Uchaguzi 2020 Sababu tano za kwanini sitoichagua CHADEMA Oktoba 28

Bekiri

Member
Jun 30, 2013
14
63
1. Ilani ya Chadema katika SURA ya 12.1 (a), inakusudia kuuza Nchi kwa kuweka REHANI madini yetu. Jaribio hili litaleta mgogoro mkubwa wa ardhi kati ya Wananchi na watakaopewa madini hayo kwa dhamana wakati wa matumizi ya ardhi kwa kuwa madini yapo chini ya ardhi na wakati wote wa REHANI ardhi yenye madini haitoruhusiwa kutumika kwa shughuli yoyote.

Si ajabu maeneo yenye madini yakawekewa UZIO na ulinzi wa hali ya juu. Mgogoro utakua mkubwa, maumivu ya watu wanaozunguka maeneo ya madini yataongezeka, Utumwa utashamiri, risasi zitakuwa hadharani na dhiki itatapataa ktk nchi hii. Kwa sababu hii SITOICHAGUA Chadema Oktoba 28.

2. Ilani ya Chadema katika SURA ya 12.1 (b) inakusudia kuirudisha nchi ktk UFISADI wa kutupwa kupitia mradi wa UMEME kwa kurudisha matumizi ya Sekta binafsi ktk uzalishaji na usambazaji wa UMEME nchini.

Nchi hii bado ina MAKOVU makubwa katika uwekezaji wa UMEME kupitia Sekta binafsi. Simulizi ya RICHMOND NA IPTL bado zinatuumiza hivyo kurejesha tena utaratibu huo ni kutengeneza mwanya mwingine wa KUFISADI pesa za Wananchi wetu. Nchi yetu imehama hatua hiyo, kwa sababu hii SITOICHAGUA Chadema katakata kwani kuichagua ni kuchagua UFISADI.

3. Ilani ya CHADEMA sura ya 3.5 (a) inasema itafuta MUUNGANO wa Serikali mbili na kuunda TATU. Uzoefu unaonesha kuwa Serikali tatu haziwezi kudumu kutokana na mgogoro wa maslahi baina ya Serikali shiriki na ile ya Muungano.

Jaribio hili linakusudia KUUUA kabisa Muungano na kuzitenganisha Tanganyika na Zanzibar. Huu utakua mwanzo wa vurumai kati ya Tanganyika na Zanzibar, kwa sababu hii Umoja wetu utapotea, maafa yatakaribia na Amani itaadimika katika Nchi yetu. Kwa ajili ya MUUUNGANO, AMANI na MSHIKAMANO baina ya Nchi zetu nakuomba usiichague CHADEMA asilani, utakuja kunishukuru. Kuichagua Chadema ni KUVUNJA Muungao wetu!!

4. Ilani ya Chadema haina UTAFITI wowote wala ufafanuzi wowote juu ya changamoto yoyote ktk nchi hii. Kwa mfano, changamoto ya MAJI, haielezwi ukubwa wake, mahitaji yaliyopo na taratibu za utatuzi wa changamoto hiyo. Ukimya huu ktk Mkataba wa miaka mitano (ILANI) ni ukwepaji wa wazi wa wajibu ili kuepuka kuwajibika. Siwezi kuchagua ILANI isiyobainisha changamoto zinazonihusu kwa ukubwa wake na utatuzi wake. Sitoipigia KURA Chadema!! Watakula walikopeleka mboga.

5. Mgombea wa Urais wa Chadema anahubiri UDINI, UKAIDI WA SHERIA na UVUNJIFU wa AMANI. Kauli zake na zile za mfuasi wake Shekhe Ponda ni ushahidi wa wazi wa machafuko siku za usoni.

Tangu zamani hata sasa Nchi yetu imekua ya AMANI na UTULIVU mkubwa kwa jitihada za CCM. Dalili zinazoonekana sasa zisipochukuliwa hatua ya haraka Taifa litavunjika na kuparaganyika. Amani na Umoja wetu vitakufa, nchi itavuja damu kwa UDINI na matabaka. Kuchagua CHADEMA ni kuchagua machafuko ktk nchi, vurumai na mapigano bila sababu. Mimi SITOICHAGUA Chadema kwa ajili ya AMANI ya Nchi yetu.

Mimi nitaichagua CCM kwa sababu imedumisha Amani na Utulivu kwa muda mrefu. Aidha, nitaichagua CCM kwa sababu imebeba dira ya maendeleo ya TAIFA letu na UHAI wa MUUNGANO wetu.
Oktoba28, Piga Kuwa kwaCCM.
#NiMitanoTenaKwaJPM.
 
Mbona sasa hivi madini yote yamebebwa na mabeberu.

Magufuli na genge lake la ccm wameyauza madini yote tumeachiwa vumbi na mashimo.

Geita Gold mine imegeuka kuwa pango la walanguzi. Ndege zinaingia na kutoka mgodini kana kwamba nchi hii ni ya wazungu. KWISHA HABARI PALE.

Miaka sitini ya uhuru bado ccm inahubiri kujenga visima.

Visima vilipaswa kuwa vimekamilika miaka ya sabini huko.

Leo 2020 bado tu wanaimba maji. Huu ni upuuzi.

Kama mmeshindwa kuisaidia nchi kaeni kando, msitupotezee muda.

Maisha ni mafupi sana hatuwezi kusubiri kisima cha maji kwa miaka sitini.
 
1. Ilani ya Chadema katika SURA ya 12.1 (a), inakusudia kuuza Nchi kwa kuweka REHANI madini yetu. Jaribio hili litaleta mgogoro mkubwa wa ardhi kati ya Wananchi na watakaopewa madini hayo kwa dhamana wakati wa matumizi ya ardhi kwa kuwa madini yapo chini ya ardhi na wakati wote wa REHANI ardhi yenye madini haitoruhusiwa kutumika kwa shughuli yoyote.

Si ajabu maeneo yenye madini yakawekewa UZIO na ulinzi wa hali ya juu. Mgogoro utakua mkubwa, maumivu ya watu wanaozunguka maeneo ya madini yataongezeka, Utumwa utashamiri, risasi zitakuwa hadharani na dhiki itatapataa ktk nchi hii. Kwa sababu hii SITOICHAGUA Chadema Oktoba 28.

2. Ilani ya Chadema katika SURA ya 12.1 (b) inakusudia kuirudisha nchi ktk UFISADI wa kutupwa kupitia mradi wa UMEME kwa kurudisha matumizi ya Sekta binafsi ktk uzalishaji na usambazaji wa UMEME nchini.

Nchi hii bado ina MAKOVU makubwa katika uwekezaji wa UMEME kupitia Sekta binafsi. Simulizi ya RICHMOND NA IPTL bado zinatuumiza hivyo kurejesha tena utaratibu huo ni kutengeneza mwanya mwingine wa KUFISADI pesa za Wananchi wetu. Nchi yetu imehama hatua hiyo, kwa sababu hii SITOICHAGUA Chadema katakata kwani kuichagua ni kuchagua UFISADI.

3. Ilani ya CHADEMA sura ya 3.5 (a) inasema itafuta MUUNGANO wa Serikali mbili na kuunda TATU. Uzoefu unaonesha kuwa Serikali tatu haziwezi kudumu kutokana na mgogoro wa maslahi baina ya Serikali shiriki na ile ya Muungano.

Jaribio hili linakusudia KUUUA kabisa Muungano na kuzitenganisha Tanganyika na Zanzibar. Huu utakua mwanzo wa vurumai kati ya Tanganyika na Zanzibar, kwa sababu hii Umoja wetu utapotea, maafa yatakaribia na Amani itaadimika katika Nchi yetu. Kwa ajili ya MUUUNGANO, AMANI na MSHIKAMANO baina ya Nchi zetu nakuomba usiichague CHADEMA asilani, utakuja kunishukuru. Kuichagua Chadema ni KUVUNJA Muungao wetu!!

4. Ilani ya Chadema haina UTAFITI wowote wala ufafanuzi wowote juu ya changamoto yoyote ktk nchi hii. Kwa mfano, changamoto ya MAJI, haielezwi ukubwa wake, mahitaji yaliyopo na taratibu za utatuzi wa changamoto hiyo. Ukimya huu ktk Mkataba wa miaka mitano (ILANI) ni ukwepaji wa wazi wa wajibu ili kuepuka kuwajibika. Siwezi kuchagua ILANI isiyobainisha changamoto zinazonihusu kwa ukubwa wake na utatuzi wake. Sitoipigia KURA Chadema!! Watakula walikopeleka mboga.

5. Mgombea wa Urais wa Chadema anahubiri UDINI, UKAIDI WA SHERIA na UVUNJIFU wa AMANI. Kauli zake na zile za mfuasi wake Shekhe Ponda ni ushahidi wa wazi wa machafuko siku za usoni.

Tangu zamani hata sasa Nchi yetu imekua ya AMANI na UTULIVU mkubwa kwa jitihada za CCM. Dalili zinazoonekana sasa zisipochukuliwa hatua ya haraka Taifa litavunjika na kuparaganyika. Amani na Umoja wetu vitakufa, nchi itavuja damu kwa UDINI na matabaka. Kuchagua CHADEMA ni kuchagua machafuko ktk nchi, vurumai na mapigano bila sababu. Mimi SITOICHAGUA Chadema kwa ajili ya AMANI ya Nchi yetu.

Mimi nitaichagua CCM kwa sababu imedumisha Amani na Utulivu kwa muda mrefu. Aidha, nitaichagua CCM kwa sababu imebeba dira ya maendeleo ya TAIFA letu na UHAI wa MUUNGANO wetu.
Oktoba28, Piga Kuwa kwaCCM.
#NiMitanoTenaKwaJPM.
Una tatizo la msongo wa mawazo..kunywa Pepsi bariid,inaondoa MAWAZO

Sent from my M100 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom