simon mato
JF-Expert Member
- Sep 27, 2015
- 926
- 484
Ndugu wanajamvi;
Kama kawaida yangu kuongea na kuandika ukweli kuhusu mambo yenye maslahi mapana katika taifa letu, Kama mada inavosema CHADEMA ndiyo chama kikuu cha upinzani hapa Tanzania ambacho kinajinasibu kushika hatamu 2020 na kuongoza kidemokrasia lakini kwangu mimi bado naona kama kuna wingu nene limetanda hapo chamani, ebu tuangalia mambo yafuatayo;
1:KILICHOTOKEA UCHAGUZI KANDA YA NYASA NI DEMOKRASIA WANAYOIHUBIRI???
Ni vyema ikaeleweka kuwa hiki chama kimejipambanua kuupinga utawala wa awamu ya tano kwa kile kinachoitwa "Udikteta" au utawala ambao haufuati demokrasia yawezekana ni kweli au si kweli! Lakini na wao wanajitawala kidemokrasia???
Tuchukulie mfano mathalani kilichotokea Uchaguzi kanda ya nyasa;
1. Wajumbe halali =98
2. Waliosusia =28
3. Waliopiga kura =106
4. Kura za ndio kwa msigwa =62
5. Kura za hapana =44
Maswali tata kutoka kwenye hizo data zetu!!
1. Wajumbe halali ni 98 je hawa waliongezeka wametoka wap? Na nani kawaleta?
2. Ni kwanini P. Ole. Sosopi akatwe siku ya kupiga kura? Is this democracy? Waliomkata wana hofu gani na huyu kijana?
3. Je kuna picha gani gani kama waliomkataa Msigwa ni 44 na waliosusa ni 28 ambao jumla yao ni 72?? Wakati msigwa jumla ana kura 62!!!
4. Ni vigezo vipi vimetumika kumkata P. Ole. Sosopi?? Na vigezo vipi vimetumika kumhalalisha P. Msigwa??
5. Ni Nani aliyemkata P. Ole. Sospi?
6. Je uchaguzi ulikuwa wa huru na haki? Wasimamizi wa uchaguzi ni akina nani? Na wanapatikaneje hawa wasimamizi wa uchaguzi?
7. Je ni kwanini hakuna kuhoji matokeo ya uchaguzi ndani ya chama kutokana na katiba ya chama? Hamuoni aibu mnataka kuhoji uchaguzi wa rais kama nyie wenyewe matokeo ya ndani ya chama hakuna kuhoji?
maswali yangu yameishia hapo lakini naomba tujikumbushe yafuatayo;
:UCHAGUZI VITI MAALUM CHADEMA:
Ni vyema tujikumbushe kwenye huo huo ukanda kulitokea uchafu na kuhalalishwa na makao makuu kwenye uteuzi wa viti maalum wengine walioteuliwa hawajulikani ata kwenye uongozi wa wilaya, mkoa na ata kanda lakini makao makuu yakabariki tuuh.
Majina yalikuwa mageni kabsaa kwenye uongozi wa wilaya na mkoa kwa sababu Mkoa wenyewe walituma jina makao makuu lakini cha ajabu na cha kusikitisha Mtu anayepewa Ubunge wa viti maalum siyo Mwenyeji wa huo mkoa bila kutolea ufafanuzi ata kidogo! Je hii ndo demokrasia wanayoitaka chadema?
:KURA ZA MAONI UBUNGE:
Hapa kulikuwa na manung'uniko mengi na yenye ushaidi wa kutosha kuwa baadhi ya majina yalitoka moja kwa moja kwa Mwenyekiti wa chama ikikuwa awe ameshinda au hajashinda ni lazima atangazwe? Is this people's power?
Wengine walipitishwa kwa rushwa, na hili mhe. SUGU angalau aliifiksha makao makuu na kuweka ushaidi lakini cha kushangaza mpaka leo hakuna ufafanuzi wowote uliotolewa Makao Makuu wameufyata kama vile hawajui kilichotokea.
: HAKUNA TAASISI AU WATU KUHOJI UHARAMIA HUU: JE HII NI DEMOKRASIA??
I mean taasisi za ndani ya chama like BAVICHA & BAWACHA sijawahi sikia wakihoji uharamia wowote ndani ya chama! Kuna nini nyuma ya pazia?? Au ata personal feeling itokee basi iwe individual! Hamna niliyesikia akihoji uharamia lakini kuna watu wamejitolea kufa na kupona kwenye chama hiki tusiwakatishe tamaaa.
Yangu ni hayo tuuh kwa leo.
Ni wako kijana mtiifu, mzalendo na Mwanaharakati wa kweli TZ.
Kama kawaida yangu kuongea na kuandika ukweli kuhusu mambo yenye maslahi mapana katika taifa letu, Kama mada inavosema CHADEMA ndiyo chama kikuu cha upinzani hapa Tanzania ambacho kinajinasibu kushika hatamu 2020 na kuongoza kidemokrasia lakini kwangu mimi bado naona kama kuna wingu nene limetanda hapo chamani, ebu tuangalia mambo yafuatayo;
1:KILICHOTOKEA UCHAGUZI KANDA YA NYASA NI DEMOKRASIA WANAYOIHUBIRI???
Ni vyema ikaeleweka kuwa hiki chama kimejipambanua kuupinga utawala wa awamu ya tano kwa kile kinachoitwa "Udikteta" au utawala ambao haufuati demokrasia yawezekana ni kweli au si kweli! Lakini na wao wanajitawala kidemokrasia???
Tuchukulie mfano mathalani kilichotokea Uchaguzi kanda ya nyasa;
1. Wajumbe halali =98
2. Waliosusia =28
3. Waliopiga kura =106
4. Kura za ndio kwa msigwa =62
5. Kura za hapana =44
Maswali tata kutoka kwenye hizo data zetu!!
1. Wajumbe halali ni 98 je hawa waliongezeka wametoka wap? Na nani kawaleta?
2. Ni kwanini P. Ole. Sosopi akatwe siku ya kupiga kura? Is this democracy? Waliomkata wana hofu gani na huyu kijana?
3. Je kuna picha gani gani kama waliomkataa Msigwa ni 44 na waliosusa ni 28 ambao jumla yao ni 72?? Wakati msigwa jumla ana kura 62!!!
4. Ni vigezo vipi vimetumika kumkata P. Ole. Sosopi?? Na vigezo vipi vimetumika kumhalalisha P. Msigwa??
5. Ni Nani aliyemkata P. Ole. Sospi?
6. Je uchaguzi ulikuwa wa huru na haki? Wasimamizi wa uchaguzi ni akina nani? Na wanapatikaneje hawa wasimamizi wa uchaguzi?
7. Je ni kwanini hakuna kuhoji matokeo ya uchaguzi ndani ya chama kutokana na katiba ya chama? Hamuoni aibu mnataka kuhoji uchaguzi wa rais kama nyie wenyewe matokeo ya ndani ya chama hakuna kuhoji?
maswali yangu yameishia hapo lakini naomba tujikumbushe yafuatayo;
:UCHAGUZI VITI MAALUM CHADEMA:
Ni vyema tujikumbushe kwenye huo huo ukanda kulitokea uchafu na kuhalalishwa na makao makuu kwenye uteuzi wa viti maalum wengine walioteuliwa hawajulikani ata kwenye uongozi wa wilaya, mkoa na ata kanda lakini makao makuu yakabariki tuuh.
Majina yalikuwa mageni kabsaa kwenye uongozi wa wilaya na mkoa kwa sababu Mkoa wenyewe walituma jina makao makuu lakini cha ajabu na cha kusikitisha Mtu anayepewa Ubunge wa viti maalum siyo Mwenyeji wa huo mkoa bila kutolea ufafanuzi ata kidogo! Je hii ndo demokrasia wanayoitaka chadema?
:KURA ZA MAONI UBUNGE:
Hapa kulikuwa na manung'uniko mengi na yenye ushaidi wa kutosha kuwa baadhi ya majina yalitoka moja kwa moja kwa Mwenyekiti wa chama ikikuwa awe ameshinda au hajashinda ni lazima atangazwe? Is this people's power?
Wengine walipitishwa kwa rushwa, na hili mhe. SUGU angalau aliifiksha makao makuu na kuweka ushaidi lakini cha kushangaza mpaka leo hakuna ufafanuzi wowote uliotolewa Makao Makuu wameufyata kama vile hawajui kilichotokea.
: HAKUNA TAASISI AU WATU KUHOJI UHARAMIA HUU: JE HII NI DEMOKRASIA??
I mean taasisi za ndani ya chama like BAVICHA & BAWACHA sijawahi sikia wakihoji uharamia wowote ndani ya chama! Kuna nini nyuma ya pazia?? Au ata personal feeling itokee basi iwe individual! Hamna niliyesikia akihoji uharamia lakini kuna watu wamejitolea kufa na kupona kwenye chama hiki tusiwakatishe tamaaa.
Yangu ni hayo tuuh kwa leo.
Ni wako kijana mtiifu, mzalendo na Mwanaharakati wa kweli TZ.