Sababu za kimaandiko kwanini baadhi ya waislamu wanao miliki nyumba Magomeni Na Ilala huwa hawapangishi wakiristu ( Hasa Hasa walokole)

Marekebisho

1. Mamajusi wa mashariki ni wasoma nyota na walikuwa wachawi. Walipeleka manemane na ubani kwa ajili ya kuichukua ile nyota na kumpelekea mfalme wa kipindi kile. Mwisho wa siku walishindwa kuichukua ile nyota
2. Manemane na yenyewe ipo upande wa shetani, sababu pesa ni Kaizari (Ceasur)
Watu mtafika mbinguni lakini mtafika mkiwa mmechoka sana
 
Kafiri (mpingaji)ni mtu anayepinga Allah na uungu wake,siyo kila asiyeamini,maana mwingine hata ujumbe wa Allah hujamfikishia,utamwitaje kafiri!!!?...Kama anakipa sifa za uungu kiumbe lingine Basi huyo ni mshirikina
Kama waislamu wanapo lipa jiwe uungu , kazi ya kusamehe dhambi jiwe Lina fanya na sio tu kusamehe jiwe linafuta dhambi

O Abu abdur-Rahman, why do I only see you touching these two corners?" He said: "I heard Muhammad say: 'Touching them erases sins.'...Sunan an-Nasa'i 2919
 
Ishu wale walokole wanayakemea Sana majini ya kiislam hayakanyagi nyumba yenye mlokole Na ndomaana waislam hawawapendi
 
Ili kubalance stori,
Unazungumziaje swala la Waislamu kuita Kafiri kwa yeyote yule asiye Muislamu?
Mimi ninafsi naona haina shida kama wakristo wanavyosema bila yesu hauendi mbinguni The words with the same meaning but different sound ,kafiri ni neno tu la kiarabu sio tusi "Mpingaji ,Non believer"
 
Harufu ya ubani ule wa kanisani huwa naipenda sana sijui unaitwaje ule

Ila harufu ya udi aisee sitaki hata kuisikia
 
Nimesema I am an open minded person.

Kwa wanao nifahamu wanajua kwamba Mimi Ni muumini mwaminifu Na mtiifi WA Dini ya Kiafrika

Mwamba Ile habari ya Mwanza kuhusu Bibi Fisi na Mwanalugondo ulitishaaaa
 
Walokole wapo hivo Hata mashuleni tulikua na mwanafunzi mlokole hostel yetu yani mnatoka prepo mmechoka mnataka mlale yeye anaanza hapo atasali huyo tena kwanguvu mpaka analia ilikua shida na simu zilikua haziruhusiw japo uweke headphones basi mnabaki tu kusikiliza hahaha
 
Nimetaja Magomeni Na Ilala kwa Sababu almost 90 percent of my extended family live there.

Awali ya yote naomba Ku declare interest.

I am a Muslim but an open minded one .

Am a kind of Muslim who can listen to Jim Reeves or Boney M bila wasiwasi wowote.

Na HII ni Kwa Sababu licha ya kusomeshwa Qur'aan Tukufu lakini nimeisoma Biblia vizuri sana , Nimeisoma Talmud vizuri sana, Nimeisoma Zohar, Vedas nakadhalika...

Back to my point. Wamiliki wengi wa nyumba katika maeneo ya Magomeni Na Ilala ambao Ni waislamu huwa hawapendelei kupangisha wakiristu..

Kwao mpangaji wanae mprefer huwa ni muislamu.

Kama akiwa ni mkristu basi awe Mkatoliki

Kamwe asiwe Mlokole au Mkiristu kutoka dhehebu lolote la kikristu ambalo Lina vinasaba vya kilokole ( Yani wanao Sali kwa kukemea kama walokole etc) mfano KKKT , ANGLICAN au lile kanisa la Wasukuma ( African Inland Church)

Kama ataamua kumpangisha Mkiristu wa madhehebu ya kilokole basi iwe Ni kwenye nyumba ya Peke yake Na ambayo Ina uzio. Yani wewe Mlokole unaweza kupangishwa nyumba Na muislamu WA Ilala au Magomeni lakini nyumba ATAKAYO kupangisha lazima Kwanza iwe Ni nyumba ya wewe Peke yake Na ambayo Ina uzio ama Fensi. ( Nyumba inayo jitegemea)


SABABU NI NINI?

Marko 12:31.
MPENDE JIRANI YAKO KAMA UNAVYO JIPENDA WEWE.


Huyu muislamu hakupangishi wewe kwenye nyumba yake ambayo Ina wapangaji wengi Kwa Sababu anakupenda.

Hataki kukukwaza ( LUKA 17: 1-4)

Kwenye nyumba yake yenye wapangaji Tano Sita Saba Na kuendelea amepangisha waislamu.


. Waislamu husikiliza Qur'aan asubuhi na usiku. Waislamu husikiliza mawaidha ya ma shekhe mbalimbali. MLOKOLE AMEANISHWA KWAMBA UISLAMU NI DINI YA MAJINI. ANAPOSIKIA HATA MTU AKIONGEA TU LUGHA YA KIARABU BASI AKILI HUTAFSIRI KWAMBA MZUNGUMZAJI WA LUGHA HUYO ANAZUNGUMZIA HABARI ZA MAJINI AMBAO KWA MUJIBU WA WALOKOLE MAJINI NI AMONG THE FALLEN ANGELS.

MLOKOLE akisikia Dua inasomwa chumba cha jirani usiku wa Tisa basi ATA Amka ataanza kukemea mapepo.

In addition to that Sisi waislamu kwetu Ni Jambo la kawaida kuchoma ubani Hasa Hasa ubani Maka ( Frank Incense) In fact Kuna hadithi Moja ya Prophet Muhammad, Peace be upon him Ina sisitiza kwamba tujitahidi nyumba ama vyumba tunavyo kaa visikose kufukizwa Kwa ubani Maka Kila siku usiku.

Hapo kwenye ubani ndio more worse Kwa Sababu Kwa typical Mlokole akisikia kuhusu ubani kitu cha Kwanza anawaza ni majini waovu n.k na Mlokole akiamka usiku aka sikia chumba cha jirani Kuna chomwa ubani, atakemea huuyo .

Yani huwa wanaona kama vile ule Moshi ikiingia kwenye pia zake basi umeingia Na Pepo ndani yake..

Most of the time Mlokole huyu ataenda kugonga kwenye chumba cha jirani huyo Na kumwambia azime Huo Moshi au atakupigia simu mwenye nyumba Ku complain kuhusu Moshi WA ubani.
Mwisho WA siku huwa wanahama Na kuacha Kodi. Yani hataki hata kurudishiwa Hela Kwa Sababu anahisi kama vile Hela Zina chuma ulete kwamba Zina majini yatakayo enda kumuibia Hela ambazo Hana.

Sasa basi Kwa kuwa huyu mwenye nyumba anayajua yote haya Na hataki kukukwaza wewe Kwa Sababu anakupenda. Anataka ukae sehemu ambayo utakuwa Na Amani, unapo enda kutafuta chumba kwake, hukujibu Hakuna nafasi..

Wakatoliki hawana shida Sana Na ubani Kwa Sababu wao ubani huchomwa Hadi kanisani kwao.

Naamini walokole miaka kadhaa ijayo NAO wataanza kuwa familiar Na ubani Kwa Sababu baadhi ya wahubiri WA kilokole wameanza kuhubiri kuhusu nguvu ya ubani Na Wana maombi maalumu Kwa ajili ya kuwafungua watu vifungo mbalimbali Kwa kutumia nguvu ya ubani( KUHANI MUSSA)

Naamini program ya KUHANI Mussa baada ya miaka.kadhaa itaondoa Hali ya unyanya paa dhidi ya ubani miongoni WA WALOKOLE Tanzania.


ON SERIOUS NOTE:

Walokole kwanini mnana unyanya paa hivyo ubani? Is it not in it Bible zawadi ya Kwanza aliyopewa Mtoto YESU Na Mamajusi baada ya kuzaliwa ilikuwa UBANI MAKA NA MANEMANE?

Kwa mujibu WA mafundisho Yeni Huu ubani ambao mna unyanyapaa Na kuuita wa mapepo Ni mti ambao umeumbwa Na YESU Mwenyewe ( JOHN 1:1-4)

Mna muudhi Mwenyezi Mungu Kwa kumpa Shetani utukufu wake ( KAZI YA UUMBAJI)

God the Almighty does not like to share his glory with anything.

Vitu vimeumbwa Na Mungu ninyi mnaviita vya Shetani, it's not fair. Can u imagine hata nikivaa Pete ya Emerald, Ruby au Dhahabu nitaambiwa nimevaa Pete ya shetani wakati hizo Ruby zimeumbwa Na Mungu mwenyewe..

Ngoja Niwa kumbushe kitu kimoja hampaswi kuwa mbumbumbu wa mbinu ZA kishetani ili asije kuwashinda

(2 Corinthians 2:11)

Lucifer is very skilled in putting what you hate in what u love as well as putting what u hate in what was useful to you.

Baadhi ya vitu ambavyo Mungu aliviumba Kwa ajili ya kumsaidia binadamu Bwana Ibilisi amefanikiwa kuwahadaa baadhi ya watu kwamba Ni vya kwake yeye. Matokeo yake mna vinyanyapaa mnaacha kuvitumia vitu ambavyo kama mngevitumia vingewasaidia Sana.

Mfano Maandiko yanasema Mali,Fedha,Dhahabu Vitu vyote Ni vyake Mungu lakini shetani amefanikiwa kuwashawishi muamini vitu hivyo Ni vya kwake..

MY PREDICTION: KWA UWEPO WA WATU KAMA KUHANI MUSSA N.K MIAKA INAYO KUJA WALOKOLE WENGI WATAANZA KUONDOKANA NA ILE ROHO YA UNYANYAPAA DHIDI YA VITU VILIVYO UMBWA NA MWENYEZI MUNGU AMBAVYO SHETANI AMEFANIKIWA KUWASHAWISHI WATU WAAMINI KWAMBA NI VITU VYAKE SHETANI.

Kwa mfano miaka Kumi Na Tano iliyo pita Kuna mtu aliamini mlokole angeweza kumwaga chumvi ya upako, au mafuta ya upako kwenye duka lake?

Kuchukua mchanga nyumbani kwake kwenda kuuombea kanisani n.k?

Itafika kipindi atakuja MHUBIRI atasema Sasa Ni wakati WA kufunguliwa Kwa kutumia Dhahabu kwamba cheni ya Dhahabu au Pete ya Dhahabu inaombewa then unavaa ..

Walokole acheni kumpa Shetani umuhimu ambao Hana
Mim nadhani wanapenda wakatoliki kwa kua wako weak spiritually, ni rahisi kuwa challenge/kuwaonea kwenye anga za kiroho kimazingara
 
Mim nadhani wanapenda wakatoliki kwa kua wako weak spiritually, ni rahisi kuwa challenge kwenye anga za kiroho
Nani kakudanganya mkuu? Unadhani kusoma Sana bible, kukemea Sana Na kukesha kanisani ndio kuwa spirituality strong ?
 
Ila walokole hata makazini tu kufanya nao kazi inahitaji moyo hata kwa sisi wakristo wenzao....
Ni kweli , hawa wanadai. Walitumwa kueneza injili kwa wote,, sasa sijui injili inamsaidia nini mungu hadi alazimishe watu wahubiriwe kwa nguvu....
Wakatolic na wasabato, Aic ni madhehebu ya watu makini hawaga papara yaani
 
Ila sisi waafrika hizi imani mbili badala ya kutusaidia imetufanya kuwa wanafiki kupita kiasi.

Mtu mweusi ni mnafiki hasa likija swala la hizi imani mbili.

Sababu kuu ya hizi imani mbili kumjia nigger ni kumkomboa. Badala yake nigger ni kiumbe wa ajabu. Nigger sisi ni wanafiki hatupendani.

Ndo maana tunakopa matrillion. Tutabaki kulipa tu matrillion bila huruma mzigo unabebeshwa halaiki ya manniger wengine. Hatuna huruma kabisa kwa manniger wengine.

Tufe tu tupoteee kabisa. Tuna bahati tu Yesu ni pendo na ana huruma.
Hata ulaya hizi imani ziliwapiganisha sana mpaka wakaona hakuna tija,
Pope urban alianzisha crusade, lengo la kuikomboa jerusalem , vita ilipiganwa kwa miaka karibu 900,na wakashindwa
Tangu hapo wazungu waliamua watapigana vita vya dini kwa akili, maana kwa nguvu ilishindikana,
Siku hizi wanatumia divide and rule tactics
 
Walokole ni watu wa amani sana wanafiti popote ukikosana na mlokole basi wewe ni kafiri mdogo ake shetani
 
Back
Top Bottom