Sababu zilizomwondoa Rais Goodluck ndizo zitaiondoa CCM

Ngwananzengo

JF-Expert Member
Jul 28, 2012
1,911
1,312
Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Bw. Ole Njorai amesema mambo ya msingi yaliyowafanya Wanigeria kumtosa Rais Goodluck ni

: 1) Ukosefu wa ajira hasa kwa vijana. Katika kila vijana 10 wanaohitimu masomo ya chuo kikuu ni vijana 4 tu wanaopata nafasi ya kuajiriwa.

2)Serikali kwa ujumla wake ilikuwa imejaa rushwa na kwa kiasi kikubwa ilishindwa kupiga vita rushwa.

3) Kuzorota kwa usalama. Sababu hizi zinashabihiana au kurandana kwa kiasi kikubwa na malalamiko ya watanzania wengi juu ya serikali ya CCM.

Kama ni rushwa imetamaraki kiasi cha wala rushwa wakikitisha chama chao "eti" majina yao yakikatwa patajimbika. Suala la Ukosefu wa ajira limekuwa haliwekewi mikakati thabiti ya kuliondoa zaidi ya vijana kushauriwa kufuga nyuki. Usalama wa raia na Mali zao umekuwa uzizorota kila uchwao.

Kila siku ni taarifa za majambazi kupora bunduki za polisi badala ya polisi kukamata majambazi. Ni wakati muafaka wa CCM kujitathimini vinginevyo wataishia kupiga propaganda zisizo na kichwa wala miguu. Ooooohhh Maalim Seif Kaishagombea mara Nyingi, Slaa ni padri.

Akitoa neno baada ya kutangazwa kushinda, Generali mstaafu na Rais mteule Bw. Bohali amesema "wanaijeria wameungana pamoja bila kujali huyu ni yoruba, ibo au vingine".

Ni hakika kwa kuchochwa na matatizo yanayowakabili watanzania wataungana bila kujali tofauti zao.
 
CCM wamelewa madaraka, wanajiona ni mungu watu.

wanapiga propagana za udini na ukabila ili watugawe waendelee kututawala
na baadhi yetu tumeanza kuimba wimbo wa mi-ccm

shoka liko shingoni mwao (oct, 2015)
 
Shoka limeishawekwa tayari kuukata mti usozaa matunda.sikujua kama kifo cha ccm kitakuja haraka kiasi hiki!
 
Sasa kama moja ya tatizo kubwa ni rushwa,iweje leo twataka Edward awe rais, tunalalamminikia rushwa ila tunawataka walarushwa na mafisadi waendeshe nchi
 
Upande wa ccm katika vijana 10 wanaohitim chuo kikuu,0 wanapata ajira.Ile wizara ya ajira sijui iliundwa ilikufanya shughuli gani.serikali kutokuwajali vijana ni sumu.
 
Sasa kama moja ya tatizo kubwa ni rushwa,iweje leo twataka Edward awe rais, tunalalamminikia rushwa ila tunawataka walarushwa na mafisadi waendeshe nchi

Hizo ndo akili za wapiga KURA wengi....wa TANGANYIKA wanaakili za NYUMBU akishapewa Kofia na Sahani ya UBWABWA kwisha
 
Sasa kama moja ya tatizo kubwa ni rushwa,iweje leo twataka Edward awe rais, tunalalamminikia rushwa ila tunawataka walarushwa na mafisadi waendeshe nchi

simple:waendekeza tumbo nchi tupo wengi.....ila kila kitu kina ukomo wake..
 
huu uchaguzi nimefuatilia vizuri sana na bahati nimewaona wanaigeria wakitaka mabadiliko na wakaamumua kuyapigia kura, je watanzania wanaweza..?
 
Basi sawa! Ila navyojua huyo balozi hawezi kutoa hizo kauli as long as ni Pure CCM. Lazima umemchomekea some words ...
Ni kweli kabisa mkuu Balozi Ole Njorai ni CCM ila Nilichonukuu alikitamka jana wakati akihojiwa na Salim Kikeke wa BBC na habari ikarushwa saa tatu usiku.
 
Back
Top Bottom