Sababu ya wanafunzi wengi kushindwa somo la Hisabati

Mengi Ayoub

Member
Apr 20, 2022
56
46
Asilimia kubwa ya wanafunzi nchini Tanzania hufanya vibaya SoMo la HISABATI , Jambo linalofanya wengi kuliita tatizo hili gonjwa la taifa . Kuna sababu mbalimbali zinazofanya wanafunzi wengi kushindwa SoMo la HISABATI . Sababu hizo ni Kama ifuatavyo:

1. Ni dhana potofu iliyojijenga katika vichwa vya watu wengi tangu enzi na enzi , juu ya ugumu wa Somo la hisabati . Watu wengi huamini kuwa Somo la hisabati ni gumu Sana . Jambo hili huwakatisha tamaa wanafunzi wengi na kuwafanya wapunguze jitihada za kulisoma somo Hilo.

2. Ni uvivu wa wanafunzi. Kila somo Lina namna yake ya kulisoma . Namna ya kusoma historia ni tofauti na namna ya fizikia. Somo la hisabati huhitaji kusoma kwa kufanya mazoezi ya Mara kwa Mara . Wanafunzi wengi ni wavivu wa kufanya mazoezi . Hivyo somo la hisabati linalohitaji kusomwa Mara kwa Mara hukosa wapenzi.

3. Uhaba wa walimu wa Somo Hili. Dhana potofu iliyojijenga tangu Zamani imeathiri wengi na kusababisha watu wachache tu wenye moyo wa kukazania SoMo Hilo kuendelea kulisoma katika ngazi za stashahada na shahada .

4. Ni ustadi wa walimu . Licha ya kuwa Somo la hisabati Lina walimu wachache , bado hao wachache wenyewe si stadi . Waalimu wengi hawajawa na uwezo mkubwa katika somo hili. Jambo hili huwaathiri wanafunzi na kuwafanya wafeli somo hili.

5. Kukariri. Wanafunzi wengi wamezoea kusoma kwa kukariri . Somo la hisabati halifai kukariri. Hii hulingana na sababu iliyozungumziwa hapo juu ya namna ya kusoma. Ingawa kukariri hakukubaliki , Kuna masomo ambayo mwanafunzi anaweza akakariri na akafaulu. Hii ni tofauti kwa SoMo la hisabati .

6. Ukali wa waalimu wa hisabti. Hii iko wazi , walimu wa hisabati ni wakali Sana . Kumbuka tu walimu waliowahi kukufundisha wewe ....Jambo hili huwatisha wanafunzi na kuwafanya kuogopa SoMo.

Hizo ni baadhi tu Ila zipo sababu nyingi ..

#Eliupendo mbise
#Leonard mbikilwa
 
Ni kweli Ila tunarudi palepale , mtoto anaweza akawa na utayari wa kujifunza Ila changamoto ikawa ukali wa mwalimu , na
Miye mwenyewe mmoja wapo nilisoma hesabu kwa mbinde sana sekonsari. Lakini mwisho wa siku baada ya kumpata ticha mzuri nikasoma pure maths mpk advance.
 
6. Ukali wa waalimu wa hisabti. Hii iko wazi , walimu wa hisabati ni wakali Sana . Kumbuka tu walimu waliowahi kukufundisha wewe ....Jambo hili huwatisha wanafunzi na kuwafanya kuogopa SoMo.


Hapa ndipo kuna suluhisho; kwanini waalimu wa somo la hisabati ndio wawe WAKALI???
 
Asilimia kubwa ya wanafunzi nchini Tanzania hufanya vibaya SoMo la HISABATI , Jambo linalofanya wengi kuliita tatizo hili gonjwa la taifa . Kuna sababu mbalimbali zinazofanya wanafunzi wengi kushindwa SoMo la HISABATI . Sababu hizo ni Kama ifuatavyo:

1. Ni dhana potofu iliyojijenga katika vichwa vya watu wengi tangu enzi na enzi , juu ya ugumu wa Somo la hisabati . Watu wengi huamini kuwa Somo la hisabati ni gumu Sana . Jambo hili huwakatisha tamaa wanafunzi wengi na kuwafanya wapunguze jitihada za kulisoma somo Hilo.

2. Ni uvivu wa wanafunzi. Kila somo Lina namna yake ya kulisoma . Namna ya kusoma historia ni tofauti na namna ya fizikia. Somo la hisabati huhitaji kusoma kwa kufanya mazoezi ya Mara kwa Mara . Wanafunzi wengi ni wavivu wa kufanya mazoezi . Hivyo somo la hisabati linalohitaji kusomwa Mara kwa Mara hukosa wapenzi.

3. Uhaba wa walimu wa Somo Hili. Dhana potofu iliyojijenga tangu Zamani imeathiri wengi na kusababisha watu wachache tu wenye moyo wa kukazania SoMo Hilo kuendelea kulisoma katika ngazi za stashahada na shahada .

4. Ni ustadi wa walimu . Licha ya kuwa Somo la hisabati Lina walimu wachache , bado hao wachache wenyewe si stadi . Waalimu wengi hawajawa na uwezo mkubwa katika somo hili. Jambo hili huwaathiri wanafunzi na kuwafanya wafeli somo hili.

5. Kukariri. Wanafunzi wengi wamezoea kusoma kwa kukariri . Somo la hisabati halifai kukariri. Hii hulingana na sababu iliyozungumziwa hapo juu ya namna ya kusoma. Ingawa kukariri hakukubaliki , Kuna masomo ambayo mwanafunzi anaweza akakariri na akafaulu. Hii ni tofauti kwa SoMo la hisabati .

6. Ukali wa waalimu wa hisabti. Hii iko wazi , walimu wa hisabati ni wakali Sana . Kumbuka tu walimu waliowahi kukufundisha wewe ....Jambo hili huwatisha wanafunzi na kuwafanya kuogopa SoMo.

Hizo ni baadhi tu Ila zipo sababu nyingi ..

#Eliupendo mbise
#Leonard mbikilwa
Sasa hizo dhana potofu na mlolongo wa sababu zingine ulizoorodhesha kwa nini usiangukie na kwa masomo mengine kama kiswahili, civics/general studies, history, maarifa ya jamii etc! Kwa nini zi we ni sababu kwa hisabati tu? Kwa nini kwa mfano, wanafunzi hawajengi dhana potofu kuwa civics au history au kiswahili au theatre art, au fine art, ni masomo magumu pia? Lazima kuna ukweli fulani kuwa somo la hisabati lipo tofauti na masomo mengine hata ujifunzaji wake. Hata waliokula mzinga shuleni wa hisabati wanaweza kuwa ndiyo wa kwanza kupost humu kuwa hisabati ni somo rahisi kama history au civics! Usijejaribu kulinganisha hapo!!
 
Naomba namimi nitoe mchango wangu, somo la Mathematics linahitaji utayari kutoka kwa mwanafunzi. Atakama Serikali itakuwa inaajiri watu wengi kwenye kada ya waalimu wa Sayansi/Mathematics bado kufeli kupo palepale.

Japo si kwa ubaya ila nakumbuka hata wakati nilipokuwa nikisoma katika shule moja ya Sekondari miaka kadhaa ya nyuma, baada ya kuripoti kidato cha kwanza masomo ya PCBM yote hayakuwa na waalimu kabisa. Na hali hiyo tulienda nayo mpaka kidato cha tatu mwishoni. Kwa bahati aliletwa mwalimu mmoja wa Mathematics naye alipitia hali ngumu mno akipambana na kidato cha I hadi Kidato cha IV. Lakini kuna wadau wangu wengi walifanikiwa kusoma combinations za Sayansi na wamefanikiwa mpaka hapa walipo.
 
Shule niliyokuwa nasoma tukitangaziwa darasani mwalimu wa mathematics anadharua hatokuwepo kwa siku mbili kwa hiyo muwe mnajisomea wenyewe , inakuwa kama sherehe kwa wanafunzi class kila mtu anatabasamu..
 
Hisabati ni ngumu kama ambavyo Physics ni ngumu kuliko hisabati.

Hisabati inahitaji kufikiria zaidi jambo ambalo watu wengi uwezo wa kufikiria ni mdogo.


Watu wanaosema Arts na wale wanaosema science , wakisema wabadilishane. Ni nani watakaosavaivu?
 
Back
Top Bottom