SACP Wambura: Jeshi la Polisi Dar lakamata Majambazi, Wauaji, Wezi wa Magari na Pikipiki, na Uvunjaji

Duh!

Huyu si mtoto mdogo kabisa
Kuna uwezekano huyu walimfundisha kuendesha gari...
Wezi wa magari, huwatumia watoto watundu /wadogo kuiba magari kisha wanawapa direction gati walipeleke wapi..

Case zishawahi tokea huko nyuma
 
Huyo kazi yake anabinjushwa kuingia nyumba za watu,grill ikitanuliwa hyo anatangulizwa ndy wanavyotumika
Kuna wengine wana miaka mpaka 13,14

Ova
Nilishawahi kuibiwa ofcn kwangu,
Yani nyuma ya frem wanatoboa/walitoa tofali moja la 6' ,level ambayo akipenya anakutana na sakafu...

na ninavyosikia lile tofali hali tinduliwi lina mwagiwa kitu so linamomonyoka kiulaini kabisa ...

so kwa mtu mwenye kimwili kidogo au hao madogo wa miaka hiyo ni rahisi kabisa kupenya bila shida...

Walikomba vitu vingi sana..

Mlinzi wa kampuni uchwara yuko mbele analinda milango ya fremu, jamaa wamepenya nyuma wanasomba vitu...
 
Nafikrir polisi gang la Anti robbery watakuwa wana info nyingi kuhusu, hawa wahalifu wanaosumbua..
 
Ukosefu wa ajira kwa vijana ni BOMU linalosubiriwa kulipuka. Mungu aepushie mbali tusije kutengeneza Bokoharam wetu!
Wangapi hawana ajira ila hawaibi,hawapori na hawadhuru watu ?

Huu ujinga ni kujiendekeza tu.

Mwizi kama adui yako tu,usiombe ukutane na adui yako ana kwa ana. Hawa adhabu yao aidha kifo au kuwafanya wasiibe tena,unakata mikono tu,kulingana na makosa yao.

Kuna muda huwa naona hizi mahakama na magereza ni kupoteza mali bure na kupotezea watu muda.
 
Wangapi hawana ajira ila hawaibi,hawapori na hawadhuru watu ?

Huu ujinga ni kujiendekeza tu.

Mwizi kama adui yako tu,usiombe ukutane na adui yako ana kwa ana. Hawa adhabu yao aidha kifo au kuwafanya wasiibe tena,unakata mikono tu,kulingana na makosa yao.

Kuna muda huwa naona hizi mahakama na magereza ni kupoteza mali bure na kupotezea watu muda.
Nigeria nao walikuwa na mentality kama hii... waliona Bokoharam ni vinyangalika fulani tu hivi - mara ikawa BOOOOM!!!
 
Nigeria nao walikuwa na mentality kama hii... waliona Bokoharam ni vinyangalika fulani tu hivi - mara ikawa BOOOOM!!!
Ishu ya Boko Haramu ni tofauti na hii.

Bokoharam ni wajinga fulani wenye kutumia dini kupotosha na kuvamia watu. Na ndiyo maana watu kama Bokoharamu mafikio yao ni mabaya.

Huwezi kuhalalisha ovu kisa umekosa la halali,cha msingi kupambana madamu uko hai na una nguvu.
 
1. Kaburu Mohamed kaburu,(30),Mkazi wa Buza Kanisani.

2. Iddi Ally Kiduku, Miaka 30, Mkazi wa Tandika.

3. Said Ramadhani @Timu, Miaka 33, Mkazi wa Kitunda.

4. Lucas Danford@Udongo wa Maka, Miaka 31, Mkazi wa Buguruni

5. Shaban Bakari@Majani, Miaka 33, Mkazi wa Tandika kaburi moja.

6. Khamis Bahati Chief, Miaka 38, Mkazi wa Buza kwa mama kibonge


Hii imekaaje Wadau?
imekaa ki Jei kei tii by look of it
 
Naunga mkono hoja.
Hii tabia ya kutumia demokrasia kupambana na watu wanao tumia silaha za moto haitofanikiwa kamwe kamwe ni lazima tuwe wawazi hawa watu wanapaswa kuchapwa risasi tuu kama ilivyokuwa kipindi cha Magu..

Hawa wapumbavu kuwakamata kama vile ni wezi wa vijiko ni ujinga na tunao teseka ni wakazi wa dares-salaam yani watu wanavamia hadi suma jk halafu unawakamata kidemokrasi hivi halafu useme uhalifu utakwisha kweli?

Lazima tuseme ukweli dawa ya moto ni moto sasa hivi dar kuna hofu kubwa ya ujambazi na njia ya kuumaliza ni kuwapa taarifa wenzao wameuwawa wakiwa wanapambana na jeshi la polisi.
Hawa wanapaswa kutwanga risasi tuu sio kuleta story za kuwakamata

Enzi za Magu walipokuwa wakitwangwa risasi na wengne miili yao kuokotwa ktk viróba huko beach, Chadema wakaja juu kusema Serikali inadhulumu na kukandamiza haki za Raia,,,, ila Magu akasema moto uendelee

Mwisho matukio yakapungua kwa asilimia kubwa sana

Leo kaja Mamá SSH madarakani,,Chadema wanamuomba atende haki na kudhulumu haki za watu, sasa matokeo yake ndio haya wizi ujambazi vimerudi.
Watuhumiwa wanakamatwa na wataendwa kufikishwa mahakamani na huko ushahidi utakosekana kuwatia hatiani na mwisho watarudi uraiani na mambo yataendelea

WITO kwa Mh Rais, sio kila maeneo ni kuyatolea lugha laini laini au kutaka mambo ya haki na sheria,,, sehemu kama hizi ni kupeleka mkono wa chuma tu mpaka hao Wapuuzi wanyooke
 
Back
Top Bottom