Zawadi B Lupelo
JF-Expert Member
- Jul 19, 2015
- 2,549
- 3,722
Wanajamvi salaam!
Nimeshangazwa sana kupata habari kwamba tajiri Sabodo aliyekuwa mfadhili wa vyama vya upinzani kwa muda mrefu ametangaza kutokuwafadhili CHADEMA tena na badala yake atamsaidia JPM kuwekeza mkoani Dodoma.
Sina tatizo na Sabodo kuwekeza ama kumsaidia Magufuli la hasha ila nataka niwatahadharishe usanii wa huyu mzee.
Kuna kipindi aliwaahidi CHADEMA kuwajengea chuo cha siasa kwa ajili ya kuandaa viongozi. Chama kilitafuta eneo alipotafutwa Sabodo aliingia mitini hata hela ya upembuzi yakinifu ambayo haizidi bilioni nne za kitanzania hakutoa.
Leo hii mtu kama huyu huwezi kumuamini tena kwa ahadi za matrilioni hata kidogo anatafuta umaarufu wa bei nafuu tu.
Nimeshangazwa sana kupata habari kwamba tajiri Sabodo aliyekuwa mfadhili wa vyama vya upinzani kwa muda mrefu ametangaza kutokuwafadhili CHADEMA tena na badala yake atamsaidia JPM kuwekeza mkoani Dodoma.
Sina tatizo na Sabodo kuwekeza ama kumsaidia Magufuli la hasha ila nataka niwatahadharishe usanii wa huyu mzee.
Kuna kipindi aliwaahidi CHADEMA kuwajengea chuo cha siasa kwa ajili ya kuandaa viongozi. Chama kilitafuta eneo alipotafutwa Sabodo aliingia mitini hata hela ya upembuzi yakinifu ambayo haizidi bilioni nne za kitanzania hakutoa.
Leo hii mtu kama huyu huwezi kumuamini tena kwa ahadi za matrilioni hata kidogo anatafuta umaarufu wa bei nafuu tu.