Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,975
- 2,755
Wanajamii mie nashindwa kuelewa inakuwaje huku serikalini wafanyakazi wanaopewa Safari na Masurufu/posho ni wale wale tu kila siku. kuna safari ambazo ni technical kwa wenye fani fulani kuhudhuria semina au workshop nje ya kituo cha kazi hizo sina neno nazo. ila kuna zile ambazo kila mfanyakazi anaweza kufanya akitumwa lakini wakuu wamejenga mazoea kwa watu fulani kwa kuwa ni ndugu zao, wapenzi na marafiki waende wajiongezee kipato nje ya mshahara au kuosha macho. miaka inapita mfanyakazi ana miaka 30 kazini hajawahi hata kutumwa hapo kunduchi beach hotel akajipatia naye posho. kuna waliojenga na kununua magari kwa fedha ya safari wakati wengine wamejikatia tamaa ya kufanya kazi kwa sababu hawakumbukwi na wakubwa. pesa ya PIF ya mwaka 2004 wapo waliogawana mamilioni wengine wakaishia kupewa kozi ya siku 4 kwa gharama ya elfu kumi kila siku ikaisha. Pesa ya mafunzo ya UKIMWI kazini wamegawana wakubwa na kadhalika. naomba mniambie sisi tutatumwa lini nje ya kituo cha kazi na sisi tujue perdiem ya mfanyakazi ni shilingi ngapi. safari za majuu ndio usiseme hata kwa wasiostahili semina hizo hupelekwa tuu ili kuendeleza nepotism na loyality!