consigliori
JF-Expert Member
- Mar 29, 2010
- 392
- 89
Jana nimeona kwenye taatrifa ya habari ya ITV, Balozi wa US nchini alitushauri watanzania kutafakari sababu zinazotufanya kuendelea kuwa masikini pamoja na ukweli kuwa Wahisani wamekuwa wakitoa misaada mingi kwa Tanzania.
Kilichonishangaza ni majibu kwa swali hilo yaliyotolewa na Waziri wetu wa mambo ya nje Mheshimiwa B.Membe. Yeye alizitaja sababu kuu kuwa ni Tanzania kujihusisha sana na harakati za ukombozi wa nchi za kiafrika. Akiendelea kufafanua, Mheshimiwa Membe alisema, TZ ilikuwa kituo cha vikundi mbalimbali vya kupigania uhuru na wakati mwinging askari wetu walitumika katika harakati hizi.
Ninachojiuliza mimi ni je;
tangu harakati hizi za ukombozi ziishe, ni miaka mingapi imepita sasa? Kwa haraka haraka, haipungui miaka 25! 1985 - 2010) Je bado tusingizie kujitolea kwetu kwa nchi nyingine kuwa sababu ya umasikini wetu mpaka leo?
Kilichonishangaza ni majibu kwa swali hilo yaliyotolewa na Waziri wetu wa mambo ya nje Mheshimiwa B.Membe. Yeye alizitaja sababu kuu kuwa ni Tanzania kujihusisha sana na harakati za ukombozi wa nchi za kiafrika. Akiendelea kufafanua, Mheshimiwa Membe alisema, TZ ilikuwa kituo cha vikundi mbalimbali vya kupigania uhuru na wakati mwinging askari wetu walitumika katika harakati hizi.
Ninachojiuliza mimi ni je;
tangu harakati hizi za ukombozi ziishe, ni miaka mingapi imepita sasa? Kwa haraka haraka, haipungui miaka 25! 1985 - 2010) Je bado tusingizie kujitolea kwetu kwa nchi nyingine kuwa sababu ya umasikini wetu mpaka leo?