Sababu kuu kwanini hakuna aliyewajibishwa hadi sasa kuhusu sakata la escrow

Hofu-less

JF-Expert Member
May 19, 2014
519
1,026
Pengine watanzania wanatega masikio kusikia "mawaziri wapya" na watendaji wengine kuwajibishwa lakini kwa utafiti wangu niliofanya nimegundua sababu za kuchelewa huko.

1. Sakata zima la escrow limeibuliwa na wapinzani sasa kama Rais atakubali kuwawajibisha ni kama amekubali kuongozwa "kuburuzwa" na wapinzani.

2. Uchaguzi huu wa serikali za mitaa. Pengine Rais anangoja upite kwanza huu..

3. IMPACT YA WATUHUMIWA kwa uchaguzi ujao.. pia hii inaleta delay hii maana watuhumiwa wengine wamesema "watamwaga mboga" pengine itahitajika "hekima" ya namna ya kuwapumzisha bila kuleta "madhara" kwenye chama mwakani.

4. Rais mwenyewe.. hapa Rais anajisikia "hatia" na pengine na "aibu" ya kubadili badili watu katika kipindi chake..

5. Muda uliobaki.. pia tuelewe umebaki muda mchache kupata viongozi wengine kupewa ofisi...

6. Nani atafaa kuchukua nafasi zao?

Kwa hiyo pengine tukasubiri hadi miguu izamie tumboni.


cc Pasco Mzeemwanakijiji MSALANI
 
Pengine watanzania wanatega masikio kusikia "mawaziri wapya" na watendaji wengine kuwajibishwa lakini kwa utafiti wangu niliofanya nimegundua sababu za kuchelewa huko..
1.Sakata zima la escrow limeibuliwa na wapinzani sasa kama Rais atakubali kuwawajibisha ni kama amekubali kuongozwa "kuburuzwa" na wapinzani.
2.uchaguzi huu wa serikali za mitaa. Pengine Rais anangoja upite kwanza huu..
3.IMPACT YA WATUHUMIWA kwa uchaguzi ujao.. pia hii inaleta delay hii maana watuhumiwa wengine wamesema "watamwaga mboga" pengine itahitajika "hekima" ya namna ya kuwapumzisha bila kuleta "madhara" kwenye chama mwakani.
4.Rais mwenyewe.. hapa Rais anajisikia "hatia" na pengine na "aibu" ya kubadili badili watu katika kipindi chake..
5.muda uliobaki.. pia tuelewe umebaki muda mchache kupata viongozi wengine kupewa ofisi...

kwahiyo pengine tukasubiri hadi miguu izamie tumboni.
cc Pasco Mzeemwanakijiji MSALANI
Aisee umemaliza hapo pekundu.....
 
Hivi kwa maazimio yale ya mihemuko ya wanasiasa mashinikizo kutoka kwa wafanyabiasha ungekuwa wewe ndiyo rais ungefanya papara ya maamuzi?
 
kama mkataba una kinga kwa serikali wa kumbana singa singa kwa lolote litakaloonekana kukosewa na singasinga yuko tayari kulipa kodi na garama nyingine zinazohitajika. KWA NINI WAWAJIBISHWE? KAMA NI KODI NA DUE DILIGENCE SINGASINGA HAJAKATA KULIPA KAMA WATENDAJI WA KUKUTOA KODI WALIKOSEA NAO NI BINADAMU.
 
kama mkataba una kinga kwa serikali wa kumbana singa singa kwa lolote litakaloonekana kukosewa na singasinga yuko tayari kulipa kodi na garama nyingine zinazohitajika. KWA NINI WAWAJIBISHWE? KAMA NI KODI NA DUE DILIGENCE SINGASINGA HAJAKATA KULIPA KAMA WATENDAJI WA KUKUTOA KODI WALIKOSEA NAO NI BINADAMU.
Huo ndiyo ukweli ila maneno yako haya ni pigo kwa REGINALD MENGI
 
Observation yako ni nzuri ila hao ulio wa cc hao sioni kama wana la maana lolote la kuchangia. Ni wasaka tonge tu.
 
hata raisi akisuasua kuwajibishwa kwa watuhumiwa kuko palepale. maana waliotoa maamuzi ni wananchi kupitia uwakilishi wa wabunge wao.
 
JK anajisikia vibaya kuwawajibisha wale watu wake alowatuma kufanya kazi ambayo bahati mbaya limesanuka kama wasemavyo watoto mjini.
Nani awe wa kwanza kumvalisha paka kengere???????
 
Niwashauri tu waliokaribu na Rais Kikwete nadhani wangemshauri achukue hatua mapema jambo hili bado la motomoto na muda anao... Akisubiri sana sisi watanzania tutazidi kuhoji zaidi, kuchimba zaidi na kutafakuri zaidi kilichopo nyuma ya pazia., atafumua na hata yale ambayo si Bunge wala CAG na TAKUKURU hawakuyaanisha.. Akifanya sasa si tu kwa faida yake lakini pia kwa chama chake na kwa taifa kwa ujumla.. Kwa atakuwa ametua mzigo ambao aliachiwa na Bunge, chama chake kitakuwa na fursa ya kujipanga upya kwa uchaguzi mkuu ujao coz muda utakuwepo na kwa taifa kutakuwa na hali ya utulivu kwa maana ya watanzania tutakuwa angalau tumeridhika kuona Rais wetu amechukua hatua lakini pia naamin hata Wafadhali waliobana fedha za msaada wataziruhusu na hatimaye sisi walalahoi kupata huduma za jamii..

Ni kosa jingine kubwa analofanya ku-delay kwake kuchukua maamuzi, hiyo haimsaidii ni kama alivyokuwa na Tezi dume, amewahi kufanya operation na faida yake kaikimbia saratani.. sasa moyo na ari hiyohiyo ya kutibu kwa haraka tezi dume nadhani ange-apply kwenye escrow.. la sivyo utakuwa ni ujanja wa mbuni kuficha kichwa chake kwenye mchanga akidhani amejicha dhidi ya adui kumbe asilimia 98 ya mwili wake mtu aliyoko maili kumi anamwona..
 
ni bora muendelee na shughuri zenu kuliko kusubiri mabadiliko.fikra zenu ni kama biashara ya rupia
 
Mleta mada Rais hawezi kumuhukumu mtu kwa kelele zenu na huyo Mengi wenu kwanza itv wamechukua eneo lawananchi pale mikocheni
 
Back
Top Bottom