Safari kuelekea uhuru wa Tanganyika: Nani anawakumbuka hawa?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,913
30,255
Ilikuwa nyumbani kwa Hamza Mwapachu miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1953.

Abdul Sykes akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika alikwenda Nansio, Ukerewe kupata kauli ya mwisho ya Hamza kuhusu Julius Nyerere.

Abdul Sykes alitaka kupata kauli ya Hamza Mwapachu kuwa Julius Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa juu wa TAA achaguliwe kuwa rais na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hamza Mwapachu aliagiza kuwa Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa TAA kama rais na mwaka 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

1575883956304.png

Kulia Abdulwahid Sykes na Hamza Mwapachu

1575881824659.png

Ukumbi wa Arnautoglo ulipofanyika uchaguzi wa TAA tarehe 17 April 1953 ambako Nyerere na Abdul Sykes waligombea nafasi ya urais na Nyerere akashinda uchaguzi na kuwa Rais wa TAA na Abdu Sykes Makamu wa Rais

1575882048241.png

Waasisi wa TANU mwaka wa 1954

1575882147712.png

Baraza la Wazee wa TANU 1954

1575881366271.png

Safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO February 1955
Wanachama wa mwanzo wa TANU wakimsindikiza Mwalimu Nyerere uwanja wa ndege.
Kulia ni Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, kushoto wa kwanza Bi. Tatu bint Mzee


1575882456983.png

Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO
Kushoto Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo Mratibu wa safari wa Mwalimu Nyerere na Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed


1575882902317.png

Kulia Ali Msham inaaminika ni katika wazalendo wa mwanzo kufungua tawi la TANU nyumbani kwake Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu mwaka wa 1954/55 picha hii inamuonyesha akiwa kwenye tawi hilo la TANU siku alipomkaribisha Julius Nyerere tawini kumkabidhi samani kwa ajili ya ofisi kuu ya TANU New Street

1575883318125.png

Uhuru Kamili 1961
Kulia ni Sheikh Issa Nasir wa Bagamoyo na pembeni yake ni Bi. Mgaya Nyang'ombe mama ya Julius Nyerere, nyuma yao ni Oscar Kambona na upande wa kulia wa Nyerere ni Rajab Diwani

Picha hizi ni chache na majina ya wazalendo waliomo katika picha hizi ni machache pia halikadhalika picha hizi haziwezi kuonyesha yale makubwa ambayo wazalendo hawa walifanya katika kuijenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Lakini ni nani anawajua wazalendo hawa na yale waliyofanya kuikomboa Tanganyika kutoka makucha ya ukoloni?
 
Mzee said wallah allah ni shahidi ni swala la muda tu Acha yatatimia haqq hua haipotei abadani, naomba kujua huyu hamza mwapachu alikua kabila gani, pia nimefurahi kuona watu wa pwani tulikuwa na mchango mkubwa sn wa harakati za uhuru japo leo hii tunadharaurika
 
Siku zote nilikuwa nadhania Sykes ni Mzungu sijui kwa nini, hilo jina nimelisikia muda mrefu sana, kumbe siyo.
 
Siku zote nilikuwa nadhania Sykes ni Mzungu sijui kwa nini, hilo jina nimelisikia muda mrefu sana, kumbe siyo.
Barbarosa,
Sykes Mbuwane alikuwa askari mamluki katika jeshi la Wajerumani aliyekuja Tanganyika na Herman von Wissman ndani ya kundi la askari Wazulu 400 kuja kuwasaidia Wajerumani vita dhidi ya Abushiri bin Salim Al Harith na Mtwa Mkwawa.

Wajerumani walikuwa askari akipata mtoto wanamsajili na kumpa jina.

Kulikuwa na Kleist Sykes, Schneider, Thomas nk.

Lakini wazazi wao pia na wao waliwapa watoto wao majina ya Kiislam.

Kleist jina lake Abdallah na Schneider ni Abdillah.
 
Kama kawaida unaegemea katika udini! Sijui lini utajisahihisha Mohamed Said ili upime mizani na historia ya uhuru ambayo wakristo na Wasio na dini walikuwa wengi sana
 
Kama kawaida unaegemea katika udini! Sijui lini utajisahihisha Mohamed Said ili upime mizani na historia ya uhuru ambayo wakristo na Wasio na dini walikuwa wengi sana
Njinjo,
Unaona Waislam katika historia ya uhuru wa Tanganyika na hili linakutaabisha.

Unamuona Ali Mwinyi Tambwe na Iddi Faiz Mafungo viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika harakati za uhuru hii inakutia simanzi.

Sasa niandikaje historia za hawa wazalendo ilhali hii ndiyo historia yao?

Hebu nielekeze nipate kujua.

Nimefanya utafiti wa kutosha katika viongozi wa harakati za uhuru sikupata kukutana na wapagani ikiwa wapo nifahamishe.

Lakini masheikh nimekutananao wengi kupita kiasi.

Ikiwa unakerwa na historia hii basi ni bahati mbaya sana kwako.

Anajisahihisha yule aliyekosea mimi nijisahihishe kitu gani?

Niogope kuwataja wazalendo waliopigania uhuru kwa kuwa ni Waislam?

Wewe unadhani hiyo ni haki?
 
Nyerere aliingia TAA baada ya kushinda uchaguzi , alimshinda Abdul Sykes kwa kura nyingi, ina maana huu uchaguzi hauutambui ? bila huu uchaguz huyo Mwapachu angeweza kumuingiza kwenye uongozi?
 
Njinjo,
Unaona Waislam katika historia ya uhuru wa Tanganyika na hili linakutaabisha.

Unamuona Ali Mwinyi Tambwe na Iddi Faiz Mafungo viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika katika harakati za uhuru hii inakutia simanzi.

Sasa niandikaje historia za hawa wazalendo ilhali hii ndiyo historia yao?

Hebu nielekeze nipate kujua.

Nimefanya utafiti wa kutosha katika viongozi wa harakati za uhuru sikupata kukutana na wapagani ikiwa wapo nifahamishe.

Lakini masheikh nimekutananao wengi kupita kiasi.

Ikiwa unakerwa na historia hii basi ni bahati mbaya sana kwako.

Anajisahihisha yule aliyekosea mimi nijisahihishe kitu gani?

Niogope kuwataja wazalendo waliopigania uhuru kwa kuwa ni Waislam?

Wewe unadhani hiyo ni haki?
Wewe hukupaswa kuwataja hao wapigania uhuru kwa kuangalia Uislamu wao, mbona hakuna mtu aliemtaja Mwalimu Nyerere na Ukristo wake, sisi tunajua hao ni wapigania Uhuru wetu kwa Utaifa wao, jirekebishe Mkuu.
 
Wewe hukupaswa kuwataja hao wapigania uhuru kwa kuangalia Uislamu wao, mbona hakuna mtu aliemtaja Mwalimu Nyerere na Ukristo wake, sisi tunajua hao ni wapigania Uhuru wetu kwa Utaifa wao, jirekebishe Mkuu.
Coaster...
Labda nikufahamishe kitu kuwa hao wote niliowataja hawako katika historia rasmi ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Hutowasoma popote wala picha hizi hazikuwapo.

Historia zao mmekuja kuzijua hivi sasa baada ya mimi kuandika historia zao na kuweka picha zao.

Labda tena nikuulize kwa nini unadhani ilikuwa hivi?

Iddi Faiz Mafungo alikuwa Mwekahazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na sifa hii ya uwezo wake wa kutunza fedha ndiyo uliomfanya pia akabidhiwe hazina ya TANU kama mtunza fedha.

Kwa nini haya yakukasirishe nikiyaeleza?
Ati nimeangalia Uislam wao.

Ali Mwinyi Tambwe alikuwa kiongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Abdul Sykes baba yake ndiye aliyeasisi chama hicho mwaka wa 1933.

Kweli nimeangalia hizi harakati zilivyokuwa maana hapa kuna maswali mengi ya kujiuliza.

Kama wewe unafanya utafiti na haya ndiyo unayokutananayo lazima utajiuliza maswali.

Kwa nini ilikuwa hivi?

Utajiuliza pia sasa mbona historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika wazalendo hawa wamefutwa?

Kulikoni?

Wa kujirekebisha ni wewe unayetaabishwa na ukweli wa historia hii si mimi ninaekusomesheni historia hii ambayo kwa bahati nzuri ni historia ya wazee wangu.

Mtu hafundishwi historia ya kwao na wageni.
 
Coaster...
Labda nikufahamishe kitu kuwa hao wote niliowataja hawako katika historia rasmi ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Hutowasoma popote wala picha hizi hazikuwapo.

Historia zao mmekuja kuzijua hivi sasa baada ya mimi kuandika historia zao na kuweka picha zao.

Labda tena nikuulize kwa nini unadhani ilikuwa hivi?

Iddi Faiz Mafungo alikuwa Mwekahazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na sifa hii ya uwezo wake wa kutunza fedha ndiyo uliomfanya pia akabidhiwe hazina ya TANU kama mtunza fedha.

Kwa nini haya yakukasirishe nikiyaeleza?
Ati nimeangalia Uislam wao.

Ali Mwinyi Tambwe alikuwa kiongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Abdul Sykes baba yake ndiye aliyeasisi chama hicho mwaka wa 1933.

Kweli nimeangalia hizi harakati zilivyokuwa maana hapa kuna maswali mengi ya kujiuliza.

Kama wewe unafanya utafiti na haya ndiyo unayokutananayo lazima urajiuliza maswali.

Kwa nini ilikuwa hivi?

Utajiuliza pia sasa mbona historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika wazalendo hawa wamefutwa?

Kulikoni?
Aaaah, kumbe wewe unapigania kujua kwa nini hawakutajwa sio ??
 
Sajosojo,
Hakika historia ya Mwalimu Nyerere ni historia ya pekee katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Na hakika wazee wangu walikuwapo wakimsindikiza katika safari hii ya kupigania uhuru wa nchi yetu.

Na kwa hakika kabisa wao ndiyo waliompokea Dar es Salaam na wao ndiyo walioridhia katika kipindi kile kigumu alipopewa uchaguzi na muajiri wake ama achague ualimu au siasa.

Na hii ilikuwa baada ya yeye kurudi UNO mwaka wa 1955 safari iliyosimamiwa na Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir na mratibu wa safari na mkusanyaji fedha za safari akiwa Iddi Faiz Mafungo.

Na kwa hakika isiyo shaka siku alipowasilisha barua aliyoandikiwa muajiri wake aliiwasilisha katika Kamati Kuu ya TANU na mmoja kati ya wajumbe alikuwa Bi. Tatu bint Mzee nyumba yake ilikuwa nyuma ya mtaa wetu.

Hawa wazee wangu ndiyo waliomshauri aache kazi na Mwalimu akaacha kazi na akaja kuishi nyumbani kwa Abdulwahid Sykes.

Kwao Abdul Sykes toka wako Mtaa wa Kipata ndipo ilipokuwa ngome ya harakati za Waafrika toka miaka ya 1920s.

Nyerere kwenda kuishi nyumba ile ulikuwa mkakati mzuri wa kumtambulisha kwa umma wakati sasa TANU inapambana waziwazi na Waingereza.

Mimi natafakhari kuwa wazee wangu walikuwa wazalendo wa kweli na wapigania uhuru wakiwa na Baba wa Taifa siku zote miaka yote hadi uhuru ukapatikana.

Inashangaza kuwa wewe unakasirishwa na historia hii na inakuchukiza kama vile hupendezewi na ule udugu na mapenzi waliojenga wazee wangu kwa Julius Nyerere na juhudi hizi za ukombozi.

Baya zaidi unakuwa sawa na mwizi wa fadhila mtu asiyethamini utu na ihsani baina ya watu.
 
Ilikuwa nyumbani kwa Hamza Mwapachu miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1953.

Abdul Sykes akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika alikwenda Nansio, Ukerewe kupata kauli ya mwisho ya Hamza kuhusu Julius Nyerere.

Abdul Sykes alitaka kupata kauli ya Hamza Mwapachu kuwa Julius Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa juu wa TAA achaguliwe kuwa rais na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.

Hamza Mwapachu aliagiza kuwa Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa TAA kama rais na mwaka 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

View attachment 1286371
Kulia Abdulwahid Sykes na Hamza Mwapachu

View attachment 1286304
Ukumbi wa Arnautoglo ulipofanyika uchaguzi wa TAA tarehe 17 April 1953 ambako Nyerere na Abdul Sykes waligombea nafasi ya urais na Nyerere akashinda uchaguzi na kuwa Rais wa TAA na Abdu Sykes Makamu wa Rais

View attachment 1286311
Waasisi wa TANU mwaka wa 1954

View attachment 1286316
Baraza la Wazee wa TANU 1954

View attachment 1286283
Safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO February 1955
Wanachama wa mwanzo wa TANU wakimsindikiza Mwalimu Nyerere uwanja wa ndege.
Kulia ni Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, kushoto wa kwanza Bi. Tatu bint Mzee


View attachment 1286326
Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO
Kushoto Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo Mratibu wa safari wa Mwalimu Nyerere na Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed


View attachment 1286341
Kulia Ali Msham inaaminika ni katika wazalendo wa mwanzo kufungua tawi la TANU nyumbani kwake Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu mwaka wa 1954/55 picha hii inamuonyesha akiwa kwenye tawi hilo la TANU siku alipomkaribisha Julius Nyerere tawini kumkabidhi samani kwa ajili ya ofisi kuu ya TANU New Street

View attachment 1286351
Uhuru Kamili 1961
Kulia ni Sheikh Issa Nasir wa Bagamoyo na pembeni yake ni Bi. Mgaya Nyang'ombe mama ya Julius Nyerere, nyuma yao ni Oscar Kambona na upande wa kulia wa Nyerere ni Rajab Diwani

Picha hizi ni chache na majina ya wazalendo waliomo katika picha hizi ni machache pia halikadhalika picha hizi haziwezi kuonyesha yale makubwa ambayo wazalendo hawa walifanya katika kuijenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Lakini ni nani anawajua wazalendo hawa na yale waliyofanya kuikomboa Tanganyika kutoka makucha ya ukoloni?
Mwalimu Mzee Said hizi picha zinanipa Amani sana kuona waasisi wa Uhuru wetu ni Wavaa kanzu kofia na Mabaibui. Masha Allah tabarakallah.

Sasa utaona makafiri wasio na elimu roho zinawauma vibaya kuona vijana wa Madrasa walivyoenea kwenye Picha hizi.

Mungu awalaze pema wote waliotangulia mbele ya Haki. Na awalipe Kheri nyingi huko waliko kwa amali zao njema walizofanya.

Amin
 
Mwalimu Mzee Said hizi picha zinanipa Amani sana kuona waasisi wa Uhuru wetu ni Wavaa kanzu kofia na Mabaibui. Masha Allah tabarakallah.

Sasa utaona makafiri wasio na elimu roho zinawauma vibaya kuona vijana wa Madrasa walivyoenea kwenye Picha hizi.

Mungu awalaze pema wote waliotangulia mbele ya Haki. Na awalipe Kheri nyingi huko waliko kwa amali zao njema walizofanya.

Amin
Kahtaan,
Amin.

Hapa ndipo lilipo tatitzo kubwa katika kuandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Idara ya Historia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam wasomi waliopo hakuna aliyekuwa na ujasiri wa kutafiti historia hii kwa sababu zilizokuwa wazi lau Mutahaba alitafiti historia ya Ali Migeyo na kuandika kitabu, "The Portrait of a Nationalist."

Watafiti kutoka nje walikuwa wananyimwa kibali ikiwa itajulikana kuwa wanataka kufanya utafiti juu ya Uislam.

Hii ndiyo sababu kwa miaka mingi hakuna mtafiti aliyetupia jicho historia hii.

Hadi leo unaona hapa majlis kuna wachangiaji wanaghadhibika ninapotoa darsa ya jinsi mambo yalivyokuwa hadi uhuru ukapatikana.

Historia hii hawaijui lakini hatokei mtu akauliza maswali kudadisi kutaka kujua zaidi akija kuchangia anaingia keshapandisha hasira anatamani kama historia hii isifundishwe watu wakaijua.

Bahati hii ni historia ya wazee wangu na ikiwa nitakaa kukueleza wewe historia hata ya shangazi yangu Mama Asha yeye aliolewa nyumba inayotazamana na nyumba ya Bi. Mruguru bint Mussa (mama yake Abdul Sykes)nitafika mahali nitakueleza kuwa alikuwa akiniambia, "Mimi nikimuona Nyerere akija na kaka Abdul kwa Bi. Mruguru Kirk Street wakati huo mambo ya kudai uhuru yamepamba moto."

Akiendelea atakupa stori nyingi za Mzee Ali Jumbe Kiro hawa walikuwa ndiyo viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na wanaharakati wa TANU.

Hii ndiyo historia yetu hatuwezi kukubali kuona inafutwa ati kwa hofu ya kuwataja Waislam katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
 
Back
Top Bottom