Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,913
- 30,255
Ilikuwa nyumbani kwa Hamza Mwapachu miezi ya mwanzo ya mwaka wa 1953.
Abdul Sykes akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika alikwenda Nansio, Ukerewe kupata kauli ya mwisho ya Hamza kuhusu Julius Nyerere.
Abdul Sykes alitaka kupata kauli ya Hamza Mwapachu kuwa Julius Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa juu wa TAA achaguliwe kuwa rais na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.
Hamza Mwapachu aliagiza kuwa Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa TAA kama rais na mwaka 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.
Kulia Abdulwahid Sykes na Hamza Mwapachu
Ukumbi wa Arnautoglo ulipofanyika uchaguzi wa TAA tarehe 17 April 1953 ambako Nyerere na Abdul Sykes waligombea nafasi ya urais na Nyerere akashinda uchaguzi na kuwa Rais wa TAA na Abdu Sykes Makamu wa Rais
Waasisi wa TANU mwaka wa 1954
Baraza la Wazee wa TANU 1954
Safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO February 1955
Wanachama wa mwanzo wa TANU wakimsindikiza Mwalimu Nyerere uwanja wa ndege.
Kulia ni Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, kushoto wa kwanza Bi. Tatu bint Mzee
Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO
Kushoto Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo Mratibu wa safari wa Mwalimu Nyerere na Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed
Kulia Ali Msham inaaminika ni katika wazalendo wa mwanzo kufungua tawi la TANU nyumbani kwake Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu mwaka wa 1954/55 picha hii inamuonyesha akiwa kwenye tawi hilo la TANU siku alipomkaribisha Julius Nyerere tawini kumkabidhi samani kwa ajili ya ofisi kuu ya TANU New Street
Uhuru Kamili 1961
Kulia ni Sheikh Issa Nasir wa Bagamoyo na pembeni yake ni Bi. Mgaya Nyang'ombe mama ya Julius Nyerere, nyuma yao ni Oscar Kambona na upande wa kulia wa Nyerere ni Rajab Diwani
Picha hizi ni chache na majina ya wazalendo waliomo katika picha hizi ni machache pia halikadhalika picha hizi haziwezi kuonyesha yale makubwa ambayo wazalendo hawa walifanya katika kuijenga TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.
Lakini ni nani anawajua wazalendo hawa na yale waliyofanya kuikomboa Tanganyika kutoka makucha ya ukoloni?
Abdul Sykes akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika alikwenda Nansio, Ukerewe kupata kauli ya mwisho ya Hamza kuhusu Julius Nyerere.
Abdul Sykes alitaka kupata kauli ya Hamza Mwapachu kuwa Julius Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa juu wa TAA achaguliwe kuwa rais na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru wa Tanganyika.
Hamza Mwapachu aliagiza kuwa Nyerere aingizwe kwenye uongozi wa TAA kama rais na mwaka 1954 TANU iundwe na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.
Kulia Abdulwahid Sykes na Hamza Mwapachu
Ukumbi wa Arnautoglo ulipofanyika uchaguzi wa TAA tarehe 17 April 1953 ambako Nyerere na Abdul Sykes waligombea nafasi ya urais na Nyerere akashinda uchaguzi na kuwa Rais wa TAA na Abdu Sykes Makamu wa Rais
Waasisi wa TANU mwaka wa 1954
Baraza la Wazee wa TANU 1954
Safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO February 1955
Wanachama wa mwanzo wa TANU wakimsindikiza Mwalimu Nyerere uwanja wa ndege.
Kulia ni Bi. Chiku bint Said Kisusa, Bi. Titi Mohamed, kushoto wa kwanza Bi. Tatu bint Mzee
Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO
Kushoto Rashid Sisso, Robert Makange, Zuberi Mtemvu, Iddi Faiz Mafungo Mratibu wa safari wa Mwalimu Nyerere na Mweka Hazina wa TANU na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika, Julius Nyerere, John Rupia na Bi. Titi Mohamed
Kulia Ali Msham inaaminika ni katika wazalendo wa mwanzo kufungua tawi la TANU nyumbani kwake Magomeni Mapipa Mtaa wa Jaribu mwaka wa 1954/55 picha hii inamuonyesha akiwa kwenye tawi hilo la TANU siku alipomkaribisha Julius Nyerere tawini kumkabidhi samani kwa ajili ya ofisi kuu ya TANU New Street
Uhuru Kamili 1961
Kulia ni Sheikh Issa Nasir wa Bagamoyo na pembeni yake ni Bi. Mgaya Nyang'ombe mama ya Julius Nyerere, nyuma yao ni Oscar Kambona na upande wa kulia wa Nyerere ni Rajab Diwani
Lakini ni nani anawajua wazalendo hawa na yale waliyofanya kuikomboa Tanganyika kutoka makucha ya ukoloni?