Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,796
- 11,959
Maafisa Habari wa Jeshi la Polisi nchini wametakiwa kuimarisha uhusiano na Waandishi wa habari ili kwa pamoja waweze kuelimisha jamii kuhusu miradi mbalimbali ya Polisi Jamii kwa lengo la kutokomeza uhalifu.
Misime alisema Waandishi wa habari ni wadau muhimu katika kuhabarisha jamii hivyo ni uhusiano utakapoimarika itakuwa chachu ya kuifikia jamii.
Aidha, Misime aliwataka Maafisa hao kufanya kazi kwa weledi na kujikita katika kutoa taarifa zenye tija kwa jamii inayowazunguka.