Sababu ya kuzidii kwa ujambazi, wizi, na maovu mengine katika jeshi la Polisi ni hii hapa.

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
Wadau- kama tunavyishuhudia siku hizi polisi wanashindana na raia wa kawaida katika kufanya vitendo vya ujambazi, wizi, mauaji nk nk ingawa wao ndiyo wanatakiwa kulinda raia.

Habari za juzi za IGP Mwema, bosi wao mkuu kabisa kuibiwa upanga wa dhahabu unadhihirisha jinsi jeshi letu kuanzia juu kabisa hadi chinilimeoza. Mtu aibe kitu kutoka ofisi ya IGP? Naye (IGP) hata haoni aibu kujiuzulu? (Anyway kwa huyu Mwema kutoona aibu ni kawaida, kwani si mnakumbuka 2002 pale mahabusi 35 walipokufa kwa kukosa hewa kule Mbarali baada ya kufungiwa katika chumba kidogo bila ya kuwepo madirisha ya kutosha?) Mwema alikuwa RPC Mbeya.

Lakini sasa hivi kidogo twaanza kuelewa kwa nini katika jeshi letu la polisi kumeongezeka wimbi la maovu na uharamia wa kila aina -- ni kwa sababu hakuna wa kuwawajibisha na hii inatokana na kwamba nao wanatarajiwa, au wameagizwa kufanya kazi moja tu, kudhalilisha wapinzani kila pale sababu inapojitokeza, hata kama sababu yenyewe ni ndogo au isiyokuwa na msingi.

Kwa utawala wa CCM ambao umefikia mahala ambapo wanazidiwa sana na hoja za wapinzani, basi silaha yao kubwa ni kutumia polisi ili eti kuonyesha raia kuwa hawa ni watu wa vurugu tu. Ajabu ni kwamba mbinu hii walianza kutumia tangu zamani -- kwa NCCR, CUF na sasa CDM. Kwa CCM vyama vyote ambavyo huwa tishio kwa uhai wao, basi ni lazima vionyeshwe kwa umma kwamba ni vyama vya vurugu kwa sababu kihoja CCM haiwezi kuzijibu zile za upinzani.

Maneno 'uvunjifu wa amani' ndiyo umekuwa mwongozo mkuu kwao -- utadhani amani katika nchi huwa inasimikwa na jeshi la polisi. Ingekuwa hivyo, basi kusingekwa na vita katika nchi mbali mbali duniani, kwani si yapo majeshi ya polisi pia?

Hivyo basi wimbi la wizi, ujambazi, uharamia unaofanywa na polisi ni kama asante yao kutoka kwa utawala wa CCM kwa matarajio kwamba waendelee 'kuwadhalilisha viongozi wa upinzani.

Nawasilisha.
 
Nakubaliana na mtoa hoja. Siku hizi polisi wanafanya watakavyo pamoja na mauaji, mradi wasiache kumtumikia Bwana kwa kuwwadhalilisha akina Mowe. Lakini yana mwisho.
 
swala la polisi kufanya uovu ni kutokana na kukosa maisha mazuri yaani mshahara mzuri sehemu ya kulala nzuri na sio mabanda ya ya full suti yaani bati nyumba nzima hii itawapelekea kutojiingia kwenye uahalifu.

chengine ni elimu waliowengi polisi ni la saba C yaani kafoji cheti cha form ilituamalizie maisha huko polisi cha mwisho ni yale mambo ya "wewe mlete tu atazoea" ndio pia nao ni mwiba zaidi..
 
swala la polisi kufanya uovu ni kutokana na kukosa maisha mazuri yaani mshahara mzuri sehemu ya kulala nzuri na sio mabanda ya ya full suti yaani bati nyumba nzima hii itawapelekea kutojiingia kwenye uahalifu.

chengine ni elimu waliowengi polisi ni la saba C yaani kafoji cheti cha form ilituamalizie maisha huko polisi cha mwisho ni yale mambo ya "wewe mlete tu atazoea" ndio pia nao ni mwiba zaidi..
Sidhani kama elimu yao duni na ugumu wa maisha vinachangia kufanya uovu na wizi. Kwani wanawaibia kina nani? Si watanzania, ambao maisha yao ni magumu? Maisha ni magumu kwa kila mtu na isiwe mwavuli wa kufanya uovu.
Tatizo linaanza na uongozi. Wamepita ma IGP wengi kwenye taifa letu. Hajawahi kutokea dhaifu kama aliyepo. Nadhani huyu ni mzuri wa kulipiza visasi na kufanya majanga, yaani ku plan michezo ya kisiasa kama ya Mwigulu, kutungia watu kesi hewa na kuwatisha watu kwa mabomu. Karibu kila kusanyiko, liwe la wanafunzi, wanasiasa nahisi hata watoto anaweza kurusha mabomu. Hivyo anaangaika na mambo ambayo siyo!!
Tuangalie baadhi ya matukio ya kutisha yalotokea akiwepo, wizi hasa Dar, hakuna suruhisho, mauaji ya albino, hakuna suruhisho, watu kumwagiwa acid, hakuna suruhisho, machafuko ya kisiasa hasa mikutano ya chadema ambapo polisi ndo uanzisha fujo, hakuna suruhisho, madawa ya kulevya, hakuna suruhisho, utekaji wa mabasi hasa mkoa wa Kagera, watu kutembea ovyo na pistol vifaa vya moto na mengine yanakuja. Mabomu ya Arusha. Yote haya, IGP hana solution zaidi ya kuahidi million 100 kwa atakayemjua mharifu. Bado waandishi wa habari kuteswa, kuuwawa na kufungiwa.
Bado tu analipwa na hela ya walala hoi. Hivi huyu na JK wangechukua nchi kwa muda alotawala Nyelele, sasa hivi nchi za Somalia, Sylia, Libya, Sudan, Egypt, zingekuwa za amani ukilinganisha na Tanzania.
Hawa wanajua tu kumkamata Mbowe na Lema, basi.
Nchi zilizoendelea, watu kama hawa, hawapewi nafasi hata kidogo, na kama Rais akiamua kuwapa zawadi ya vyeo, uchaguzi ukija, raia wanampa fundisho rais, mpaka hawezi kurudia. Kwetu, watu bado wananunuliwa na kanga na kofia...yaani hayo ni malipo ya amani yao, rasilimali zao na maisha yao. Inabidi hii tabia tuiache. Tunayo nguvu ya kuwaadabisha hawa watu na wasisikike kabisa katika jamii yetu na njia hiyo ni kuweka kiongozi mwenye akili na uwezo wa kufikilia. Sasa mtu amchague Mwigulu kuwa kiongozi wa chama, Wasira kuwa na office, unategemea nini?
Vinginevyo jeshi la polisi ni zuri na imara, ni viongozi wakuu ndo wameriharibu. Ukiwa baba wa familia, ukawa mwizi na mtu wa vituko, huwezi kuwanyooshea vidole watoto wako kwa kufanya ufanyalo wewe. Hivi ndivyo jeshi letu lilivyo.
Tunahitaji tu Rais atakayeweka watu makini jeshini na kulifanyia mabadiriko kidogo. Mfano jiji la Dar halina ulinzi kabisa. Unaweza kuteka mtaa wote ukawaibia watu. Inabidi polisi wasambaze vituo vyao kulingana na mji unavyoenda na wawe na vifaa vya kurespond haraka kwenye uharifu.
Mfano nilitembelea kituo cha polisi kiko Mbezi beach. Yaani ni kajumba kadogo, humo ndani kuna polisi kama watatu. Kajumba kana vyuma (grills) kila dirisha na milangoni, sasa nikajiuliza, hawa polisi wenyewe wanaogopa kuibiwa, watalinda mali ya nani?
uchache wao, ukitokea uhalifu kilometer moja, hawawezi kuukabiri, IGP hilo halioni ila anajua Mbowe kazidisha dakika ngapi kwenye mkutano.
Ndugu zangu watanzania, uwezo wa kutoa mara moja matatizo haya, upo mikononi mwenu. Tuamue sasa kuwa watu wa kulalamika kila siku au 2015 tumwambie IGP, "you are fired" kwa njia hiyo, itakuwa ni funzo hata kwa yule atakayekuja.
 
Tusiwalaumu sana hawa viongozi wa majeshi yetu kwa kuwa remoti yao iko magogoni
Muangalie siro mambo aliyofanya au aliyopitia ni mengi ambayo mengine yalifanya watu wamshushe thamani lakini kupitia hayo ameonekana ndio mfanyakazi bora na kutunukiwa vyeo vya juu zaidi
Hii ni mbaya zaidi jeshi linakuwa kisiasa zaidi kwa nchi watu watataka vyeo
 
Back
Top Bottom