Sababu ya Pwani, Kanda ya Ziwa kuwa na Wagonjwa Wengi Saratani ya Shingo ya Kizazi

John Haramba

JF-Expert Member
Feb 4, 2022
365
1,373
Cervical cancer.jpeg

Takwimu za Dunia za mwaka 2018 za Shirika la Afya Duniani (WHO) zilionesha Wanawake zaidi ya 570,000 waligundulika kuwa na Saratani ya Shingo ya Kizazi,

Kwa mujibu wa tovuti ya cancer.net ni kuwa kwa mwaka 2020 kulikuwa na Wanawake 604,127 ambayo walikuwa wameathiriwa na ugonjwa huo.

Kwa Tanzania katika miaka ya hivi karibuni utafiti unaonesha maeneo ya Pwani na Kanda ya Ziwa ndipo kulipokuwa na waathirika wengi wa ugonjwa huo.

Elias Kuyamba, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Kina Mama bila kutaja idadi ya namba amefafanua kwa kusema:

“Maeneo ya Ukanda wa Pwani yamekuwa na matukio mengi ya wasichana wadogo kuanza ngono wakiwa na umri madogo.

“Upande wa Kanda ya Ziwa kulikuwa na ile tamaduni ya mwanaume mmoja kumiliki wanawake wengi au kuwa na uhusiano na wanawake wengi, inapotokea mdudu wa saratani ameingia kwa mmoja ni rahisi kusambaa kwa wengine,” anasema daktari.

Amesema inasadikika Kirusi cha HPV ndicho kinasambaza ugonjwa huo, kinachosambaa wakati wa kujamiiana.

“Mwanamke anapovunja ungo kisha akashiriki ngono na mwanaume mwenye kirusi hicho anaweza kuambukizwa na kukaa na kirusi hicho kwa miaka mingi bila kuumwa.

“Mwanaume hata akiwa na hicho kirusi mara nyingi baada ya muda huwa kinapotea chenyewe, tofauti na mwanamke akiwa nacho, ndio maana kumekuwa na kesi nyingi za Saratani ya Shingo ya Kizazi kwa wanawake kuanzia umri wa miaka 35 na kuendelea,” anasema Dkt. Kuyamba.

Amesema kuokoa hali hiyo, Serikali ya Tanzania imepitisha watoto ngazi ya shule hasa wale ambao hawajawahi kufanya ngono kupatiwa chanjo ya kuwakinga na Saratani ya Kizazi, kwa kuwa yeyote ambaye ameshashiriki ngono na ameambukizwa virusi hivyo akiwa anaishi navyo, chanjo haitasaidia.

DALILI ZA SARATANI
-Kutoka damu ukeni baada ya kujamiiana
-Kutoka damu wakati ambao siyo wa hedhi
-Kutoka maji yenye harufu mbaya sehemu za siri
-Maumivu wakati wa kujamiiana
-Haja ndogo na kubwa kutoka hovyo

MATIBABU YA SARATANI
-Mgonjwa anaweza kupona akipata huduma mapema
-Matibabu ya mionzi au upasuaji katika hatua ya awali

KUJIKINGA
-Chanjo
-Kuwe na Awareness kwenye jamii
-Kushiriki ngono salama
 
Kanda ya ziwa ni kwa sababu ya madini.
Ukanda wa Pwani ni kwa sababu ya kuwepo na ndoa za wake wanne
 
Japokuwa saratani ya shingo ya kizazi ndiyo ina cases nyingi nchini ila Kanda ya ziwa ina mchanganyiko wa aina tofauti tofauti nyingi za cancer siyo hiyo tu.

Tafiti zinahitajika maana nadharia zingekuwa nyingi mno.
 
Jamani, hata kama mimi sio mtaalam wa sektabya afya, muwe mnatumia akili kidogo kutudanganya. Hivi kwa akili ya kawaida tu, kirusi kinawezaje kusababisha ‘Cancer’? Kwanza tujue cancer ni nini, na mechanism ya kansa ikoje, tukishajua hii, mtaona how absurd it is kusema kirusi kinasababisha cancer, how? What sort of mechanics could enable a virus to actually cause cancer, naomba kuelimishwa.., maana hii ni sawa na useme radi imesababishwa na jengo kuwa refu..
 
Jamani, hata kama mimi sio mtaalam wa sektabya afya, muwe mnatumia akili kidogo kutudanganya. Hivi kwa akili ya kawaida tu, kirusi kinawezaje kusababisha ‘Cancer’? Kwanza tujue cancer ni nini, na mechanism ya kansa ikoje, tukishajua hii, mtaona how absurd it is kusema kirusi kinasababisha cancer, how? What sort of mechanics could enable a virus to actually cause cancer, naomba kuelimishwa.., maana hii ni sawa na useme radi imesababishwa na jengo kuwa refu..
Kweli aisee, wametumia akili ndogo sana kudanganya, saratani na virus?!
 
Kweli aisee, wametumia akili ndogo sana kudanganya, saratani na virus?!
U
Jamani, hata kama mimi sio mtaalam wa sektabya afya, muwe mnatumia akili kidogo kutudanganya. Hivi kwa akili ya kawaida tu, kirusi kinawezaje kusababisha ‘Cancer’? Kwanza tujue cancer ni nini, na mechanism ya kansa ikoje, tukishajua hii, mtaona how absurd it is kusema kirusi kinasababisha cancer, how? What sort of mechanics could enable a virus to actually cause cancer, naomba kuelimishwa.., maana hii ni sawa na useme radi imesababishwa na jengo kuwa refu..
Unajua kuna mambo mangapi yanayosababisha cancer?
Ni vizuri ukasoma kwanza kabla kubisha vitu usivyovijua
 
Back
Top Bottom