesa
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 905
- 624
Kiongozi taratibu, sio wote kuna baadhi ambao ni shida kidogo kwa ufahamu wao na mtizamo walio nao, tatizo watu hawasomi yawezekana hata baadhi ya nyaraka a=zianazopatikana hata humu zikizi=ungumzia maswala haya labda hazikuwa katika lugha wanayoielewa.Kwakweli ninasikitishwa na lugha hizi na hasa zinapotolewa na watanzania " ETI VITA YAKO NAPE DHIDI YA UFISADI" hivi kumbe ni vita yangu?!!!! Kwa kuwa mie ndo mwathirika mkubwa wa ufisadi!!!??? Nape wa 2005 ni yupi na Nape wa2012 ni yupi? INAVUNJA MOYO SANA UNAPOJITOLEA KUPAMBANA NA UFISADI KWA FAIDA YETU NA WATOTO WETU NA HATA WAJUU ZETU HALAFU ANATOKEA MTU ANADAI HII VITA NI YANGU KAMA VILE NI KWA FAIDA YANGU, OOOOPS! Watanzania zaidi ya uwajuavyo!
Unajua pia usisahau hawa ndiyo wanaoshangilia wakisikia mtu anadhalilika au kudhurika, hawa ni hatari sana maana wao tuhuma huzigeuza hukumu haraka haraka, bila kutumia muda kufikiri wanakumbwa na upepo wa kisiasa na wa magazeti yanayojaribu kufanya biashara na mwisho wanakuwa na mawazo ya ajabu kabisa.
Laiti wangeujua ukweli wa haya yote