Sababu ya Lissu kushindwa uchaguzi

ForeverMore

JF-Expert Member
Nov 12, 2014
813
1,928
Ki ukweli, kama wewe kwa akili zako zooote, umekaa na kuwaza, ukafanya utafiti na jibu ulilopata ni kuwa Lissu angechukua nchi uchaguzi huu, walahi wewe ni KILAZA.

Magufuli kawa zunguka sana. Kapiga pasi ndefu.

Embu soma hiki

1. Wakati upinzani wamefanikiwa kufanya kampeni miezi 2 tu. CCM wamefanya kampeni miaka yote mi5. Yaani kila siku, mara Magufuli yupo huku, Majaliwa kule, Samia pale, Jafo Ndiyo kabisaa, Ummy Mwalimu naye kila sehemu. Safari zote hizo za "kusimamia" miradi ni kampeni. Wamefika karibia kila kona ya nchi.

Miezi miwili ya kampeni haiwezi tosha kuzunguka maeneo yote na kumwaga sera kwa ufasaha.

2. Watanzania wengi siyo watu complicated. Tupo simple, wachache ndiyo wenye uwezo wa kuchambua mambo.

Magufuli katumia miaka 5 kutuaminisha kuwa mabeberu ni watu wabaya. Miaka mitano (five years) kuonyesha msisitizo, alafu unatarajia Tundu Lissu katika miezi miwili ya kampeni, aweze kuwashawishi watu kuwa ni sawa yeye kuwa na wakili mzungu (Amsterdam) tena shoga. Haiwezekani.

3. Magufuli katumia miaka 5 kutuaminisha watanzania kuwa tunaibiwa mali asili zetu madini na wazungu. Na kuwa ni vita kubwa ya kiuchumi.

Lissu amekuja na kutarajia ndani ya miezi 2 atawabadilisha watu, Kweli? Tena anasema ataweka rehani madini kwa hao wazungu ili apate hela ya maendeleo wakati Magufuli akaweka sherehe ya kupokea Bil 100 kutoka Barrick siku chache kabla ya uchaguzi.

Kwa hili, Magufuli akafanikiwa kuwaonyesha watu kuwa sera ya kuweka rehani madini ni mbaya maana mbona tumeanza kupokea gawio la Bil 100?

Jamaa mjanja sana.

4. Miaka mi 5 yote, Serikali ya Magufuli imepambana kutengeneza uhusiano mzuri na viongozi wa dini zote. Katika kila uzinduzi, kila mkutano, viongozi wa dini wamealikwa na kuhudhuria. Na amehakikisha Kija Jumapili amehudhuria kanisani.

Kama unavyojua, watanzania wengi hasa vijijini ni wapenda dini.

Alafu unatarajia kutumia viongozi wawili watatu kwenye kampeni ya miezi 2 utaweza kuwa shawishi watanzania wengi waachane na mtu wanaye muona anaunga mkono dini? ni miss calculations kubwa sana.

5. Ni lazima upinzani uache kuangalia na kutunga sera za watu wachache wa mjini na kuangalia Watanzania wengi kwa mapana.

Sera ya Huru, haki na demokrasia ni sera nzuri lakini, inawagusa watu wachache.

Binadamu wengi ni Tomaso. Kwa wale wasiyoelewa, Tomaso ni kuwa mpaka uone ndiyo uamini.

Katika hili, mpaka janga la kukosa uhuru au haki inayotokana na serikali (CCM) limkute, hataona wala kuelewa maana ya huru, haki na demokrasia.

Haswa ukilinganisha na idadi gani ya watanzania walioguswa na kuielewa sera ya Elimu Bure, vituo vya afya, ujenzi wa barabara, reli, vivuko na kadharika.

Uongozi wa Upinzani hapa imechukua kero na matatizo walionayo wao ya kushitakiwa na kupelekwa mahakamani kila siku kuwa ni tatizo la watanzania wote. Hivyo wakaja na sera ya Huru, Haki na Demokrasia. Kwa hili wame zingua sana.

Kiukweli, ukiweka ushabiki pembeni, nakuangalia kwa makini hizo Point, unaona kabisa kulikuwa hakuna uwezekano wowote wa Lissu kuchukua nchi mwaka huu.

Kama bado unadhani hivyo, siyo ishu. Kuna maisha baada ya uchaguzi. Wacha tupambane na hali zetu. Tukatane tena 2025.
 
Ki ukweli, kama wewe kwa akili zako zooote, umekaa na kuwaza, ukafanya utafiti na jibu ulilopata ni kuwa Lissu angechukua nchi uchaguzi huu, walahi wewe ni KILAZA...
Lissu hakushindwa, Magu kaiba uchaguzi, mimi najuwa hivyo, wewe unajuwa hivyo na wengine wote wanajuwa hivyo. Simple and clear. Msitupotezee muda wa kusoma gazeti zima.
 
Ki ukweli, kama wewe kwa akili zako zooote, umekaa na kuwaza, ukafanya utafiti na jibu ulilopata ni kuwa Lissu angechukua nchi uchaguzi huu, walahi wewe ni KILAZA...
Nina mashaka na uwezo wako wa kufikiri. Unatumia makalio badala ya kichwa.
FB_IMG_16032145903427749.jpeg
 
Wapinzani hawataki kuelewa.

Ishu ya ushoga nilikuwa naiona ni ndogo. Ila baada ya kuzungumza na watu hasa upinzani ni hawaikubali. Naamini hio pia imechangia kumporomosha.
 
...
Uongozi wa Upinzani hapa imechukua kero na matatizo walionayo wao ya kushitakiwa na kupelekwa mahakamani kila siku kuwa ni tatizo la watanzania wote. Hivyo wakaja na sera ya Huru, Haki na Demokrasia. Kwa hili wame zingua sana. UBINAFSI NA UCHU WA MADARAKA
. .

Ni aya moja tu, hiyo hapo juu, ya bandiko lako imehitimisha kosa alilolifanya Lissu na hatimaye kufanikiwa kuuzika kabisa upinzani Tanzania. Hata mizunguko yake ya kutafuta wadhamini, huku akifanya kampeni kinyume na sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi, hakuitumia ipasavyo. Aliendelea kuibeza serikali kwa kushughulikia kero za wananchi za maendeleo.

It was the ”Means to an End". Ama zake ama zangu, Lissu alisema hadharani kuhusu Mgombea Urais kupitia CCM, ambaye kaibuka kidedea kwa chama chake kuzoa viti 262 kati ya 264 na kura za Urais 12,516,252 wakati Tundu Lissu akiambulia kura 1, 9 33, 271.

Apeleke madai yake "The Hague" tu kuwa Uchaguzi hakuwa "Huru na wa Haki", wakati yeye alitumia kampeni zake kuubomoa upinzani kwa lugha yake ya matusi, tuhuma na majivuno
 

Acha pumba za kutafuta mchawi mzee; wagombea walikuwa wengi sana kutoka vyama mbalimbali. Kwa nini wewe utumie matokea ya wagombea wa CCM na chadema tu kutoa conclusion? Halafu inawezekana kabisa mtu kumpigia kura rais na asimpigie mbunge yeyote kama hakubaliani nao wote. CHADEMA ijipange upya tena, na itabidi ilie sana kwa kumkosa Slaa ambaye ndiye aliyeipaisha kufikia kilelelni, Electoral politics inahitaji ku grassroots kushikamana na wapiga kura, siyo mihemko ya uanaharakati kwenye mitandao.

Tangu Slaa aoandoke, sijawahi kuona Katibu Mkuu aki-organize chama huko vijijini, wao wanachotaka ni maandamanao na mikutano mikubwa ya hadhara lakini hiyo siyo namna ya kuendesha organization ya chama cha siasa, ni mambo ya uanaharakati ambayo watanzania wengi hawakubaliani nayo kwani uanaharakati ni kuingiliana na mambo ya usalama ambayo hukaribisha polisi.

Kuna watu hapa tuliwahi kuwaonya viongozi wa chadema wawe wanazungummzia mambo ya "bread and butter" wao wanakuja na matusi na haki za binadamu kama vile hiyo ndiyo kiu ya raia. Muda wote Mbowe na wafuasi wake wakuu Lema, Bulaya, Matiko, na Mdee wao walikuwa kuendeleza vurugu tu dhidi ya vyo,mbo vya sheria kutafuta huruma ya wananchi, lakini ime-backfire. Ukipanda bange utavuna bange.
 
Ki ukweli, kama wewe kwa akili zako zooote, umekaa na kuwaza, ukafanya utafiti na jibu ulilopata ni kuwa Lissu angechukua nchi uchaguzi huu, walahi wewe ni KILAZA...

TUME HURU YA UCHAGUZI mengine yote sawa je kuhusu Tume huru ya Uchaguzi hili vipi nalo?
 
Back
Top Bottom