SADC wakubaliana kupeleka wanajeshi kukabiliana na ugaidi Msumbiji

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika siku ya Jumatano umeazimia kupeleka wanajeshi nchini Msumbiji kukabiliana na kitisho cha usalama katika jimbo la Kaskazini la Cabo Delgado.

Hatua ya SADC inakuja baada ya vifo vya zaidi ya watu 3,000 huku wengine takriban 800,000, wengi wao wakiwa watoto, kulazimika kukimbia makazi yao tangu kuanza kwa machafuko mwaka 2017.

Baada ya Mkutano wa siku moja uliofanyika katika jijini Maputo, Katibu Mkuu wa SADC, Stergomena Tax amesema nchi 16 zimekubaliana kupeleka wanajeshi bila kutaja idadi ya wanajeshi watakaopelekwa, siku watakayopelekwa na majukumu watakayotekeleza, akibainisha kuwa lazima misaada ya kibinadamu iwafikie wale walio na uhitaji.

Makubaliano ya SADC yanamaliza mgogoro wa miezi kadhaa kuhusu hatua inayotakiwa kuchukuliwa kumaliza mgogoro, baadhi ya nchi wanachama kama Afrika Kusini wakitaka hatua za kijeshi huku wengine, akiwamo Rais Philipe Nyusi wa Msumbiji akipinga wanajeshi wa kigeni nchini kwake.

Mashambulizi ya magaidi wanaojiita al-Shabab yameongezeka siku za hivi karibuni, wakitajwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi duniani la ISIL. Serikali ya Msumbiji imepeleka maelfu ya wanajeshi katika eneo hilo, lakini wachambuzi wameonya udhaifu wa jeshi la nchi hiyo katika mafunzo na vifaa.

Chanzo: Al Jazeera

1624515799578.png
 
Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika siku ya Jumatano umeazimia kupeleka wanajeshi nchini Msumbiji kukabiliana na kitisho cha usalama katika jimbo la Kaskazini la Cabo Delgado.

Hatua ya SADC inakuja baada ya vifo vya zaidi ya watu 3,000 huku wengine takriban 800,000, wengi wao wakiwa watoto, kulazimika kukimbia makazi yao tangu kuanza kwa machafuko mwaka 2017.

Baada ya Mkutano wa siku moja uliofanyika katika jijini Maputo, Katibu Mkuu wa SADC, Stergomena Tax amesema nchi 16 zimekubaliana kupeleka wanajeshi bila kutaja idadi ya wanajeshi watakaopelekwa, siku watakayopelekwa na majukumu watakayotekeleza, akibainisha kuwa lazima misaada ya kibinadamu iwafikie wale walio na uhitaji.

Makubaliano ya SADC yanamaliza mgogoro wa miezi kadhaa kuhusu hatua inayotakiwa kuchukuliwa kumaliza mgogoro, baadhi ya nchi wanachama kama Afrika Kusini wakitaka hatua za kijeshi huku wengine, akiwamo Rais Philipe Nyusi wa Msumbiji akipinga wanajeshi wa kigeni nchini kwake.

Mashambulizi ya magaidi wanaojiita al-Shabab yameongezeka siku za hivi karibuni, wakitajwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi duniani la ISIL. Serikali ya Msumbiji imepeleka maelfu ya wanajeshi katika eneo hilo, lakini wachambuzi wameonya udhaifu wa jeshi la nchi hiyo katika mafunzo na vifaa.

Chanzo: Al Jazeera

Haita saidia kitu kupeleka majeshi msumbiji bila kwanza kumsaka mfa
dhili wa hawa magaidi ya ISS, Boko haram na Answa surat(mali). Huyo Huyo mfadhili anapiganisha vita kule mali, Somalia na sasa kawapeleka msumbiji.Kuna taifa kubwa huko mashariki ya kati linalowapa afya hawa magaidi kueneza sharia law na kuteka himaya kubwa za kidini. SADC kwa nini hawamsaki huyo mfadhili? hawa magaidi kupewa siraha,hela za kujenga makazi yao, hela za petroli, chakula na mavazi hawawezi bila kufadhiliwa. Huyo huyo mfadhili anawapa afya chafu BOKO haram.

hata ukitumia akiri za kichanga, Boko haram, Al shabab na ISS hawawezi kujilipia gharama zote hizo za kusafili na kula bila pesa kutola kwa hilo taifa. sasa AU, EAC na SADC lazima waombe msaada wa kulikabili taifa hilo la sivyo jitiohada zao zitaishia kuwa za kitoto.
 
Haita saidia kitu kupeleka majeshi msumbiji bila kwanza kumsaka mfa
dhili wa hawa magaidi ya ISS, Boko haram na Answa surat(mali). Huyo Huyo mfadhili anapiganisha vita kule mali, Somalia na sasa kawapeleka msumbiji.Kuna taifa kubwa huko mashariki ya kati linalowapa afya hawa magaidi kueneza sharia law na kuteka himaya kubwa za kidini. SADC kwa nini hawamsaki huyo mfadhili? hawa magaidi kupewa siraha,hela za kujenga makazi yao, hela za petroli, chakula na mavazi hawawezi bila kufadhiliwa. Huyo huyo mfadhili anawapa afya chafu BOKO haram.

hata ukitumia akiri za kichanga, Boko haram, Al shabab na ISS hawawezi kujilipia gharama zote hizo za kusafili na kula bila pesa kutola kwa hilo taifa. sasa AU, EAC na SADC lazima waombe msaada wa kulikabili taifa hilo la sivyo jitiohada zao zitaishia kuwa za kitoto.
Kwa iyo hata hao wafadhili wanawafundisha mafunzo ya Quran na hadithi??

Hopeless and Pathetic!
 
Haita saidia kitu kupeleka majeshi msumbiji bila kwanza kumsaka mfa
dhili wa hawa magaidi ya ISS, Boko haram na Answa surat(mali). Huyo Huyo mfadhili anapiganisha vita kule mali, Somalia na sasa kawapeleka msumbiji.Kuna taifa kubwa huko mashariki ya kati linalowapa afya hawa magaidi kueneza sharia law na kuteka himaya kubwa za kidini. SADC kwa nini hawamsaki huyo mfadhili? hawa magaidi kupewa siraha,hela za kujenga makazi yao, hela za petroli, chakula na mavazi hawawezi bila kufadhiliwa. Huyo huyo mfadhili anawapa afya chafu BOKO haram.

hata ukitumia akiri za kichanga, Boko haram, Al shabab na ISS hawawezi kujilipia gharama zote hizo za kusafili na kula bila pesa kutola kwa hilo taifa. sasa AU, EAC na SADC lazima waombe msaada wa kulikabili taifa hilo la sivyo jitiohada zao zitaishia kuwa za kitoto.
Technology itakuja maliza huu upumbavu, ngoja watu waachane na petrol, petrol iwe kama mafuta ya TAA yalivyo kwasasaUgaidi utaisha wenyewe.

Mtu ana kitaru cha kuchimba na kuuza mafuta, ana magari kadhaa ya kifahari, ana wake wanne na nyumba kali akaunt imejaa, anajenga miskiti ya kutosha, ana baki kuwa mtu wa kusali muda wote, taratibu anaanaza kujiona yeye ndiyo anaijua dini kuliko wengine.
Muda wote a nasoma AYA za kwenda peponj, Aya zinamwambia aipiganie imani, apambane na makafiri, ikiwa mtume alitolewa JINO kuieneza dini ni vipi wewe usipigane kwasababu ya DINI? .
Kwasababu Wana rasimali pesa na hazina kazi, ndo ujaanza kuona Boko HARAM, ISIS nk, wanapigania nchi iongozwe SHARIA.

Sasa siku petrol hainunuliki kwasababu haihitajiki, ugaidi utaisha,utaisha kwasababu pesa hakuna.
 
Sisi tumeshapeleka wanajeshi wetu huko Msumbiji sana, miaka nenda rudi. Huu ni muda sasa nchi nyingne za SADC nazo zipeleke wanajeshi huko msumbiji.
Tukijipendekeza kupeleka wanajeshi, tujue tu msumbiji ni nchi jirani, hao Magaidi watavuka mpaka na kutuletea tabu kwenye vijiji vyetu.
Halafu Jeshi la Msumbiji litashindwaje kudeal na wanamgambo wachache hao?-Msumbiji waache uvivu, wapigane kama wanaume, waache kujibebisha!

Hivi vikundi huenda kuna mkono wa CIA, Mossad, MI16
Tusiingie kichwakichwa wakatuletea fight ndani mwetu
 
Kama Rais wa nchi anapinga ujio wa Wanajeshi wa kigeni Kuna tatizo hapo, Kuna hatari magaidi kuuziwa mipango yote toka serikali ya Msumbiji.
 
Humo kwenye vidoti vyeusi wamepiga kote na kwenye viduara vikubwa vyeusi wamepiga siku mbili hizi ; kwenye kiduara cha blue ndo mradi ulipo na macamp ya wafanyakazi inamaana mda wwte kuanzia sasa wanawezA kusambaratisha hayo ma camp na ma office na biashara itakuwa imeishia hapo!!
IMG-20210623-WA0004.jpg
 
Haita saidia kitu kupeleka majeshi msumbiji bila kwanza kumsaka mfa
dhili wa hawa magaidi ya ISS, Boko haram na Answa surat(mali). Huyo Huyo mfadhili anapiganisha vita kule mali, Somalia na sasa kawapeleka msumbiji.Kuna taifa kubwa huko mashariki ya kati linalowapa afya hawa magaidi kueneza sharia law na kuteka himaya kubwa za kidini. SADC kwa nini hawamsaki huyo mfadhili? hawa magaidi kupewa siraha,hela za kujenga makazi yao, hela za petroli, chakula na mavazi hawawezi bila kufadhiliwa. Huyo huyo mfadhili anawapa afya chafu BOKO haram.

hata ukitumia akiri za kichanga, Boko haram, Al shabab na ISS hawawezi kujilipia gharama zote hizo za kusafili na kula bila pesa kutola kwa hilo taifa. sasa AU, EAC na SADC lazima waombe msaada wa kulikabili taifa hilo la sivyo jitiohada zao zitaishia kuwa za kitoto.
Kabisa mkuu huu ndo ukweli majamaa wamejipanga na mbaya zaidi wamewachelewa ila huyo nyusi ni ......yeye ndo aloifikisha nchi hapo hikk kikundi kulianza kama mzaha 2017 akazembea sasa wanasilaha zote eti ndo anaomba msaada Total wamekimbia kazi yamebaki magofu tu palma na mcimboa da praia!!wilaya kubwa kabisa zinamilikiwa na Alshababy nyusi atalaumika sana!!
 
Kama Rais wa nchi anapinga ujio wa Wanajeshi wa kigeni Kuna tatizo hapo, Kuna hatari magaidi kuuziwa mipango yote toka serikali ya Msumbiji.
Asante mkuu yyte mwwnye akili timamu lazima atafikilia hivyo mana nyusi kaweka ugumu tangu wanaanza 2017 kupindi,hicho wakitumia mapanga kuchinja watu,vijijini,amewaacha mpka sasa wanamiliki silaha za htr eti ndo aombe msaada watu washakimbia makazi na kupoteza kila kitu wilaya kubwa kubwa zipo mikononi mwao hawa wapumbavu karibia wafanyakazi 15000 wamepoteza ajira zao na makampuni,kibao yameathirika sana mana mpka sasa vifaa,vyao bado vipo kwnye ma site sasa ni vipi wataenda kuvitoa?alshababy washatanda kila kona inasikitisha sana Africa Bara langu!!
 
Haita saidia kitu kupeleka majeshi msumbiji bila kwanza kumsaka mfa
dhili wa hawa magaidi ya ISS, Boko haram na Answa surat(mali). Huyo Huyo mfadhili anapiganisha vita kule mali, Somalia na sasa kawapeleka msumbiji.Kuna taifa kubwa huko mashariki ya kati linalowapa afya hawa magaidi kueneza sharia law na kuteka himaya kubwa za kidini. SADC kwa nini hawamsaki huyo mfadhili? hawa magaidi kupewa siraha,hela za kujenga makazi yao, hela za petroli, chakula na mavazi hawawezi bila kufadhiliwa. Huyo huyo mfadhili anawapa afya chafu BOKO haram.

hata ukitumia akiri za kichanga, Boko haram, Al shabab na ISS hawawezi kujilipia gharama zote hizo za kusafili na kula bila pesa kutola kwa hilo taifa. sasa AU, EAC na SADC lazima waombe msaada wa kulikabili taifa hilo la sivyo jitiohada zao zitaishia kuwa za kitoto.
Usijali mkuu kufika 2040 biashara ya mafuta itakuwa imeshakufa kama so kuisha, makampuni mengi yanayotengeneza injini na vifaa vingine wanahamia kwenye nishati ya umeme na jua na gas kwa mbali! Nadhani Nickel na Lithium zitakuwa ghali sawa na dhahabu!
Waarabu watahaha vibaya mno na huenda ukawa ndo mwisho wa ugaidi
 
Back
Top Bottom