Safari ya Igunga

Lukansola

JF-Expert Member
Sep 5, 2010
5,435
1,597
Ninapoandika habari hii, nipo safarini nikitoke Igunga, hii ndio imekuwa mara yangu ya kwanza kutembelea wilaya hii.

napenda ku-share nanyi ndugu zangu kuhusu machache niliyojifunza katika siku mbili nilizoishi hapo. Nikianzia na hali ya hewa kwa sasa Igunga kuna joto kiasi. Jambo ambalo nimeliona pia ni kwamba maisha ya wananchi wa Igunga hayana tofauti sana na maisha ya wakazi wa wilaya zingine za nchi hii. Umeme upo lakini mgao ni kama sehemu zingine. Maji ya Igunga ni ya visima na ni meusi kusema kweli.

Nimekuwa nikisikia mara nyingi kuwa RA amewapa Igunga maisha bora na hata Mkapa kwenye kampeni alisema Igunga iko juu katika mkoa wa Tabora. Mimi napinga kwa sababu wananchi wa Igunga wamechoka tu, mji umejaa vumbi jekundu. Stendi mpya ya mabasi ni mavumbi matupu.

Jambo lililonishanga ni kusikia kuwa kumbe Rostam hana nyumba Igunga na kuna sehemu nyingi za vijijini ambazo hawamji wala hawakuwahi kumwona Rostam, mwenyeji mmoja aliniambia Rostam hajawahi kulala Igunga hata siku moja, huwa analala Mwanza.

Nikiwa nasubiri basi, nimepata fursa ya kupiga story na vijana pale stendi, inaoneka safari hii ccm haikatishi maana kusema kweli watu wamebadilika, wanasema wamechoka kudanganywa na hawaitaki ccm. wanasema ccm imeleta watu ili kuwapeleleza na kuwashawishi vijana kuichagua ccm lakini wamekuwa wakiwaambia waziwazi kuwa wameshachoka na wasipotezewe muda wao.

Kuhusu Dr. Kafumu ni kuwa amejenga nyumba chapchap wakati wa kura za maoni ili kujionesha ni mwenyeji wa huko.

Pembeni yangu nilimsikia mzee mmoja wa kike akiwauliza wazee wenzie wa kiume wawili aliokuwa akizungumza nao kwamba wao ni vyama gani? Yeye aliwaambia ni chadema hata wale wazee walimjibu hivyohivyo.

Kwa mtazamo wangu kutokana na experiance yangu ya muda mfupi ccm huenda wakalikosa jimbo hilo. I've got some pictures of Igunga but can't attach them cause am using a phone.
 
ahsante mkuu lukansola kwa kutushirikisha uzoefu ulioupata igunga. mkuu ulijaribu kufanya ka utafiti kadogo juu ya hizi jezi za ccm, wananchi wa igunga wanaziheshimu, au wakimuona mtu kava sare hizo wanamuhusisha na rushwa, kama hakutaoa basi kapokea! ingawa hivyo tunakutakieni safari njema.
 
Lets hope chadema wins, for our own benefit we need More opposition MPs to make the government deliver
 
ahsante mkuu lukansola kwa kutushirikisha uzoefu ulioupata igunga. mkuu ulijaribu kufanya ka utafiti kadogo juu ya hizi jezi za ccm, wananchi wa igunga wanaziheshimu, au wakimuona mtu kava sare hizo wanamuhusisha na rushwa, kama hakutaoa basi kapokea! ingawa hivyo tunakutakieni safari njema.

Nilimtania kijana mmoja aliyekuwa amevaa T shirt ya kijani, akaniambia kaka hizi tuavaa tu, kwa kifupi watu wengi sana wanaonesha kuchoka na ccm. Pia nimekumbuka Igunga kuna ATM moja tu na haichukui Visa Card, mitandao ya mawasiliano kama simu na intenet pia ni dhaifu sana. Jogi kwa mtazamo wangu kama uchaguzi ukiwa huru na haki... Mmmmhhh.
 
Ninapoandika habari hii, nipo safarini nikitoke Igunga, hii ndio imekuwa mara yangu ya kwanza kutembelea wilaya hii.

napenda ku-share nanyi ndugu zangu kuhusu machache niliyojifunza katika siku mbili nilizoishi hapo. Nikianzia na hali ya hewa kwa sasa Igunga kuna joto kiasi. Jambo ambalo nimeliona pia ni kwamba maisha ya wananchi wa Igunga hayana tofauti sana na maisha ya wakazi wa wilaya zingine za nchi hii. Umeme upo lakini mgao ni kama sehemu zingine. Maji ya Igunga ni ya visima na ni meusi kusema kweli.

Nimekuwa nikisikia mara nyingi kuwa RA amewapa Igunga maisha bora na hata Mkapa kwenye kampeni alisema Igunga iko juu katika mkoa wa Tabora. Mimi napinga kwa sababu wananchi wa Igunga wamechoka tu, mji umejaa vumbi jekundu. Stendi mpya ya mabasi ni mavumbi matupu.

Jambo lililonishanga ni kusikia kuwa kumbe Rostam hana nyumba Igunga na kuna sehemu nyingi za vijijini ambazo hawamji wala hawakuwahi kumwona Rostam, mwenyeji mmoja aliniambia Rostam hajawahi kulala Igunga hata siku moja, huwa analala Mwanza.

Nikiwa nasubiri basi, nimepata fursa ya kupiga story na vijana pale stendi, inaoneka safari hii ccm haikatishi maana kusema kweli watu wamebadilika, wanasema wamechoka kudanganywa na hawaitaki ccm. wanasema ccm imeleta watu ili kuwapeleleza na kuwashawishi vijana kuichagua ccm lakini wamekuwa wakiwaambia waziwazi kuwa wameshachoka na wasipotezewe muda wao.

Kuhusu Dr. Kafumu ni kuwa amejenga nyumba chapchap wakati wa kura za maoni ili kujionesha ni mwenyeji wa huko.

Pembeni yangu nilimsikia mzee mmoja wa kike akiwauliza wazee wenzie wa kiume wawili aliokuwa akizungumza nao kwamba wao ni vyama gani? Yeye aliwaambia ni chadema hata wale wazee walimjibu hivyohivyo.

Kwa mtazamo wangu kutokana na experiance yangu ya muda mfupi ccm huenda wakalikosa jimbo hilo. I've got some pictures of Igunga but can't attach them cause am using a phone.

Hapo kwenye red, kujenga chap chap ni within how many days or weeks, tangu msingi hadi finishing? Ina maana Kafumu kama huko ni kwao hakuna nyumba ya wazazi wake hapo kijijini kwao hata ahitaji kujenga nyumba chap chap ili kujionesha ni mwenyeji wa huko?
 
Mkuu, hukupata "bahati" ya kukutana na Malaria Sugu? Yupo huko tangu last week akigawa t-shirt na kofia za ccm. Nimeona na Ritz1 nae akiandika kuwa tar 3 atapitia Moro akitokea huko!
Ulipata bahati ya kushuhudia mkutano wowote wa kampeni huko. Kama ndiyo, how was it!?
 
Mkuu, hukupata "bahati" ya kukutana na Malaria Sugu? Yupo huko tangu last week akigawa t-shirt na kofia za ccm. Nimeona na Ritz1 nae akiandika kuwa tar 3 atapitia Moro akitokea huko!
Ulipata bahati ya kushuhudia mkutano wowote wa kampeni huko. Kama ndiyo, how was it!?

Mkuu hao wajakazi wa nape wamekwenda igunga kwenye keyboards, kama bosi wao mwenyewe amepigwa marufuku kukanyaga igunga sasa wao watapataje nafasi ya kwenda huko?
 
Mkuu, hukupata "bahati" ya kukutana na Malaria Sugu? Yupo huko tangu last week akigawa t-shirt na kofia za ccm. Nimeona na Ritz1 nae akiandika kuwa tar 3 atapitia Moro akitokea huko!
Ulipata bahati ya kushuhudia mkutano wowote wa kampeni huko. Kama ndiyo, how was it!?

Niliona uzi wake akisema yuko Igunga nikamwambia tukutane tupige story akaniambia anaogopa tindikali.
 
Lets hope chadema wins, for our own benefit we need More opposition MPs to make the government deliver

Honestly kwa hali niliyoiona huko ni kwamba ccm hawana chao, mpaka wazee wana support cdm kwa sasa.
 
Hapo kwenye red, kujenga chap chap ni within how many days or weeks, tangu msingi hadi finishing? Ina maana Kafumu kama huko ni kwao hakuna nyumba ya wazazi wake hapo kijijini kwao hata ahitaji kujenga nyumba chap chap ili kujionesha ni mwenyeji wa huko?

Mama Mdogo kwa taarifa yako hata RA hana nyumba Igunga, this means hakuna mtu anayejua kwa RA ni wapi igunga.
 
Niliona uzi wake akisema yuko Igunga nikamwambia tukutane tupige story akaniambia anaogopa tindikali.



How!? Anaogopa tindikali wakati ameibeba! Alisema anakwenda kuimaliza kabisa cdm huko, nikajua yupo full equiped!
 
Back
Top Bottom