Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Kuna taarifa kutoka kwa polisi wenyewe kwamba wanaona aibu kuonekana kwa kuhofia macho ya watu au hata kuzomewa. Ambao hawawezi kukwepa ni traffic polisi na wale wanaolinda benki na majengo ya wakubwa.Taarifa zinadai kwamba polisi wengi wa arusha siku hizi wanakwenda kazini wakiwa na mabegi madogo au mifuko ya rambo. Kwenye begi kunakua na sare. Wakifika kituoni wanavaa hiyo sare, kama ambavyo manesi wanafanya siku hizi. wakitoka kituoni wanavaa kiraia.