Sababu za kimaandiko kwanini baadhi ya waislamu wanao miliki nyumba Magomeni Na Ilala huwa hawapangishi wakiristu ( Hasa Hasa walokole)

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
15,099
27,067
Nimetaja Magomeni Na Ilala kwa Sababu almost 90 percent of my extended family live there.

Awali ya yote naomba Ku declare interest.

I am a Muslim but an open minded one .

Am a kind of Muslim who can listen to Jim Reeves or Boney M bila wasiwasi wowote.

Na HII ni Kwa Sababu licha ya kusomeshwa Qur'aan Tukufu lakini nimeisoma Biblia vizuri sana , Nimeisoma Talmud vizuri sana, Nimeisoma Zohar, Vedas nakadhalika...

Back to my point. Wamiliki wengi wa nyumba katika maeneo ya Magomeni Na Ilala ambao Ni waislamu huwa hawapendelei kupangisha wakiristu..

Kwao mpangaji wanae mprefer huwa ni muislamu.

Kama akiwa ni mkristu basi awe Mkatoliki

Kamwe asiwe Mlokole au Mkiristu kutoka dhehebu lolote la kikristu ambalo Lina vinasaba vya kilokole ( Yani wanao Sali kwa kukemea kama walokole etc) mfano KKKT , ANGLICAN au lile kanisa la Wasukuma ( African Inland Church)

Kama ataamua kumpangisha Mkiristu wa madhehebu ya kilokole basi iwe Ni kwenye nyumba ya Peke yake Na ambayo Ina uzio. Yani wewe Mlokole unaweza kupangishwa nyumba Na muislamu WA Ilala au Magomeni lakini nyumba ATAKAYO kupangisha lazima Kwanza iwe Ni nyumba ya wewe Peke yake Na ambayo Ina uzio ama Fensi. ( Nyumba inayo jitegemea)


SABABU NI NINI?

Marko 12:31.
MPENDE JIRANI YAKO KAMA UNAVYO JIPENDA WEWE.


Huyu muislamu hakupangishi wewe kwenye nyumba yake ambayo Ina wapangaji wengi Kwa Sababu anakupenda.

Hataki kukukwaza ( LUKA 17: 1-4)

Kwenye nyumba yake yenye wapangaji Tano Sita Saba Na kuendelea amepangisha waislamu.


. Waislamu husikiliza Qur'aan asubuhi na usiku. Waislamu husikiliza mawaidha ya ma shekhe mbalimbali. MLOKOLE AMEANISHWA KWAMBA UISLAMU NI DINI YA MAJINI. ANAPOSIKIA HATA MTU AKIONGEA TU LUGHA YA KIARABU BASI AKILI HUTAFSIRI KWAMBA MZUNGUMZAJI WA LUGHA HUYO ANAZUNGUMZIA HABARI ZA MAJINI AMBAO KWA MUJIBU WA WALOKOLE MAJINI NI AMONG THE FALLEN ANGELS.

MLOKOLE akisikia Dua inasomwa chumba cha jirani usiku wa Tisa basi ATA Amka ataanza kukemea mapepo.

In addition to that Sisi waislamu kwetu Ni Jambo la kawaida kuchoma ubani Hasa Hasa ubani Maka ( Frank Incense) In fact Kuna hadithi Moja ya Prophet Muhammad, Peace be upon him Ina sisitiza kwamba tujitahidi nyumba ama vyumba tunavyo kaa visikose kufukizwa Kwa ubani Maka Kila siku usiku.

Hapo kwenye ubani ndio more worse Kwa Sababu Kwa typical Mlokole akisikia kuhusu ubani kitu cha Kwanza anawaza ni majini waovu n.k na Mlokole akiamka usiku aka sikia chumba cha jirani Kuna chomwa ubani, atakemea huuyo .

Yani huwa wanaona kama vile ule Moshi ikiingia kwenye pia zake basi umeingia Na Pepo ndani yake..

Most of the time Mlokole huyu ataenda kugonga kwenye chumba cha jirani huyo Na kumwambia azime Huo Moshi au atakupigia simu mwenye nyumba Ku complain kuhusu Moshi WA ubani.
Mwisho WA siku huwa wanahama Na kuacha Kodi. Yani hataki hata kurudishiwa Hela Kwa Sababu anahisi kama vile Hela Zina chuma ulete kwamba Zina majini yatakayo enda kumuibia Hela ambazo Hana.

Sasa basi Kwa kuwa huyu mwenye nyumba anayajua yote haya Na hataki kukukwaza wewe Kwa Sababu anakupenda. Anataka ukae sehemu ambayo utakuwa Na Amani, unapo enda kutafuta chumba kwake, hukujibu Hakuna nafasi..

Wakatoliki hawana shida Sana Na ubani Kwa Sababu wao ubani huchomwa Hadi kanisani kwao.

Naamini walokole miaka kadhaa ijayo NAO wataanza kuwa familiar Na ubani Kwa Sababu baadhi ya wahubiri WA kilokole wameanza kuhubiri kuhusu nguvu ya ubani Na Wana maombi maalumu Kwa ajili ya kuwafungua watu vifungo mbalimbali Kwa kutumia nguvu ya ubani( KUHANI MUSSA)

Naamini program ya KUHANI Mussa baada ya miaka.kadhaa itaondoa Hali ya unyanya paa dhidi ya ubani miongoni WA WALOKOLE Tanzania.


ON SERIOUS NOTE:

Walokole kwanini mnana unyanya paa hivyo ubani? Is it not in it Bible zawadi ya Kwanza aliyopewa Mtoto YESU Na Mamajusi baada ya kuzaliwa ilikuwa UBANI MAKA NA MANEMANE?

Kwa mujibu WA mafundisho Yeni Huu ubani ambao mna unyanyapaa Na kuuita wa mapepo Ni mti ambao umeumbwa Na YESU Mwenyewe ( JOHN 1:1-4)

Mna muudhi Mwenyezi Mungu Kwa kumpa Shetani utukufu wake ( KAZI YA UUMBAJI)

God the Almighty does not like to share his glory with anything.

Vitu vimeumbwa Na Mungu ninyi mnaviita vya Shetani, it's not fair. Can u imagine hata nikivaa Pete ya Emerald, Ruby au Dhahabu nitaambiwa nimevaa Pete ya shetani wakati hizo Ruby zimeumbwa Na Mungu mwenyewe..

Ngoja Niwa kumbushe kitu kimoja hampaswi kuwa mbumbumbu wa mbinu ZA kishetani ili asije kuwashinda

(2 Corinthians 2:11)

Lucifer is very skilled in putting what you hate in what u love as well as putting what u hate in what was useful to you.

Baadhi ya vitu ambavyo Mungu aliviumba Kwa ajili ya kumsaidia binadamu Bwana Ibilisi amefanikiwa kuwahadaa baadhi ya watu kwamba Ni vya kwake yeye. Matokeo yake mna vinyanyapaa mnaacha kuvitumia vitu ambavyo kama mngevitumia vingewasaidia Sana.

Mfano Maandiko yanasema Mali,Fedha,Dhahabu Vitu vyote Ni vyake Mungu lakini shetani amefanikiwa kuwashawishi muamini vitu hivyo Ni vya kwake..

MY PREDICTION: KWA UWEPO WA WATU KAMA KUHANI MUSSA N.K MIAKA INAYO KUJA WALOKOLE WENGI WATAANZA KUONDOKANA NA ILE ROHO YA UNYANYAPAA DHIDI YA VITU VILIVYO UMBWA NA MWENYEZI MUNGU AMBAVYO SHETANI AMEFANIKIWA KUWASHAWISHI WATU WAAMINI KWAMBA NI VITU VYAKE SHETANI.

Kwa mfano miaka Kumi Na Tano iliyo pita Kuna mtu aliamini mlokole angeweza kumwaga chumvi ya upako, au mafuta ya upako kwenye duka lake?

Kuchukua mchanga nyumbani kwake kwenda kuuombea kanisani n.k?

Itafika kipindi atakuja MHUBIRI atasema Sasa Ni wakati WA kufunguliwa Kwa kutumia Dhahabu kwamba cheni ya Dhahabu au Pete ya Dhahabu inaombewa then unavaa ..

Walokole acheni kumpa Shetani umuhimu ambao Hana
 
Aseee, so baada ya kufaham Imani zote hizo na mienendo yake nini umegundua?.

Maana bado imani moja tu ambayo sidhani kama unaweza kujaribu kuifuatilia, imani/dini ya mwafrika ambayo hapo kabla ya hizo ulizojifunza ilikuwepo.
Nimesema I am an open minded person.

Kwa wanao nifahamu wanajua kwamba Mimi Ni muumini mwaminifu Na mtiifi WA Dini ya Kiafrika
 
Aseee, so baada ya kufaham Imani zote hizo na mienendo yake nini umegundua?.

Maana bado imani moja tu ambayo sidhani kama unaweza kujaribu kuifuatilia, imani/dini ya mwafrika ambayo hapo kabla ya hizo ulizojifunza ilikuwepo.
@LIKUD Huko Ndio Anaweza Kuwa Mbobezi Zaidi Kuliko Huku Kwenye Hizi Mbili, Pitia Baadhi Ya Nyuzi Zake Unaweza Kusema Ni Mganga Maana Imani Ya Kiafrika Ukiizingatia Sana Kuitwa Mganga Hakukwepeki.
 
Hahaha nimecheka mpaka nimepaliwa. Sawa una hoja mkuu LIKUD kutokana na research ambayo ulisema utaifanya na kuja na majibu yake kuhususiana na maswala ya uchawi na imani kwa ukubwa wake.
Nataka kukuthibitishia kwamba "WALE WAMWABUDIO MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI HAWATAKUJA KUKUBALIANA NA UYASEMAYO MILELE" kwasababu Biblia haifundishi kushirikiana (kufungamana kwa jinsi ya kufuatana) kwa namna yoyote na wasio wa imani moja zaidi sana ushirikiano na mtenda dhambi wanakatazwa kabisa.
 
Ila sisi waafrika hizi imani mbili badala ya kutusaidia imetufanya kuwa wanafiki kupita kiasi.

Mtu mweusi ni mnafiki hasa likija swala la hizi imani mbili.

Sababu kuu ya hizi imani mbili kumjia nigger ni kumkomboa. Badala yake nigger ni kiumbe wa ajabu. Nigger sisi ni wanafiki hatupendani.

Ndo maana tunakopa matrillion. Tutabaki kulipa tu matrillion bila huruma mzigo unabebeshwa halaiki ya manniger wengine. Hatuna huruma kabisa kwa manniger wengine.

Tufe tu tupoteee kabisa. Tuna bahati tu Yesu ni pendo na ana huruma.
 
Ubani haufukuzi majini Bali ni chakula cha majini

Usiponielewa Sasa utaelewa tu hata kama ni baadaye Sana

Afu kuhusu kuomba kwa sauti au kukemea
Mbona watu Wana subwoofer na wanaweka sauti mpaka inakera
Niliomba kwa sauti Kuna Nini
Me nadhan shida sio kelel shida ni mapepo ndo yanawafanya msipende (japo binafs siombag kwa sauti Kali (wisdom))
 
Ubani haufukuzi majini Bali ni chakula cha majini

Usiponielewa Sasa utaelewa tu hata kama ni baadaye Sana

Afu kuhusu kuomba kwa sauti au kukemea
Mbona watu Wana subwoofer na wanaweka sauti mpaka inakera
Niliomba kwa sauti Kuna Nini
Me nadhan shida sio kelel shida ni mapepo ndo yanawafanya msipende (japo binafs siombag kwa sauti Kali (wisdom))
Chakula cha majini how? Andiko lolote?unazungumziaje ishu ya mama jusi kupeleka Kwa Mtoto YESU zawadi ya Ubani Na MANEMANE?
Vipi kuhusu wakatoliki kufukiza ubani altareni?
 
Hahaha nimecheka mpaka nimepaliwa. Sawa una hoja mkuu LIKUD kutokana na research ambayo ulisema utaifanya na kuja na majibu yake kuhususiana na maswala ya uchawi na imani kwa ukubwa wake.
Nataka kukuthibitishia kwamba "WALE WAMWABUDIO MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI HAWATAKUJA KUKUBALIANA NA UYASEMAYO MILELE" kwasababu Biblia haifundishi kushirikiana (kufungamana kwa jinsi ya kufuatana) kwa namna yoyote na wasio wa imani mocha zaidi sana ushirikiano na mtenda dhambi.
Wee nae ni wale wale tu, yaan hiyo dini ya mkoloni inakupa kiburi cha kujiona mtakatifu na mkweli, lkn ungejua nn kipo nyuma ya hizo imani zenu uchwara, kwa hakika ungeshaachana nazo
 
Dini zote chanzo chake ni kimoja na mmilik ni mmoja.

Haya tunaongea kila siku humu lkn watu hawaelewi, hiv muafrika inakuwaje unamtenga na kumkebehi mwenzako kisa dini uliyoletewa?

Huyo Mungu wa dini kama alkuwa na upendo why alete imani zake kupitia ukoloni na mauwaji ya kutisha?

Dini ni ujinga na upumbavu, Muumba wa kwel hapatikan ktk hayo magenge yenu ya ibada za jumapil, ijumaa,na jmos.

Dini zote muanzilishi ni mmoja kupitia vibaraka wake yaan warumi&waarabu bila kuwasahau wahindu na takataka zingine ziitwazo dini.

Viumbe wote hao majin,malaika,wakina yesu, Allah,yehova, yahwe,elishadai, alpha&Omega, hawa woote ni kiumbe mmoja ktk uhalisia wa majina tofaut tofaut, na ndye yule aliyejivka utakatifu na kuchukua mamlaka yasiyo yake kwa kuwafanya watu wamuabudu bila wao kujua ama kwa kujua.

Dini ya kweli ambayo wanajua nini wanakiabudi na nan wanamtumikia ni hao muwaitao waabudu shetan na freemason, maana hawa wanaabudu directly kiumbe wakijuacho kuwa ni shetan, lkn nyie wengine mko brainwashed kwa uongo mliokalilishwa na viongoz wenu wa dini.

Ukiwa open minded utanielewa nini namaanisha, chunguza maandiko, chunguza history ya dunia, utagundua kuwa tunaish ktk dunia iliyojawa uongo, na ukwel unajulkana kwa kiwango kidogo sana.


1641550725947.jpg
 
Ubani siutaki kabisa , kuna binti nilimweka ofisini kila siku nakuta kachoma ubani ,nikimwambia why hana jibu ,nikamwambia sitaki fanya ukiwa kwako ,mwisho siku haachi basi nikamtoa kazini.

Ubani haifukuzi hata mbu ina kazi gani ya maana.
 
Back
Top Bottom