Sababu za wananchi kukosa matumaini ya mabadiliko kwenye utendaji wa haki chini ya Rais Samia

M-mbabe

JF-Expert Member
Oct 29, 2009
13,203
23,020
I) POSITIVES
Tangu ameingia madarakani, tumeona mabadiliko kidogo sana yenye mwelekeo chanya. Nimetumia expression ya "kidogo sana" kwa vile si mambo yaliyohitaji kutumia effort kubwa sana kuyatekeleza bali yanahitaji self-restraint pamoja na busara ya kawaida tu ya kiuongozi.

1. Kutotumia lugha ya kijeuri, matusi, ubabe, vitisho na majigambo
2. Kukiri kuwa nchi ina hali tete kiuchumi na anahitaji kuinyanyua - of course kinyume na tambo za mtangulizi wake
3. Reconciliatory tone na private sector na investors
4. Kukiri uwepo wa COVID-19 na kuruhusu sayansi ichukue nafasi yake

II) NEGATIVES
1. Rais Samia ameendelea kuwakumbatia watendaji wakuu katika nafasi zote nyeti - hawa wote (angalia orodha hapa chini) aliwarithi kutoka kwa mtangulizi wake.
Ukiukwaji wa haki kwa baadhi ya Watanzania ulitokea right under their watch. Kuna kila dalili kuwa ukiukwaji huu umeshaanza kurejea tena (rejea dinner get together ya wamama wa Chadema hivi karibuni):
  • PM (huyu binafsi sitamsahau kwa kitendo chake cha kutosema ukweli - tena akiwa madhabahuni - kuhusu afya ya Magufuli. Alidai Magufuli haumwi ila yupo bize na mafaili!)
  • IGP (polisi ni kama ndiyo walikuwa watendaji na wasemaji wakuu wa chama tawala)
  • DGISS (tunaweza kumuita alikuwa ni pacha wake na IGP)
2. Ukiukwaji wa katiba bado unaendelea chini ya Rais Samia:
  • Ndani ya bunge kuna wabunge ambao hawatambuliki kikatiba. Samia analijua hilo na repercussions zake kisheria, kiuchumi, kijamii na kisiasa lakini ka-mute tu
  • Kisiasa, Rais Samia ameipa likizo katiba - tafsiri yake ni kwamba ameruhusu baadhi ya watu (akiwemo yeye mwenyewe kutumia fursa hiyo kufanya maamuzi yanayoweza kuwa yanakiuka sheria na watu kama IGP kama tulivyoshuhudia hivi karibuni polisi walivyokwenda kuwafanyia vurugu wamama wa Chadema kwenye dinner yao)
3. Kuingiza siasa katika kukabiliana na COVID-19:

Pamoja na sasa kuamua kui tackle COVID-19 kisayansi, bado tumeshuhudia kauli zinazokinzana kutoka kwa Rais Samia. Alinukuliwa akiwataka Watanzania wajilinde na COVID-19 kwa kukwepa mikusanyiko isiyo ya lazima. Siku chache baadaye akanukuliwa akiwasifu vijana waliolundikana kwa wingi sehemu moja kwa starehe zao huku hawajachukua tahadhari yoyote ya kujikinga. Tukumbuke vijana hao waliokusanyika ndiyo wale wale waliokuwa wakitumiwa katika propaganda mbalimbali za mtangulizi wake.

III. TUTOKEJE HAPA?
Ili Rais Samia aache lasting legacy, inampasa afanye kitu kurejesha tabasamu lililopotea miongoni mwa Watanzania tangu awamu ya 5 ilivyoingia madarakani kwa kufanya yafuatayo:

1. Hatua ya kwanza ni kuwaondoa wahifidhina kwenye ranks za uongozi (serekalini na chamani)
2. Kinachofuata akutane na wawakilishi kutoka makundi mbalimbali ndani ya nchi - vyama vya siasa, taasisi zinazosimamia haki, jumuiya za wasomi, taasisi za dini, nk
3. Atangaze mchakato wa undikwaji wa katiba mpya. Tayari tunayo rasimu ya Warioba - tuanzie hapo. Ashirikiane na taasisi nilizozitaja hapo # 2 kuunda mfumo muafaka wa namna kuunda bunge la katiba kwa ajili ya kuipitia rasimu a Warioba
4. Aamuru mahubusu wote wa kisiasa waachiwe huru (ikiwamo kutangaza msamaha kwa waliofungwa kwa sababu hizo hizo)
5. Atamke hadharani usalama wa Watanzania waliokimbia nchi kwa sababu za kisiasa
 
Umeandika kwa busara Sana na mantiki kubwa. Very few vijana kama wewe (sijui Kama wewe ni kijana) wanaweza kuandika hivi.

2. Huyu mama hawezi kufanya tofauti na Magufuli, haya ya mwanzo Ni kuwapoza watu. Lkn ni replica ya Magufuli and the worse is to come! Huyu anaweza kuwa katili kuliko Magufuli, Idd Amin na akina Bokassa na Mobutu! Time is ticking.
 
Umeandika kwa busara Sana na mantiki kubwa. Very few vijana kama wewe (sijui Kama wewe ni kijana) wanaweza kuandika hivi.

2. Huyu mama hawezi kufanya tofauti na Magufuli, haya ya mwanzo Ni kuwapoza watu. Lkn ni replica ya Magufuli and the worse is to come! Huyu anaweza kuwa katili kuliko Magufuli, Idd Amin na akina Bokassa na Mobutu! Time is ticking.
Niko kwenye wrong side of 50 mkuu!
 
Duh! Hatayaweza yote hayo pamoja kwa muda mfupi. Tumpe muda lama yeye alivyotaka apewe muda aweke baadhi ya mambo sawa kama alivyoanisha kwenye mkutano na wahariri wa vyombo vya habari.
 
Tulikuwa na matumaini makubwa na Samia. Kumbe yeye anataka kufanya cosmetic changes, hayuko serious na reforms za msingi za kuipeleka nchi mbele.

Samia kumbe kuna mambo ya hovyo ya Magufuli anayahusudu, mwanzo nilidhani yale mazuri ya Magufuli kama vile miradi ya kimkakati ndo atayachukua, kumbe hata yale ya kijinga kama kuvunja katiba nayo anayakumbatia.

Samia asipofanya reforms za msingi za kisiasa na kudhani kuwa uchumi pekee ndo jambo la msingi atajikuta katika hali ngumu sana huko mbeleni hasa kama hatua zake za kiuchumi zitafeli, Atakuwa hana mtaji wowote wa kisiasa wa kuvuka mawimbi ya dissatisfaction za wananchi. Ikifikia hatua hiyo ataanza kutumia njia zilezile za kidhalimu za Magufuli za kunyamazisha watu, kubambikiza kesi, makundi ya wasiojulikana ili kuzima kelele!.

Kama Samia hatoona umuhimu wa katiba nzuri, basi uraisi wake utaishia kuwa ni wa "CARE TAKING" Presidency, yaani kumalizia tu muhula wa Magufuli huku yeye binafsi akiacha alama ndogo sana kwenye historia ya nchi hii!
 
Umeandika kwa busara Sana na mantiki kubwa. Very few vijana kama wewe (sijui Kama wewe ni kijana) wanaweza kuandika hivi.

2. Huyu mama hawezi kufanya tofauti na Magufuli, haya ya mwanzo Ni kuwapoza watu. Lkn ni replica ya Magufuli and the worse is to come! Huyu anaweza kuwa katili kuliko Magufuli, Idd Amin na akina Bokassa na Mobutu! Time is ticking.
Hii tabia ya kilalamishi ndio iliyowafanya watu wengine kutamani kiongozi mbabe ili mambo yaende mwishowe ikawa vilio tena. Nchi imepata kiongozi very accommodating angepewa nafasi afanye kazi.. Tusiwe walalamaji sana kama Waisraeli jangwani wakati wanatoka utumwani Misri.
 
Sishauri kuondolewa kwa top yeyote ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama

Kama Siro Mabeyo na Diwani

Hawa watu hawana shida yeyote walitaka kuburuzwa na Magufuli kwa kuwatishia kuwapoteza halafu akapotea yeye.

Ni watu makini sana na sio wezi

Naomba usimshauri mama kutikisa kiberiti!!
 
I) POSITIVES:

Tangu ameingia madarakani, tumeona mabadiliko kidogo sana yenye mwelekeo chanya. Nimetumia expression ya "kidogo sana" kwa vile si mambo yaliyohitaji kutumia effort kubwa sana kuyatekeleza bali yanahitaji self-restraint pamoja na busara ya kawaida tu ya kiuongozi..
Sawa huo ndio ukweli.
 
Sishauri kuondolewa kwa top yeyote ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama

Kama Siro Mabeyo na Diwani...
Sirro ni askari mwema sana ni basi mtu amepata bahati mbaya ya kufanya kazi na Magufuli.

Mabeyo ni askari mwaminifu vile vile, angeweza kuvuruga nchi baada ya kifo cha Magu. Ila kafanya mambo very smooth.
Inavyoonekana alikuwa anaburuzwa sana na Magu, kila muda kwenye media. Sasa hivi naamini ana amani.

PM hata kama ni mbovu kiasi gani busara ni kumwacha amalize muda wake maana nchi hii ina mzigo mzito wa kulea wastaafu. Utakuwa ni upuuzi kuongeza udadi bila sababu za msingi.
 
I) POSITIVES:

Tangu ameingia madarakani, tumeona mabadiliko kidogo sana yenye mwelekeo chanya. Nimetumia expression ya "kidogo sana" kwa vile si mambo yaliyohitaji kutumia effort kubwa sana kuyatekeleza bali yanahitaji self-restraint pamoja na busara ya kawaida tu ya kiuongozi...
Hongera Sana kop kwa andiko lako
Kiufupi huyu mama Hana nia ya dhati ya kuukuza huu uchumi Wala kuleta ustawi kwa wananchi, kilichowakimbiza wawekezaji wenye mitaji ya kuleta msisimko wa uchumi wetu ni kitendo cha mtangulizi wake kuvunja katiba waziwazi na yeye hapa Kati karudia yaleyale na ilhali alijua kiwa hakuna mwekezaji makini anaeweza kuweka pesa zake ktk nchi ya namna hii

Pili kuhimiza madalali wetu kuharakisha kumaliza maongezi na wawekezaji kwenye sekta ya mafuta na gesi huku akijua sheria na viwango vya tozo vilivyowekwa na mtangulizi kwa hati ya dharura havimithiriki,ilitakiwa nae apeleke hati ya dharura kwenye kubadilisha hayo kabla ya kuharakisha au kutaka kuwatoa watu ufahamu

Kwenye suala la covid 19 niungane naye kwa kuwa anataka pesa kutoka kwa wafadhili na si kuwa ana nia ya dhati ya kutaka kulinda na kusimamia afya zetu kwani nae bado namuona ni kigeugeu kwenye hili

Kuna mambo ya kumpa muda ila Kuna mengine hatakiwi kuchukua muda mreefu na nguvu nyingi kuyarekebisha km wale wabunge wasio na chama,msimamo kuhusiana na covid19,kutokuvunja katiba na kufanya Tena reform ya uongozi ikiwezekana IGP apumzike
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom