mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 16,027
- 35,835
Jinga wewe,hao ni majambaziSababu kubwa kwanini hawastahili kushitakiwa ni Katiba yetu inatoa mamlaka kubwa sana kwa taasisi ya Urais ,hivyo kila Rais anateua kulingana na mfumo anaotaka kuongoza.
Awamu iliyopita iliamini ukitakuongoza nchi za Afrika ni lazima ulazimishe watu watii amri, wafanye kazi, na hela iingie serikalini kwa Namna yoyote ile ili Miradi mbali mbali iindelee.
Hivyo Viongozi kama kina Sabaya na Makonda waliteuliwa sababu walikuwa na uwezo wa kusimamia hayo aliyo amini Rais
Vivyo hivyo kwa awamu zilipita kuna wateuliwa /watumishi walikuwepo kwa Ajili ya kutumika na Ofisi hiyo, hata Awamu hii kuna ni hivyo hivyo.
Hivyo tukianza kushitakiana:
1. Taasisi hiyo kuna kipindi itakosa watu wa kuitumikia vyema kila mtu atakuwa muoga.
2. Hizo kesi hazitaisha mahakamani ukianza kushitaki kuanzia Awamu ya Kwanza mpaka sasa ni nyingi sana.
Mwisho sio rahisi kama tunavyo chukulia nadhani ambao wameshawahi kuwa viongozi wanaelewa ugumu ulivyo Wewe una plan hivi kuna baadhi ya watu wanakwamisha juhudi hapo ndio inapokuja shida ya kushughulika na hao watu.
Kikubwa hao vijana walikuwa wanafanya kulingana na mfumo ulikuwa unataka nini labda tushitaki mfumo au Katiba kwa kuiipa Madaraka makubwa hiyo Taasisi.