Sababu kuu ya ajali za barabarani Tanzania ni hii hapa!!!

pageup

Senior Member
Oct 12, 2012
156
59
pamoja na uzembe wa madereva kuchangia katika asilimia kubwa sana ya ajali za magari barabarani,na kusababisha vifo vya maelfu ya raia wasio na hatia yoyote sasa tunakuletea sababu moja wapo ya msingi ya kukithiri kwa ajali siku za hivi karibuni:
AJALI YA GARI T 601 APK BARABARA YA KOROGWE MORO MISITU PIX NO 2.JPG
madereva wengi sana wanaojifunza gari mijini(dar-arusha-tanga)wakishapata lessen tu,huwa na mzuka wa kukata masafa marefu na gari zao au za kuazima,kimatembezi,au kwa shida nyengine yoyote ile!!bila kuweka katika akili zao kuwa barabara zote zinazokwenda mikoani huwa zinamisukosuko ya aina mbali mbali!!
1:inahitaji uwe mzoefu wa hali ya juu katika ku overtake
2:inatakiwa ujuwe sehemu za ku overtake au kuto overtake ili kujiepusha na ajali
3:uwe na uvumilivu wa kukwepa makosa ya madereva wengine,ili kujiepushia ajali
4:masafa ya km200-1200km si sawa na 20km au 15 km,safari ndefu zinataka angalau ukae kushoto hata mara mbili
5.jpg
barabara zetu za mikoani zina changamoto mbali mbali unapoendesha gari majira ya usiku huwezi kuyaepuka kama wewe si dereva mzoefu wa njia hizo!!!
1:kuna gari nyingi usiku huwa zinatembea na taa moja tu,unaweza ukadhani pikipiki ukiibana imekula kwako!
2:kuna matreckta yanavuta matela nyakati za usiku bila kuwa na ishara yoyote,na ajali nyingi hutokea hapo!!
3:kuna madereva wanaowasha taa zenye mwanga mkali bila kuzizima,hivyo kukusababishia kupata ajali!
DSC2936-web60-copy.jpg
ninachopenda kuwaeleza madereva wa mjini muliokuwa hamuna idea na barabara za mikoani,kabla ya kuchukua maamuzi ya kuhatarisha maisha yako au ya familia yako,unapotaka kukata masafa marefu ya mikoani hali ya kuwa huna idea ya marabara za huku,ajiri dereva akuendeshe angalau tripu mbili au tatu,upate uzoefu,na muchangie katika kutupunguzia ajali,ambazo sisi wakazi wa mikoani tunaona madereva wengi wanaotusababishia ajali nyingi hutokana na kutokuwa wazoefu wa njia zetu!!!!!!
 
Asante sana kwa maelekezo yako mkuu
madereva wengi aise haswa usiku ni balaa haswa wa magari makubwa
Wengine wanakuwa wanadrive huku wamesinzia maana unapishana na lori liko katikati ya barabara na amewasha full light hakjali kama kuna wengine wanaumizwa na mwanga wa hizo taa
Wanaovertake vibaya na kwenye corner za hatari na madaraja bila kujali watumiaji wengine wa barabara
Uendeshaji wa gari kwa kweli unahitaji umakini mkubwa sana na bora kudrive speed nndogo uchelewe kufika kuliko kudrive speed kubwa na uwahi kuitwa marehem maana waweza kuwa makini ila ukakutana na dereva ambaye hamnazo akakufanya asusa
 
Ni kweli unayosema, kufanya safari ya masafa inatakiwa uwe na uzoefu wa kutosha.Kwanza hata macho kuangalia lami muda wa masaa matatu au manne huwainafikia yanachoka na hatimaye kupelekea usingizi wa ina flani ambao unaweza ukapelekea gari kutoka nje ya barabara.
 
Tunashukuru kwa darsa. Wengi wa madereva wa mijini hawapati nafasi ya kukimbiza sana magari kutokana na misongamano ya magari na ufupi wa safari hivyo wakiambiwa kuenda masafa basi wanawaza kuitafuta 140, 160, 180km/h. matokeo yake hafiki mbali. kama unahamu ya kuona spidi panda ndege uone inavyokimbia wakati wa ku take off.
 
View attachment 72660
Duh huyu dereva ana hatari sana,una overtake mlimani afu na nissan diesel kwa scania
this is more than danger

Huu ni mlima kitonga naujua kama sala. hapa huwezi kuwa safe kama huwezi kuendesha kama huyo mwenye basi.

Huu mlima una kona mithili ya nyoka halafu ni mkali sana(very steep). ukiendesha nyuma ya lori unaona kama linaweza rudi nyuma either kwa kukosa nguvu au kuisha upepo lika feli brake.

You dont have any other alternative Buddy.

Binafsi hapa nimekoswa koswa mara Mbili. its such a dangerous place.

Haya ndio maeneo watu waliozea kuendesha mjini tu si washauri kabisa kujaribu.
 
Huu ni mlima kitonga naujua kama sala. hapa huwezi kuwa safe kama huwezi kuendesha kama huyo mwenye basi.

Huu mlima una kona mithili ya nyoka halafu ni mkali sana(very steep). ukiendesha nyuma ya lori unaona kama linaweza rudi nyuma either kwa kukosa nguvu au kuisha upepo lika feli brake.

You dont have any other alternative Buddy.

Binafsi hapa nimekoswa koswa mara Mbili. its such a dangerous place.

Haya ndio maeneo watu waliozea kuendesha mjini tu si washauri kabisa kujaribu.

Hapo sio kitonga mkuu,hapo ni mlima sekenke ukiwa unauanza kama unatokea igunga!!
 
Mlachake uko salama mkuu
Za masiku kibao aise
Dah kitonga na sekenke ni balaa aise
 
Last edited by a moderator:
mkuu umenena!naongeza unapopishana na lori ujue kuna super feo ya songea nayo ina overtake hivyo punguza mwendo
 
Inaoneka ndugu huijui Iyovi, hayo ni maisha ya kawaida kabisa hao jamaa wa mabasi eneo hilo

Iyovu ndio nini mkuu?ni kweli siijui
hata kama wanafanya hivyo ni hatari sana assume kuna gari nyingine inashuka
si balaa hilo!
 
Duh! na wewe jiografia kabisa, sekeke ukitokea sherui unapandisha, hapo wanashuka sasa itakuwaje sekenke?anayesema kitonga inaweza kuwa sawa, ila hiyo barabara ni ya lami, kitonga siku hizi kuna zege... hi
Hapo sio kitonga mkuu,hapo ni mlima sekenke ukiwa unauanza kama unatokea igunga!!
 
Iyovi ni kipande ya barabara kutoka mikumi kabla ya kufika ruaha mbuyuni, hapo ukiendesha gari machana ni hatari sana
Iyovu ndio nini mkuu?ni kweli siijui
hata kama wanafanya hivyo ni hatari sana assume kuna gari nyingine inashuka
si balaa hilo!
 
Duh! na wewe jiografia kabisa, sekeke ukitokea sherui unapandisha, hapo wanashuka sasa itakuwaje sekenke?anayesema kitonga inaweza kuwa sawa, ila hiyo barabara ni ya lami, kitonga siku hizi kuna zege... hi

Unapoinza kitonga ina lami siku hizi. angalia vizuri pembeni pia kuna zege
 
Mr Rocky nipo. mambo yamepandiana tu lakini hayajagandana. kumbu unaijua kitonga. pale ni noma kaka


Ile njia nimepita sana mkuu Mlachake wakati nasoma mikoa ya huko nyanda za juu kusini aise karibu miaka miwili mizima napita kila mwando wa mwaka katikati ya mwaka na mwisho wa mwaka kwenda na kurudi
Dah tusitupane hivyo mkuu
Na ni sawa na sekenke nimepita sana ile milima wakati wa barabara ikiwa bado unapita kwenye milima na sasa japo hata hivyo maeneo yale ya sekenke kwa sasa ni balaa maana yamaeharibika mbaya
 
Last edited by a moderator:
pita kitonga alafu hiwe usiku nibalaa..unaomba Mungu tu uvuke salama..zamani ilikuwaga sekenke..alafu shida ya watanzania tumekwisha kuona ajari za barabarani ni jambo la kawaida kumbe siyo.
 
Ile njia nimepita sana mkuu Mlachake wakati nasoma mikoa ya huko nyanda za juu kusini aise karibu miaka miwili mizima napita kila mwando wa mwaka katikati ya mwaka na mwisho wa mwaka kwenda na kurudi
Dah tusitupane hivyo mkuu
Na ni sawa na sekenke nimepita sana ile milima wakati wa barabara ikiwa bado unapita kwenye milima na sasa japo hata hivyo maeneo yale ya sekenke kwa sasa ni balaa maana yamaeharibika mbaya

Uko juu Mr. Rocky.

Enzi hizo nafanya kazi Iringa weekend naenda kunywa beer Dar. yaani wacha mchezo. Ndio tulikua tunaendesha spidi zote zikiisha tunakopa. ha ha ha ha ha.

Namshukuru Mungu tu nipo salama kwa sasa. ila ujana maji ya moto meeen.
 
Back
Top Bottom