Syston
JF-Expert Member
- Nov 6, 2017
- 243
- 339
Habari wanajamvi,
Leo ninawasogezea hii ambayo ni sehemu ya uzoefu nilionao katika maisha yangu ya mahusiano.
Mara nyingi imezoeleka na inafahamika hivyo, kwamba wanaume ndio walaghai katika mapenzi na hutongoza wasichana ili kukidhi haja zetu.
Huo sio ukweli, wanaume tulio wengi tunatongoza tukiamini tunaweza kupata wife material, hakuna mwanaume anayetongoza mwanamke anayeonekana ni kicheche. Wanaume tunapenda kuuliza kama mpenzi mpya ana mahusiano na mwanaume mwingine mapema kabisa siku za mahusiano, majibu ya wanawake huwa ni, "Ningekuwa na mtu ningekukubali wewe?" Akiwa mstaarabu atakwambia alikuwa nae na waliachana siku,miezi au miaka kadhaa nyuma.
Hapo mwanaume unaingia mzima mzima ukiamini umepata mwenza ila cha kusikitisha miezi kadhaa badae unagundua ana uhusiano na mtu au watu wengine na ukifuatilia (binafsi huwa namtafuta jamaa nakaa nae chini namsilikiza mwanzo mwisho, sina tabia ya kupanic) unagundua ni mahusiano yaliyokuwapo kabla hajawa na wewe na wala hawajawaji kuachana na ushahidi unakuwa wazi kabisa na mwanamke anakosa cha kusema na kujikuta anaomba msamaha. Hapa mwanaume anaetaka wife material hawezi kukuelewa labda akugeuze Cocacola Baridi.
Katika hali hiyo mwanaume huamua kuachana na mwanamke wa namna hiyo ila cha ajabu mwanamke ndo huwa wa kwanza kumtangaza mwanaume kuwa kampotezea muda na kamchezea, kamtumia kamchoka kamuacha. Wanaume tumeumbwa mateso ila sio na kwenye mapenzi jamani mtuhurumie kesi zenu zingine mzikubali tu. Wanawake ndio mnachezea wanaume.
Leo ninawasogezea hii ambayo ni sehemu ya uzoefu nilionao katika maisha yangu ya mahusiano.
Mara nyingi imezoeleka na inafahamika hivyo, kwamba wanaume ndio walaghai katika mapenzi na hutongoza wasichana ili kukidhi haja zetu.
Huo sio ukweli, wanaume tulio wengi tunatongoza tukiamini tunaweza kupata wife material, hakuna mwanaume anayetongoza mwanamke anayeonekana ni kicheche. Wanaume tunapenda kuuliza kama mpenzi mpya ana mahusiano na mwanaume mwingine mapema kabisa siku za mahusiano, majibu ya wanawake huwa ni, "Ningekuwa na mtu ningekukubali wewe?" Akiwa mstaarabu atakwambia alikuwa nae na waliachana siku,miezi au miaka kadhaa nyuma.
Hapo mwanaume unaingia mzima mzima ukiamini umepata mwenza ila cha kusikitisha miezi kadhaa badae unagundua ana uhusiano na mtu au watu wengine na ukifuatilia (binafsi huwa namtafuta jamaa nakaa nae chini namsilikiza mwanzo mwisho, sina tabia ya kupanic) unagundua ni mahusiano yaliyokuwapo kabla hajawa na wewe na wala hawajawaji kuachana na ushahidi unakuwa wazi kabisa na mwanamke anakosa cha kusema na kujikuta anaomba msamaha. Hapa mwanaume anaetaka wife material hawezi kukuelewa labda akugeuze Cocacola Baridi.
Katika hali hiyo mwanaume huamua kuachana na mwanamke wa namna hiyo ila cha ajabu mwanamke ndo huwa wa kwanza kumtangaza mwanaume kuwa kampotezea muda na kamchezea, kamtumia kamchoka kamuacha. Wanaume tumeumbwa mateso ila sio na kwenye mapenzi jamani mtuhurumie kesi zenu zingine mzikubali tu. Wanawake ndio mnachezea wanaume.