Sababu Kuu za Watanzania Kupinga Tozo Mbalimbali

Umkonto

JF-Expert Member
Dec 27, 2018
2,102
3,613
Hili halina ubishi, Watanzania wengi wanapinga ongezeko la tozo mbalimbali kuanzia kwenye mafuta mpaka kwenye miamala ya simu. Hii tabia ya kupinga haijaja ghafla, bali ni matokeo ya muda mrefu.

Sababu kubwa zinazowafanya Watanzania kupinga tozo hizi, ni kukosekana kwa uwazi (Transparency) na uwajibikaji (Accountability) katika nchi kwa muda mrefu. Haya masuala yanaonekana ni madogo ila ndiyo yametufikisha hapa.

Kwa mfano, miaka na miaka, wananchi wamekuwa hawawekwi wazi kuhusu mambo yanayohusu nchi kama vile; ukopaji na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya nchi. Mnamkumbuka yule aliyekuwa anasema, "leo tunajenga kwa fedha za ndani", kesho anasema "tunakopa kwa faida".

Kuhusu accountability, kuna baadhi ya maeneo ndani ya nchi yana hali ngumu sana kimaisha, mfano, hakuna umeme, maji, barabara nk.

Kukosekana kwa mambo haya mawili (transparency and accountability) kumewaathiri sana Watanzania kisaikolojia, hivyo kutokubali kirahisi rahisi tozo zinazoongezeka, hata kama zina nia ya dhati ya kuliendeleza taifa.

Wananchi wangekuwa wepesi kuzikubali tozo, endapo tangu zamani wangekuwa wanaona matokeo chanya katika maisha yao. Leo, hii mwananchi haiamini serikali, kwa sababu anaona kama inamdanganya pale inaposema tunaongeza tozo ili kujenga barabara za vijijini. Hii ni kwa sababu, kwa miaka mingi mwananchi huyu amekuwa akiishi maisha magumu na anaiona serikali haina msaada kwake.

Wito wangu kwa viongozi, tuwe na uwazi na uwajibikaji kwa wananchi, ili huko mbeleni iwe rahisi kuwachangisha wananchi.

Leo, mnasema mmeongeza tozo ili kupata hela ya kujenga barabara za vijijini na mijini zenye ubora. Najua hilo limeishapita na Watanzania watazoea, ila sasa hizo barabara zijengwe jamani. Wananchi siyo wajinga kihivyo. Mwaka 2025 wananchi watawauliza kama hamtakuwa mmezijenga hizo barabara.

Watanzania tubadilike. Madhara ya kukosa uwazi na uwajibikaji wa serikali ni makubwa sana, kama inavyoonekana sasa. Hakuna kuaminiana tena Tanzania kati ya serikali na wananchi, kwa sababu huko nyuma wananchi waliisha-experience maumivu, rejea: escrow, richmond, epa, etc. Leo hii wananchi wanaona hizo tozo zinaenda kuwanufaisha viongozi wa serikali hata kama si kweli. Ni kwa sababu wananchi waliishapigwa sana huko nyuma.
 
Njia rahisi ambayo inaweza kutumiwa na serikali, ili wananchi waielewe hii bajeti, ni wabunge kujipunguzia posho na mishahara.

Hakika hili likifanyika, utawaona wananchi wakipunguza malalamiko kuhusu hizi tozo. Lakini kinachofanyika kwa sasa ni unafiki wa wabunge. Wabunge wanapitisha mambo ambayo yanawabana wananchi, ila wao hawajibani. Tubadilike Watanzania, na tuwe kitu kimoja katika kulijenga taifa.
 
Njia rahisi ambayo inaweza kutumiwa na serikali, ili wananchi waielewe hii bajeti, ni wabunge kujipunguzia posho na mishahara.

Hakika hili likifanyika, utawaona wananchi wakipunguza malalamiko kuhusu hizi tozo. Lakini kinachofanyika kwa sasa ni unafiki wa wabunge. Wabunge wanapitisha mambo ambayo yanawabana wananchi, ila wao hawajibani. Tubadilike Watanzania, na tuwe kitu kimoja katika kulijenga taifa.
Na sio tu mishahara ipungue.. Walipe na kodi zote zakiserikali mishahara ikatwe paye, kodi ya uzalendo, mifuko ya Jamii,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaletaje tozo kiubwegebwege ivo wakati ajira hamtoi umebaki km wimbo wa Taifa? Visent vya mtaji wa nyanya na vitunguu kwenye magenge yetu ndo mnataka mvikwapue huoni ni ubwabwazu mtupu?

Unataka nikuchangie harusi yako hakikisha tunafahamiana sio unikute kwenye daladala unitupie likadi lako lenye mchango usiopungua elfu80 utazani uliiweka.
 
Ninaunga mkono hoja, hasa ile budget ya ofisi ya Rais inawekwa siri na CAG haruhusiwi kuikagua, lile ndiyo fuko la maovu mengi.
Na ili fuko hakuna wakuligusa zaidi ya katiba mpya!!!! Ila kiukweli Tanzania ni nchi yangu ila kuna time unatamani ujipoteze.... Yani hawa viongozi waanshidwa kabisa kujali raia wao...!!! Wao wanalipana mahela mengi, wao wanaendeshwa na magari mazuri, wanaishi vzuri na familia zao then kwenye kulichangia taifa sisi raia ndo tuchangie taifa!!! Mwigulu kama kweli unapenda uzalendo anza wewe kuwa mfano achana na viette tembelea Cruiser lx ili kupunguza cost!!! Ivi hawa jamaa viongozi hawaoni kweli kuna umuhimu wa wao kubana matumizi ili serikali iwe na pesa???? Wanarudi kwa raia ambao kipate chai kwa siku buku wanapita nayo kwenye uzalendo.... Sawa tunakubali kuwa wazalendo na nyie muachie izo nyazifa vjana.... Mwigulu ebu jaribu kujiuzulu uje uku mtaani tupambane kiume yani ile kula kwa jasho... Huwezi kufeel maumivu wakati unaishi kwa kodi zetu... Na bado unaleta zarau etu tukaishi burundi we mzee uko sawa sawa kweli kichwani? Burundi ndo tulipo ziliwa? Tunataka wewe uwache iyo kazi yenye posho, jiuzulu ubunge, acha nafasi zote za kiserikali then karibu kwenye uzalendo
 
Back
Top Bottom