Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,769
Nimeshitushwa na taarifa ya Barrick Gold inayokanusha kwamba hawajafikia makubaliano kwamba Watailipa Tanzania, bali walichosema ni kwamba wako tayari kufanya na mazungumzo na Tanzania ili kufikia muafaka juu ya suala la Acasia.
Sasa jiulize, hivi ujumbe wa Tanzania haukuelewa walichoongea Barrick Gold hadi kukimbilia kutoa press release kwamba Tanzania italipwa fidia na Acasia? Ni aibu sana kwa press release kutoka Ofisi ya Raisi kukanushwa namna hii. Inatufanya Watanzania tuonekane hatuna akili na hatujui kiingereza.
Sasa ni wazi kwamba sababu zilizoifanya Tanzania iingie mikataba mibovu ni pamoja na zifuatazo;
Sasa jiulize, hivi ujumbe wa Tanzania haukuelewa walichoongea Barrick Gold hadi kukimbilia kutoa press release kwamba Tanzania italipwa fidia na Acasia? Ni aibu sana kwa press release kutoka Ofisi ya Raisi kukanushwa namna hii. Inatufanya Watanzania tuonekane hatuna akili na hatujui kiingereza.
Sasa ni wazi kwamba sababu zilizoifanya Tanzania iingie mikataba mibovu ni pamoja na zifuatazo;
- Kutoilewa kwa ufasaha lugha ya kiingereza na lugha ya kisheria na kimikataba wakati wa mazungumzo na wawekezaji
- Kutoilewa sekta inayohusika katika huo mkataba (mfano madini, mafuta, usafirishaji wa anga, uzalishaji umeme, nk)
- Rushwa za moja kwa moja na kulainishwa kwa zawadi kubwa na ndogondogo
- Kuwathamini sana wazungu na kuamini kila wanachosema wanapodai wanaweka maslahi ya Tanzania mbele na ushirikiano
- Kutokuwa na uzoefu wa kufanya mazungumzo (negotiations) yanayohusu mikataba ya kimataifa
- Kushinikizwa na viongozi wa juu, na hasa Ofisi ya Raisi
- Kutokuwa na uzalendo na Tanzania