Sababu za Bunge la Jamhuri ya Muungano kukosa umaana

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Bunge letu, kikatiba ni chombo muhimu sana, na ni miongoni mwa mihimili mitatu ya Taifa. Bunge siyo club ya mpira. Bahati mbaya, wabunge wengi wa Bunge letu la sasa, inaonekana hawatambui hadhi ya Bunge, nguvu ya Bunge na majukumu muhimu ya Bunge.

Hivi sasa tunashuhudia Bunge ambalo kwa vigezo vya chombo cha uwakilishi, kukosa umaana. Bunge limekuwa likitumia muda mwingi kujadili mambo yasiyo na tija kwa Taifa na wananchi.

Bunge kwa sasa, kwa mtazamo wa baadhi ya wananchi walio wengi, imekuwa ni chombo cha kutafuna pesa za umma bila ya umma kunufaika na chombo hicho. Bunge limekuwa kama club ya mabishano, mahali pa kupigana vijembe, kutoleana masimango, mahali pa kufanyiana kejeli, kuumbuana, na mahali pa kufanyia ushabiki.

Kutokana na mwenendo usio na tija wa Bunge la sasa, hata Mh. Rais amevumilia lakini baadaye ameshindwa, akalazimika kutoa neno. Ni aibu kubwa kwa wabunge wenyewe, ni aibu kwa Spika na aibu kubwa zaidi kwa Bunge zima kama mhimili.

Mara nyingi, uimara au udhaifu wa kitu hutokana na uanzishwaji wake na upatikanaji wake. Kama ulikuwa unapita jirani na bar, ukamwona msichana mrembo pale bar, ukavutiwa naye, na baadaye ukamchumbia na kumwoa, usishangae kuwa na mke mlevi.
Maana ulitakiwa kujiuliza pale bar alikuwa anatafuta nini, kabla unamchumbia.

Bunge letu ni matokeo ya sheria, kanuni na taratibu zetu mbaya zinazotuongoza namna ya kumpata Mbunge, na sifa za yule anayeutaka ubunge.

Karne hii, bado tuna sheria zinazosema elimu ya Mbunge ni Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK), wakati dereva wa gari la serikali, sifa yake mojawapo ni kwamba angalao awe amemaliza kidato cha nne. Ndiyo maana haishangazi kuona watu ambao walitakiwa kwenda kwenye taasisi za kufuta ujinga, kwa Tanzania, wapo Bungeni tukitarajia watunge sheria za kuendeleza elimu wakati wao wenyewe hawana elimu.

Upatikanaji wa wabunge wa Bunge la sasa, ilikuwa ni mchakato mchafu kuliko mchakato wowote uliowahi kuwepo katika Taifa hili. Bunge hili, ni bunge la chama kimoja, CCM.

Huko CCM, mchakato wa kuwapitisha wagombea ulikuwa magumashi na uchafu wa hali ya juu. Maeneo mengine, mtu aliyepata kura za mapendekezo zaidi ya 300 aliachwa, alipewa mtu aliyepata kura 3.

Kwenye uchaguzi mkuu, wagombea wa vyama vingine walifutwa bila sababu yoyote ya msingi. Waliobakizwa, ushiriki wao uliofanywa kuwa wasindikizaji katika mchakato ambao Tume ya Uchaguzi walikuwa na maelekezo ya kutomtangaza mgombea asiye wa CCM.

Tunaweza kupinga kwa sababu ya ushabiki, lakini ni ukweli usiopingika kuwa Bunge hili ni Bunge ambalo wabunge wake waliteuliwa na kupitishwa na mtu mmoja, na zaidi kwa kuangalia watu hao wana uwezo wa kumsifu kwa kiwango gani. Na siku zote watu wanaopenda kusifu sana, ni wanafiki na watu wenye uwezo mdogo kifikra. Mwenye akili kabisa na uwezo unaojitegemea, hawezi kukubali kufanywa mtu asiye na mawazo ambaye kazi yake ni kusifia tu.

Kutarajia kupata tija yoyote kutoka kwenye Bunge hili, ni kusubiria embe chini ya mchongoma.

USHAURI
Turudi kwenye mchakato wa katiba mpya. Na kwenye kipengere cha Bunge, mapendekezo yangu:

Kwanza kwa aina ya wabunge hawa tulio nao, hata kama tusingekuwa na Bunge kabisa, hakuna kitakachobadilika.

Tuwe na Bunge ambalo lina wabunge wanaotokana na mikoa. Kila mkoa wabunge wawili. Hivyo, Bunge zima lisizidi wabunge 100. Sifa za hao wabunge zifafanuliwe vizuri ili kuepuka wabunge wanaojua KKK tu, wa aina za akina Kibajaji, Musukuma, Japipo, n.k.

Na Spika naye sifa zake zifafanuliwe, na sifa mojawapo ni kuwa aliwahi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu au mwenye sifa zinazomwezesha kuwa jaji wa Mahakama Kuu.

Baraza la Mawaziri litokane na watu wasiokuwa wabunge ili Rais awe na uwanja mpana wa kuwapata watu wenye uwezo wa kumsaidia katika kuendesha Serikali.

Rais apeleke majina mawili Bungeni ya watu wasiokuwa wabunge kwaajili ya kumpata Waziri mkuu. Waziri Mkuu ni yule ambaye atapata zaidi ya theluthi 2 za kura za wabunge. Akikosekana aliyepata zaidi ya theluthi 2, Rais apeleke jina la tatu, na wote watatu wapigiwe kura na wabunge. Waziri mkuu awe yule aliyepata zaidi ya 50% ya kura.
 
Upo sahihi, lakini CCM na serikali yake ndio master plan wa Bunge hilo la hovyo na ndio wanufaika wakubwa wa ujinga wa Mtanzania, tusitegemee hata siku moja CCM na serikali yake kutupatia katiba iliyo bora na kutuwekea mifumo imara ya kuliendeleza Taifa na raia wake,haita wezekana kwa sababu wanajua ndio utakuwa mwisho wa utawala wao.
 
Haya pia yanahitajika katika katiba mpya

1.Viti maalum viondolewe na viti kumi vya ubunge vya Rais viondolowe.Tuwe na wabunge waliochaguliwa na wananchi tu.

2.Katibu wa bunge achaguliwe na spika wa bunge sio Rais

3.Mbunge asinyanga'anywe ubunge wake akihama chama.
 
Hapo kwenye upatikanaji wa wabunge, naunga mkono kuwe na wabunge wawili toka kila mkoa, na kwenye upigaji wa kura nafasi moja iwe ya mbunge kutoka chama pinzani na ingine toka chama Tawala, ila nafasi ya Rais iwe moja kila chama kisimamishe mgombea. Pia tuwe na vyama viwili tu vya siasa hii mambo ya kuwa na utitiri wa vyama vya siasa ni Kansa ingine.

Katiba mpya ni muhimu sana kwa nyakati hizi na zijazo.
 
Hapo kwenye upatikanaji wa wabunge, naunga mkono kuwe na wabunge wawili toka kila mkoa, na kwenye upigaji wa kura nafasi moja iwe ya mbunge kutoka chama pinzani na ingine toka chama Tawala, ila nafasi ya Rais iwe moja kila chama kisimamishe mgombea. Pia tuwe na vyama viwili tu vya siasa hii mambo ya kuwa na utitiri wa vyama vya siasa ni Kansa ingine.

Katiba mpya ni muhimu sana kwa nyakati hizi na zijazo.
Tushuke chini kidogo; kuwe na Wabunge wawili kutoka kila wilaya mmoja jinsi moja na mwingine jinsi ya pili. Hii itakuwa na uwakilishi mzuri zaidi na kwa idadi bado watakuwa pungufu ya idadi ya wabunge waliopo sasa. Hata hivyo, sio kwa muundo wa NEC iliyopo ambayo inatakiwa kufumuliwa 100%.
 
Haya pia yanahitajika katika katiba mpya

1.Viti maalum viondolewe na viti kumi vya ubunge vya Rais viondolowe.Tuwe na wabunge waliochaguliwa na wananchi tu...
Hapo namba 3 umeyumba kidogo.

Maana litasababisha umalaya wa kisiasa leo yupo chama hiki kesho kile.

Halafu kumbuka mbunge anaenda kwa ilani ya chama chake
 
Bunge letu, kikatiba ni chombo muhimu sana, na ni miongoni mwa mihimili mitatu ya Taifa. Bunge siyo club ya mpira. Bahati mbaya, wabunge wengi wa Bunge letu la sasa, inaonekana hawatambui hadhi ya Bunge, nguvu ya Bunge na majukumu muhimu ya Bunge...
Umeongea vyema kabisa mkuu, ila tatizo kubwa nchi hii ni ccm wao kwa wingi wao na kutumia dola wamejikita zaidi kwenye maeneo yanayobeba chama na siyo taifa. Ukiangalia bunge letu halina msaada wowote ule kwa jamii, wao kwa wingi wao wapo kama kikundi cha kutetea serikali na siyo kushauri serikali.

Sijawahi kuona bunge hili limepeleka pendekezo lolote la kuishauri na kuisimamia serikali zaidi ya kupitisha miswada yenye ukakasi na kunyonga wananchi. Kwa kupitia Rais Samia nafikiri angesimamia tupate chombo/bunge lenye nguvu na ushawishi pia hili haliwezekani bila katiba mpya itakapowekwa kwa maslahi ya kila mtanzania na siyo chama.

Tupiganie katiba mpya ile ya Jaji Waryoba na siyo vingine tofauti na hapo bunge siku zote watakuwa rubber stamp wa serikali.


Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Umeongea vyema kabisa mkuu, ila tatizo kubwa nchi hii ni ccm wao kwa wingi wao na kutumia dola wamejikita zaidi kwenye maeneo yanayobeba chama na siyo taifa...
Ninaamini, kwa Mh. Rais Samia, hakuna kitu kitakachompa legacy kubwa na ya pekee kama kuimarisha demokrasia na ulinzi wa haki za raia kwa kusimamia uoatikanaji wa katiba itakayokuwa bora, na itakayodumu kwa karne nyingi zijazo.

Kule Marekani, marais wawili pekee ambao Wamarekani wanawaenzi nyakati zote, ni George Washington na Abraham Lincoln.

George Washington anatajwa kwa Baba wa Taifa la Marekani, na Abraham Lincoln kama Baba wa Demokrasia wa Marekani.

Mwalimu Nyerere = George Washington

Samia Suluhu Hassan = Abraham Lincoln?

Tanzania, tunamtafuta Abraham Lincoln. Je, ni Mama Samia Suluhu Hassan, au tusubirie mwingine?
 
Bunge letu, kikatiba ni chombo muhimu sana, na ni miongoni mwa mihimili mitatu ya Taifa. Bunge siyo club ya mpira. Bahati mbaya, wabunge wengi wa Bunge letu la sasa, inaonekana hawatambui hadhi ya Bunge, nguvu ya Bunge na majukumu muhimu ya Bunge..
Wanajadili eti nguvu za kiume hakuna nijuavyo mimi kama huna pesa ujasiri unaondoka 'No money no confidence' nashauri hao wanawake wanao sema vijana hawana nguvu za kiume wawape burungutu kama hawatapata majibu chanya
 
Umeongea vyema kabisa mkuu, ila tatizo kubwa nchi hii ni ccm wao kwa wingi wao na kutumia dola wamejikita zaidi kwenye maeneo yanayobeba chama na siyo taifa...
Bunge la awamu ya 5 lilikuwa kibogoyo, sura za manahodha wa bunge hili ni zilizile. Problems cannot be solved by the same level of thinking that created them
 
Bunge letu, kikatiba ni chombo muhimu sana, na ni miongoni mwa mihimili mitatu ya Taifa. Bunge siyo club ya mpira. Bahati mbaya, wabunge wengi wa Bunge letu la sasa, inaonekana hawatambui hadhi ya Bunge, nguvu ya Bunge na majukumu muhimu ya Bunge.

Hivi sasa tunashuhudia Bunge ambalo kwa vigezo vya chombo cha uwakilishi, kukosa umaana. Bunge limekuwa likitumia muda mwingi kujadili mambo yasiyo na tija kwa Taifa na wananchi.

Bunge kwa sasa, kwa mtazamo wa baadhi ya wananchi walio wengi, imekuwa ni chombo cha kutafuna pesa za umma bila ya umma kunufaika na chombo hicho. Bunge limekuwa kama club ya mabishano, mahali pa kupigana vijembe, kutoleana masimango, mahali pa kufanyiana kejeli, kuumbuana, na mahali pa kufanyia ushabiki.

Kutokana na mwenendo usio na tija wa Bunge la sasa, hata Mh. Rais amevumilia lakini baadaye ameshindwa, akalazimika kutoa neno. Ni aibu kubwa kwa wabunge wenyewe, ni aibu kwa Spika na aibu kubwa zaidi kwa Bunge zima kama mhimili.

Mara nyingi, uimara au udhaifu wa kitu hutokana na uanzishwaji wake na upatikanaji wake. Kama ulikuwa unapita jirani na bar, ukamwona msichana mrembo pale bar, ukavutiwa naye, na baadaye ukamchumbia na kumwoa, usishangae kuwa na mke mlevi.
Maana ulitakiwa kujiuliza pale bar alikuwa anatafuta nini, kabla unamchumbia.

Bunge letu ni matokeo ya sheria, kanuni na taratibu zetu mbaya zinazotuongoza namna ya kumpata Mbunge, na sifa za yule anayeutaka ubunge.

Karne hii, bado tuna sheria zinazosema elimu ya Mbunge ni Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK), wakati dereva wa gari la serikali, sifa yake mojawapo ni kwamba angalao awe amemaliza kidato cha nne. Ndiyo maana haishangazi kuona watu ambao walitakiwa kwenda kwenye taasisi za kufuta ujinga, kwa Tanzania, wapo Bungeni tukitarajia watunge sheria za kuendeleza elimu wakati wao wenyewe hawana elimu.

Upatikanaji wa wabunge wa Bunge la sasa, ilikuwa ni mchakato mchafu kuliko mchakato wowote uliowahi kuwepo katika Taifa hili. Bunge hili, ni bunge la chama kimoja, CCM.

Huko CCM, mchakato wa kuwapitisha wagombea ulikuwa magumashi na uchafu wa hali ya juu. Maeneo mengine, mtu aliyepata kura za mapendekezo zaidi ya 300 aliachwa, alipewa mtu aliyepata kura 3.

Kwenye uchaguzi mkuu, wagombea wa vyama vingine walifutwa bila sababu yoyote ya msingi. Waliobakizwa, ushiriki wao uliofanywa kuwa wasindikizaji katika mchakato ambao Tume ya Uchaguzi walikuwa na maelekezo ya kutomtangaza mgombea asiye wa CCM.

Tunaweza kupinga kwa sababu ya ushabiki, lakini ni ukweli usiopingika kuwa Bunge hili ni Bunge ambalo wabunge wake waliteuliwa na kupitishwa na mtu mmoja, na zaidi kwa kuangalia watu hao wana uwezo wa kumsifu kwa kiwango gani. Na siku zote watu wanaopenda kusifu sana, ni wanafiki na watu wenye uwezo mdogo kifikra. Mwenye akili kabisa na uwezo unaojitegemea, hawezi kukubali kufanywa mtu asiye na mawazo ambaye kazi yake ni kusifia tu.

Kutarajia kupata tija yoyote kutoka kwenye Bunge hili, ni kusubiria embe chini ya mchongoma.

USHAURI
Turudi kwenye mchakato wa katiba mpya. Na kwenye kipengere cha Bunge, mapendekezo yangu:

Kwanza kwa aina ya wabunge hawa tulio nao, hata kama tusingekuwa na Bunge kabisa, hakuna kitakachobadilika.

Tuwe na Bunge ambalo lina wabunge wanaotokana na mikoa. Kila mkoa wabunge wawili. Hivyo, Bunge zima lisizidi wabunge 100. Sifa za hao wabunge zifafanuliwe vizuri ili kuepuka wabunge wanaojua KKK tu, wa aina za akina Kibajaji, Musukuma, Japipo, n.k.

Na Spika naye sifa zake zifafanuliwe, na sifa mojawapo ni kuwa aliwahi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu au mwenye sifa zinazomwezesha kuwa jaji wa Mahakama Kuu.

Baraza la Mawaziri litokane na watu wasiokuwa wabunge ili Rais awe na uwanja mpana wa kuwapata watu wenye uwezo wa kumsaidia katika kuendesha Serikali.

Rais apeleke majina mawili Bungeni ya watu wasiokuwa wabunge kwaajili ya kumpata Waziri mkuu. Waziri Mkuu ni yule ambaye atapata zaidi ya theluthi 2 za kura za wabunge. Akikosekana aliyepata zaidi ya theluthi 2, Rais apeleke jina la tatu, na wote watatu wapigiwe kura na wabunge. Waziri mkuu awe yule aliyepata zaidi ya 50% ya kura.
Huyu ndiye ameshusha hadhi ya Bunge.
FB_IMG_1618336478528.jpg
 
Huyu ndiye ameshusha hadhi ya Bunge.View attachment 1756237
Kwenye management tunafundishwa, 'failure of the organization, is failure of the management'.

Hakika Bunge kuwa la hovyo linaashiria management ya Bunge ni hovyo zaidi. Spika, Naibu Spika, Katibu wa Bunge - hawa ndiyo chanzo cha uhovyo wa Bunge la sasa. Lakini juu ya hao kuna management ya CCM, na zaidi ni failure ya management ya nchi iliyoruhusu watu wa hovyo kupata nafasi ya kuingia bungeni, na wengine kushika mamlaka ya kusimamia taasisi kubwa kama Bunge.
 
Bila katiba bora mjengo utaendelea kuwa hivyo hivyo
Ni hakika. Kilichopo Bungeni kinawakilisha ubaya wa katiba yetu. Katiba yetu inaruhusu hata wa ltu wa hovyo kabisa, kuweza juwa wabunge.
 
Back
Top Bottom